Jumamosi, 29 Desemba 2012

HARUSI YA ELIZABETH NA YOHANA ALLEN

Aliyependeza namna hii ni mwimbaji wa Tanya Prise & Worship Team ya jijini Tanga akisema neno siku ya harusi yake 

Mheshimiwa Yohana Allen akilishwa kiapo na  Mchungaji Georgre Nywage siku ya alipofunga ndoa na Eliza.

wanaoonekana kwa mbele ni wapambe wa harusi wakiwasindikiza maharusi kutoka nje ya kanisa.

Bwana na bibi wakitoka nje ya ukumbi wa kanisa.

Haya jamani mbona mnapiga picha kabla hatujaweka pozi

haya sasa piga picha yako haraka tusije tukapoteza pozi.

mh! na sisi pia tusikose kumbukumbu hii muhimu sana.

huku Tanga huwa tunaenda kupiga picha baharini, sijui wenzetu msio na bahari mnapiga picha wapi?


Duh! mama Cesi naye hakuwa nyuma alishika nafasi yake sawasawa.

Mmh hili pozi hapa wala sio mahali pake.

Hapo ni sisi hao tulipendeza si kidogo.

Hapo  naona bibi harusi alikuwa keshachoka na hekaheka za harusi. inabidi na mimi niishie hapa kwa kuwatakia maisha mema heri na baraka tele.

Jumanne, 4 Desemba 2012

KUMBUKUMBU MAZISHI YA DR REMMY


ALIYEFARIKI ATOKEA GHAFLA.


Hizi picha haihusiani na tukio linalolipotiwa ila imewekwa hapa kwa sababu ya mahusiano na vitendo vya kishetani


Bado huyu yumo ndani amefungiwa, lakini saa saba za usiku wa kuamkia leo (jana) alitaka kutoka, aling’ang’ana sana ili atoke, akapiga sana mlango...wakamfanya dawa ndipo akajaribu kutulia hadi sasa bado yumo ndani na usiku alipewa chakula akala na asubuhi amepewa uji” alisema mtu wa karibu wa mwanamke huyo.
MAMIA ya wakazi wa Kijiji cha  Lamadi, wilayani Busega mkoani Simiyu, juzi walifurika katika Kitongoji cha Mabulugu kumshuhudia mwanamke Ngulima Kilinga (30), aliyedaiwa kufufuka huku mwili wake ukiwa umehifadhiwa katika hospitali ya Mkula iliyopo mkoani humo.
Inadaiwa kuwa mwanamke huyo aliyefariki dunia tangu juzi, alionekana saa chache baadaye akiwa mzima wa afya na kuingia nyumbani kwake.


Habari zaidi kutoka katika kitongoji hicho zinasema mwanamke huyo bado amefungiwa ndani ya nyumba yake akifanyiwa dawa za kienyeji ili arudie katika hali yake ya kawaida, kwani kwa sasa anaonekana kama zezeta.
“Bado huyu yumo ndani amefungiwa, lakini saa saba za usiku wa kuamkia leo (jana) alitaka kutoka, aling’ang’ana sana ili atoke, akapiga sana mlango...wakamfanya dawa ndipo akajaribu kutulia hadi sasa bado yumo ndani na usiku alipewa chakula akala na asubuhi amepewa uji” alisema mtu wa karibu wa mwanamke huyo.
Pia inadaiwa kuwa tayari mganga wa kienyeji amekwisha kuja kwa ajili ya kutengeneza mwanamke huyo ili aweze kurudia hali yake na kwamba amewashukuru wananzengo hao kwa kuweka maiti kwenye nyumba ya mtuhumiwa huyo, kwamba hiyo ndiyo njia sahihi.
Kamanda wa Polisi mkoani Simiyu, Salum Msangi alithibitisha tukio hilo, lakini akabainisha hayo ni mambo ya imani za kishirikina.
Kamanda Msangi alisema polisi walipelekwa katika eneo la tukio kuhakikisha usalama wa wananchi na hadi saa 9:00 jioni jana, maiti ya mwanamke huyo iliyokuwa hospitali ilikuwa haijazikwa.
Jana umati mkubwa wa watu ulifurika katika Hospitali ya Mkula kulikohifadhiwa mwili wa mwanamke huyo kuushuhudia.
Ndugu wa mwanamke huyo akiwamo mumewe Ngitu Masisanga na mama yake mzazi, Mwashi Myeya walisema Ngulima aliugua ghafla juzi baada ya kukwama na mfupa wa samaki wakati akila chakula nyumbani kwake.
“Baada ya kuugua alipelekwa hospitali ambako alifariki ghafla na kuwekwa kwenye nyumba ya kuhiofadhiwa maiti’’ alisema.
Alisema  cha ajabu ni kwamba wakati wamelala nyumbani kwa marehemu sambamba na waombolezaji wengine, saa 7 usiku marehemu alitokea akiwa uchi.
Walisema marehemu huyo alimwita mtoto wake ampatie nguop na kuchukua albamu ambapo aliangalia picha.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa mbali na kutazama picha hizo na kutaka kupewa nguo zake, pia marehemu huyo alichukua tochi iliyokuwa ikiwaka na kuizima.
Mama mzazi wa marehemu alisema, “Kabla ya kukimbia nje tulimzuia yeye kutoka nje tulimfungia mlango na sisi ndio tukakimbilia nje, licha ya kufunga mlango alikuwa akiupiga kwa nguvu ufunguke ila na yeye aweze kutoka nje, kuna mtu amefanya dawa za kienyeji ndio tunasubiri majibu.”
CHANZO:GAZETI LA MWANANCHI

HALI HALISI YA KANISA LA TANZANIA


Moses Kulola

INGAWA takwimu zilizotokana na Sensa ya taifa zinaonyesha kuwa Ukristo kwa ujumla wake unakua kwa kasi ndogo, ikiwa ni chini ya asilimia 35 ya Watanzania wanaokadiriwa kufikia milioni 40, takwimu hizi haziendani na hali halisi inayoonekana hata kwa macho ya kawaida.

Utafiti wa awali uliofanywa na Tanzania Christian Directory unaonyesha kuwa kasi ya ukuaji wa makanisa ya kiroho, unaoendana na idadi ya kubwa ya watu wanaookoka kila siku inapingana kwa kiasi kikubwa na takwimu za Sensa.
Ingawa takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya Wakristo na wapagani inakaribiana, huku Waislamu wakiwa ni wengi zaidi, vugu vugu la wokovu na ukuaji wa kasi wa makundi ya waumini wa makanisa ya Kiroho vinaashiria kuwa hali si kama inavyodhaniwa.
 Kwa mfano, utafiti kuhusu ukuaji wa makanisa unaonyesha kuwa Huduma ya Kitume na Kinabii ya Efatha imekua kutoka watu 100, miaka kumi iliyopita na sasa ina idadi ya watu 100,000 katika makanisa yake yaliyosambaa nchi nzima.Huu ni mfano wa kanisa moja tu la kiroho, na ikumbukwe kuwa Tanzania ina maelfu ya makanisa yanayokua kwa kasi ya kati. Katika kanisa hilo la Efatha ambalo watafiti walilitumia kama mfano, kwenye mkutano mmoja mwishoni mwa mwaka jana, jumla ya watu 2000, waliokoka baada ya semina ya wiki moja.
Inakadiriwa kuwa waumini 15,000 huhudhuria ibada ya Jumapili katika kusanyiko moja tu na kanisa hilo lina matawi kila kona ya Tanzania. Kulingana na ukweli huu lazima takwimu za Sensa ambayo hufanyika mara moja kila baada ya miaka 5, au 10 haziwezi kutoa hali halisi ya ukuaji wa makanisa. Dar es Salaam, ambayo ni kioo cha ukuaji wa makanisa, ina makanisa mengi yanayokua kiidadi kutokana na:
1.Watu kuyaacha maisha ya dhambi na kuamua kumpokea Bwana Yesu 

2.Kukua kibailojia, kutokana na watu kuzaliwa na kukulia katika imani ya Kikristo
3.Kuhama kutoka dini nyingine kwenda Ukristo wakivutwa na ishara na miujiza ambayo inadhihirika kila kukicha katika makanisa ya Kiroho.
UKUAJI WA UKRISTO NCHINI
Ukiachilia mbali Kanisa la Efatha linaloongozwa na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, ambalo linaaminika kuwa linaongoza kwa kukua kwa kasi na kuenea nchi nzima, likiwa na watumishi wanaosoma katika Chuo cha Huduma hiyo kilichopo Kibaha mkoani Pwani, Kanisa la Ufufuo na uzima, chini ya Askofu Josephat Ngawajima (maarufu kama kanisa la Misukule) nalo limekuwa na idadi kubwa ya watu wanaookoka kanisani hapo kila siku na inakadiriwa kuwa umati wa watu 12, 000 wanakutana pamoja kila Jumapili. Msisitizo wa kanisa hilo ni kuwafufua watu waliochukuliwa au kupotea katika mazingira ya kutatanisha. Mwishoni mwa mwaka jana kiongozi wa kanisa hilo alionyesha hadharani watu 150, ambao wanaaminika kuwa walirejeshwa kutoka mikononi mwa wachawi.

Hata hivyo utafiti unaonyesha kuwa kasi yake ya kujitanua nje ya Dar es Salaam, si kubwa sana na ukilinganisha na Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) linalongozwa na Askofu Zakaria Kakobe, likiaminika kuwa msisitizo wa mahubiri yake ni Utakatifu na kuzingatia maadili.

Pamoja na kuwa na msimamo mkali wa kuzingatia maadili na msimamo wa kuwapiga marufuku wanawake wasiofunika vichwa na waliovaa nywele za bandia kuingia kanisani humo, bado kanisa hilo limebaki kuwa miongoni mwa makanisa ya uamusho na lenye matawi sehemu nyingi za Tanzania.

Ngurumo ya Upako
Huduma hii iko chini ya mwanzilishi wake Mheshimiwa Nabii GeorDavie , na makao makuu yake yako nje kidogo ya jiji la Arusha, katika bara bara ya kuelekea Dodoma. Huduma ya Ngurumo ni miongoni mwa vituo vinavyokusanya idadi kubwa sana ya waumini kwa wakati mmoja.

Inaaminika kuwa zaidi ya watu 12,000 hukusanyika pamoja kumtukuza Mungu kila Jumapili na tayari inapanuka kwa kasi ya kutisha ikiwa na matawi katika mikoa mbali mbali ya Tanzania na nje.

Mafundisho ya Huduma hii yamelenga zaidi kwenye ukombozi na uponyaji. Kuna shuhuda nyingi za watu waliokuwa wamekaribia kufa walipoamini walipona na wako hai wakimtukuza Mungu wa mbinguni.

Pia ni mahali ambapo kuna shuhuda za kurejeshwa kwa watu waliokuwa wamechukuliwa misukule na wale ambao wanateswa na ibilisi.

Makala zake kwenye magazeti na vipindi vya Televisheni vimeelezwa kuwavuta watu wengi katika ufalme wa Mungu.

Living Water Center
Huduma hii kama ilivyo kwa huduma nilizotaja hapo juu, haikuanza siku nyingi sana, lakini pia imekuwa na uamusho mkubwa na tayari ina matawi kadhaa nchini ikiwa ni pamoja na jiji la Arusha na Mwanza.

Mikutano ya hadhara, iliyoongozwa na Kiongozi wake Mtume Onesmo Ndegi, katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza na Arusha, pamoja na uwezo wake mkubwa wa kutumia njia za kisasa za mawasiliano kuhubiri, inaelezwa kuwa kivutio na uamsho mkubwa.

Muundo wa kanisa lake ambalo limejengwa kwa makuti kitaalamu na kuonekana kama kiota cha kitalii ni miongoni mwa mambo ya kipekee katika huduma hii ambayo huvutia watu wengi.

Kanisa hili ni pia linasisitiza mafundisho ya utakatifu, lakini likijikita zaidi kwenye ukombozi na mafanikio ya mwili na roho.

Kiongozi wake ni miongoni mwa wachungaji wa mwanzo kutumia televisheni kupeleka habari njema za injili ulimwenguni kote.

Mikocheni B. Assemblis of God
HILI ni kanisa la kipekee ambalo linaongozwa na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mchungaji Dk. Getrude Rwekatare, ambaye licha ya kuwa Mchungaji mwenye uwezo mkubwa wa kuhubiri, ni mwanamke ambaye mafanikio ya kimwili pia ni mfano wa mahubiri yake.

Pamoja na kuhubiri injili kwa muda mrefu tangu alipokuwa kiongozi wa wanawake kwenye kanisa la Tanzania Assemblies of God, Ilala, jijini Dar es Salaam, ni mwanaharakati wa haki za akina mama na watoto na mfanyabishara anayemiliki mtandao mpana wa shule za St. Mary’s International, Kenton, na kituo maarufu cha Redio kiitwacho Praise Power, ambacho kinatoa nafasi sawa kwa wahubiri wengine kuhubiri Injili kupitia vipindi vyake mbali mbali.

Kanisa lake pamoja na mambo mengine linahubiri Injili yenye msisitizo wa mafanikio. Pia anaendesha vituo kadhaa vya watoto yatima na tayari kanisa lake limefungua matawi katika jiji la Dar es Salaam.

Kanisa hili lilianzia kwenye majengo ya shule ya msingi Mikocheni mika tisa hivi iliyopita, lakini sasa limekua na kuweza kujenga jengo la ibada lenye uwezo wa kukusanya zaidi ya waumini 8,000 kwa ibada moja ya Jumapili.

Shule alipoanzia kanisa mchungaji huyo ameipa zawadi ya kuijengea majengo ya kisasa ya kufundishia na huu umebaki kuwa mfano wa jinsi kanisa linavyojali jamii.


HAKUNA LISILOWEZEKANA
Hii ni huduma ya Kiroho iliyoanzishwa na Askofu Sylvester Gamanywa, mmoja wa maaskofu vijana na shupavu mwenye jicho la kuona mbali na kushiriki katika harakati kadhaa.

Mara nyingi ni mtu wa kuingia katika kila jambo na kutumia mamlaka yake kutafuta ufumbuzi. Katika uchaguzi mkuu uliopita alikuwa miongoni mwa wahubiri wa kwanza kujitoa katika kuendesha kampeni ya kuhimiza amani na kuliombea taifa.

Akitumia kituo chake cha Redio ya Kikristo itwayo Wapo F.M, Askofu Gamanywa, aliongoza pia harakati za kuhimiza watu kubadili tabia ili kujikinga na gonjwa la UKIMWI, hapo serikali ikatambua mchango wake na akateuliwa kuwa mmoja wa Makamishina wa Tume ya kupambana na ugonjwa huo Tanzania.

Ingawa alikuwa mhubiri kwa muda mrefu, akimiliki pia Gazeti la Kikristo la Msema Kweli, Askofu Gamanywa alipata mafanikio makubwa katika miaka sita tu iliyopita ambapo uamsho mkubwa umedhihirika katika huduma yake.

Baada ya huduma yake kupanuka alifungua kituo cha miujiza na uponyaji huko Mbezi Beach, jijini kiitwacho BCIC, ambacho mbali ya kuwa ni kituo cha maombi na uponyaji kwa damu ya Yesu, ni mahali ambapo semina na masomo maalumu yanayolenga kuibadili tabia ya Watanzania hufanyika kwa mafanikio makubwa.

Kwa wakati huu Askofu Gamanywa, anaendesha kampeni iliyolenga kuokoa kizazi kijacho kwa kupambana na uharibifu wa maadili kwa vijana.

Calvary Assemblies of God (CAG)
Huduma hii ni moja kati ya huduma za kiroho hapa nchini, Ilianza miaka 15 iliyopita na imekuwa ikikua kwa kasi na kupata mafanikio makubwa sana ya kiroho. Mbeba maono wa huduma hii ni Mtume Dustun Maboya, ambaye yeye ndiye kiongozi mkuu wa huduma.

Hudumu hii chini ya Mtume Dustun Maboya, ilianzia mjini Morogoro mwaka 1994 huku ikiwa na waumini 200 tu, katika ibada moja na hadi kufikia sasa inakadiriwa kufikia zaidi ya waumini 5000 kwa ibada.

Msimamo na mkazo wa mafundisho ya huduma hii ni kuhubiri mafundisho ya wokovu na mafanikio ya kiroho na kimwili pia.

Mtume Dustan Maboya aliokoka mwaka 1977 na mwaka 1978 mara baada ya kupata wito wa kumtumikia Mungu alijiunga na chuo cha biblia cha mkoani Arusha na kuhitimu mwaka 1981. Baada ya hapo aliacha kazi na kuamua kumtumikia Mungu kwa kuanzisha huduma hii.

Kwa sasa Calvary Assemblies of God, chini ya Mtume Dunstun Maboya, imeenea nchi nzima na kufikisha idadi ya makanisa 460 kwa nchi nzima mjini na vijijini.

Silioam Ministry International
Huduma hii, ikiwa chini ya mbeba maono Mtume N.Z.Munuo, ilianza miaka mitano iliyopita na kuwa na makao yake makuu jijini Dar es salaam.

Huduma hii ambayo inaonyesha kukua kwa kasi sana, ilianza ikiwa na washirika watatu tu waliokuwa wakifanya ibada nyumbani kwa Mtume Munuo. 

Kwa sasa huduma hii imetanuka nchi nzima na kuwa na matawi kila Wilaya na inakadiriwa ibada moja inakusanya waumini zaidi ya 3000 kwa jumapili.

Msimamo na mkazo wa mafundisho ya huduma hii ni kuvunja misingi mibovu ya shetani ndani ya watu na kisha kuwajenga watu hao katika nguzo nne, NENO,IMANI, UTAKATIFU na UTII.

Mtume Munuo, alipata wito wa kumtumikia Mungu na kumjengea nyumba ya ibada ambayo watu watamwabudu katika roho na kweli akiwa mwajiriwa wa Shirika la Umeme nchini na baadaye aliamua kuacha kazi na kwenda kumtumikia Mungu. Hiyo ilikuwa mwaka 2003.

Kwa sasa huduma hii tayari imekwishaanzisha chuo cha Biblia kinachoitwa Siloam Bible College, ambacho kimetumika kuwaandaa watumishi mbalimbali wa Mungu kutoka katika makanisa na huduma mbalimbali hapa nchini. Kwa sasa hudumu hii ya Siloam hapa nchini, chini ya mtume N.Munuo, ina jumla ya makanisa yapatayo 70 nchini.

Alhamisi, 29 Novemba 2012

BOB MARLEY MHUBIRI WA AMANI NA UPENDO BILA YESU




Mcheza mpira wa miguu, Mhubiri wa amani na upendo, Mwanamapinduzi, Mwanaharakati, Mpiganaji, Mwanasiasa, Mwanamuziki wa Reggae na Nyota ya kwanza katika ulimwengu wa tatu Bob Marley.


Alizaliwa akiitwa Robert Nesta Marley na mama wa Kijamaica mwenye asili ya Afrika, bi Cedella Booker na baba mwanajeshi Mwingereza aliyefariki kijana Robert akiwa bado mdogo sana akiwaacha katika umasikini mkubwa.



Bob Marley alizaliwa panapo usiku wa kuamkia Februari 6, 1945, St Anns Parish kijiji cha Nine Miles (maili tisa) huko Jamaica.

Kumbukumbu zake za utotoni na ujanani zimejaa harakati za maisha na muziki. Harakati zilizomkutanisha na kijana machachari Peter Tosh na pia Bunny Livingstone (Wailer) na hatimaye vijana wengine kama Junior Braithwaite na Beverly Kelso. Panapo mwaka 1963, Bob akiwa na wenzake waliojiita Wailing Wailers waliweza kusaini mkataba na prodyuza maarufu wakati huo Coxsone Dodd na kutoa vibao kadhaa kikiwemo 'Simmer Down' kilichowatambulisha vema katika ulimwengu wa muziki wa Jamaica.



Bob na Rita Anderson walioana mwaka 1966 baada ya Bob kurejea Jamaica akitokea Marekani ambako alikacha kwenda vitani Vietnam. Aliporudi Jamaica, Bob alikuta imani ya Kirastafari ikiwa imepamba moto kufuatia ziara ya Mfalme wa Ethiopia Haile Sellassie (Ras Tafarr Makonen) hapo mwaka 1965. Hotuba ya Sellassie ndicho kibao cha Bob kiitwacho 'War'

Kundi la Wailing Wailers halikudumu sana. Lilivunjika mwaka 1974 na Bob kuunda kundi lake maarufu zaidi katika historia ya muziki wa reggae la 'Bob Marley and the Wailers' wakafanikiwa kutoa albamu ya 'Catch A Fire' panapo mwaka 1975 ikiwa na kibao maarufu kilichopatwa kuimbwa tena na wanamuziki wengi sana cha 'No Woman No Cry'



Mwaka 1976, Bob Marley alifanikiwa kuwapatanisha mahasimu wakubwa wa kisiasa nchini Jamaica, waziri mkuu na kiongozi mkuu wa upinzani, Michael Manley na Edward Seaga. Wajamaica walimwona Bob Marley kama shujaa halisi wa taifa lao. Bob na kundi lake walishambuliwa na risasi siku tatu kabla ya tukio hilo, lakini walipona.

Mwaka huohuo wa 1976, Bob Marley na kundi lake walitoa albamu ya 'Exodus' iliyovunja rekond ya mauzo na kukaa kwenye chati ya Billboard kwa majuma 52 ikikamata namba moja.



Bob Marley alizunguka mabara yote ya ulimwengu kupiga muziki wake uliokubalika sana. Maonesho makubwa zaidi aliyafanya Uingereza, Ujerumani, New Zealand, St. Barbara, California huku pia akishiriki kama mgeni mwalikwa muhimu katika sherehe ya uhuru wa Zimbabwe mwaka 1980.

Maradhi ya kansa iliyoanzia kidoleni mguuni kwake, yaliukatisha uhai wake panapo Mei 11, 1981 huko Miami Marekani akiwa angali kijana wa umri wa miaka 36. Katika kibao chake cha 'Rastaman Chant' alipata kusema, "One bright morning when my work is over, I'll fly away to Zion"
Hata hivyo aliiacha kazi yake kama mhubiri wa amani na upendo.

Serikali ya Jamaica, kwa kuutambua mchango wake, ilimtunukia nishani ya juu zaidi 'Order of Merit.'

Bob Marley aliacha watoto 12, wengi wao wanajihusisha na muziki wa reggae na hip hop.

Bob Marley atakumbukwa zaidi duniani kama balozi na shujaa halisi wa muziki wa reggae. Atakumbukwa kwa kuuweka muziki huu wenye nguvu katika ramani ya ulimwengu.



Muziki wake utaendelea kuishi vizazi na vizazi. Ni urithi muhimu sana kwa wanaoupenda muziki wake. Ama kwa hakika wanajivunia sana miaka 36 ya uhai wake.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi daima. Amina.

MKASA WA MELI YA TITANIC

Pichani, meli ya RMS Titanic ikiondoka Southampton Uingereza hapo Aprili 10, 1912


kwa meli ya Titanic kulitokana na tatizo la usukani


LONDON – Meli ya Titanic iligonga siwa barafu (iceberg) tarehe 14 Aprili 1912 mnamo saa 5.40 usiku kutokana na hitilafu ya usukani.  Lakini ikazama kwa kasi zaidi kutokana na Afisa mwandamizi wa meli hiyo kumwamuru nahodha aendelee na safari.  Hayo yameelezwa jana Jumatano na mwandishi wa Kiingereza alipohojiwa na shirika la habari la Reuters.


Louise Patten, mwandishi na mjukuu wa Afisa mwandamizi wa meli hiyo Charles Lightoller, ameamua kusema ukweli juu ya kile kilichotokea karibia miaka 100 iliyopita.  Ukweli huo ulikuwa umefichwa kwa makusudi kwa kiasi cha miaka 100 ili kulinda heshima ya babu yake aliyekuja kuwa shujaa wa vita kuu ya dunia.

Lightoller, afisa mkuu aliyesalimika katika ajali ile ya kihistoria aliuficha ukweli huo alipohojiwa mara mbili.  Alihofu kuwa ukweli huo ungeifilisi kampuni iliyoitengeneza meli hiyo na pia kuwapotezesha ajira wenzake walioajiriwa katika kampuni hiyo.


"Wangeweza kuikwepa barafu ile kama isingekuwa kasoro kwenye usukani," Patten ameiambia Daily Telegraph.


Mabaki ya meli ya Titanic kama yanvyoonekana katika picha hii iliyopigwa hivi karibuni.

"Badala ya kuuelekeza usukani wa Titanic kwa usalama kuelekea kushoto kwa siwa barafu lile, iligundulika kuwa usukani haufanyi kazi upande huo.  Aliyeushika usukani, nahodha  Robert Hitchins, alichanganyikiwa na kuuelekeza upande usio sahihi."


Patten, ameyafunua hayo ili kwenda sambamba na utowaji wa riwaya yake mpya "Good as Gold" ambayo ameitumia kuelezea mazungumzo ya manahodha hao.  Kwa mujibu wa mazungumzo hayo, kulikuwa na mifumo miwili tofauti ya usukani.

Jambo lililokuwa la muhimu sana, mfumo mmoja  ulikusudiwa kuuzungusha usukani kuelekea upande mmoja, na mfumo mwingine, kinyume chake.

Kosa hilo la usukani lilipofanyika,  Patten akaongeza, "walikuwa na dakika 4 tu za kuubadili mfumo huo.  Wakati afisa mkuu William Murdoch alipoligundua kosa la Hitchin na kujaribu kulirekebisha, alikuwa amechelewa."

Babu yake Patten hakuwa akiangalia wakati meli ikigonga siwa barafu, lakini alikuwepo wakati wa kikao cha mwisho cha maafisa wa meli ya Titanic kabla ya meli hiyo kuzama kabisa.


Babu yake Patten si tu alisikia juu ya makosa hayo, bali pia amri kutoka kwa J. Bruce Ismay, mwenyekiti wa White Star Line, kampuni iliyoitengeneza meli hiyo akimwamuru nahodha wa meli kuendelea na safari.  Tendo la kuendelea na safari lilisababisha meli kuzama kwa kasi kubwa sana.  Masaa saba tu hadi kufikia saa 2.20 asubuhi, meli ilikuwa imezama yote.

"Kama Titanic ingesimamishwa pale pale, isingezama kamwe kwani ingeweza kumudu kusubiri meli za uokoaji na pasingekuwepo vifo vile.," alisema Patten.

Meli ya RMS Titanic ilikuwa ndiyo meli kubwa zaidi duniani wakati ikiondoka Southampton, Uingereza, kuelekea New York katika safari yake ya kifahari zaidi melini panapo Aprili 10, 1912. Siku nne baadaye ikiwa safarini iligonga siwa barafu na kuzama.  Ajali hiyo kubwa zaidi ya meli katika historia, iligharimu maisha ya watu 1517 kati ya watu 2227 waliokuwa ndani ya meli hiyo ikijumlisha abiria na wafanyakazi.


Nimeiandika habari hii baada ya kuisoma kwenye mtandao wa Reuters kwa sababu moja.  Nimetaka tuone tofauti ya wenzetu wa Ulaya.  Miaka 100 sasa, wao bado wanajali juu ya chanzo cha ajali.  Sisi meli ya Mv Bukoba iliyozama miaka 14 tu nyuma, nani anajali tena kujua chanzo kilikuwa nini?  Wenzetu na rekodi nzuri ya watu waliokuwemo.  Sisi wala hatujawahi kuwa na idadi kamili ya wahanga

Hebu litazame hili jedwali juu ya rekodi za abiria wa Titanic.  Sisi hadi leo hatuna idadi kamili ya wahanga wa majanga makubwa.  

category
waliokuwa melini
waliopona
asilimia waliopona
waliokufa
asilimia waliokufa
1st class
329
199
60.5 % 
130
39.5 % 
2nd class
285
119
41.8 % 
166
58.2 %
3rd class
710
174
24.5 % 
536
75.5 %
crew
899
214
23.8 % 
685
76.2 %
Jumla
2,223 
706 
31.8 %
1,517
68.2 %

Chanzo jedwali:  wikipedia



 FA