Ijumaa, 21 Septemba 2012

KUCHEKA HUONGEZA MAISHA




Habari za leo mpenzi msomaji wangu. Leo nimekuja na somo zuri ambalo nalitoa kama zawadi kwako. Kama wengi wetu tujuavyo, kiwango cha miaka ya kuishi hasa katika nchi za ulimwengu wa tatu kimepungua sana nyakati hizi, hivyo kila tunaposherekea mwaka mpya tunasherekea pia uzee na utimilifu wa miaka yetu ya kufa, lakini hilo lisitupe hofu kwani wataalam wamegundua maajabu yapatikanayo kwa mtu kucheka.

Kwa kutambua umuhimu wa maajabu hayo nimeona ni vema nikaelezea faida za mtu kucheka. Ifahamike kuwa watafiti mbalimbali duniani wamebaini kuwa mtu anaweza kujikinga, kujiponya na magonjwa hatari ya kansa, moyo na kisukari kwa kucheka na isitoshe achekaye anatajwa kuufanya mwili wake usionekane umezeeka hata kama atakuwa na umri mkubwa.

Kwa mujibu wa watafiti wa masuala ya kijamii, ugumu wa maisha unaoleta msongo wa mawazo ndiyo unaotajwa kuchangia vifo vya wanadamu wengi sambamba na kufupisha umri wa kuishi. Wanasema mtu mwenye kutingwa na sononi kila mara huchoma seli nyingi muhimu katika mwili wake, hivyo kumfanya awe katika hatari ya kushambuliwa na magonjwa niliyoyataja hapo juu.
Katika tafiti za hivi karibuni ukiwemo ule uliyoendeshwa na wasomi wa Chuo Kikuu cha Amerika Cardiology, imebainika kuwa uhaba wa furaha hasa fursa ya watu kupata muda wa kucheka kwa siku ni moja kati ya sababu kubwa zinazochangia magonjwa hatari miongoni mwa watu wengi. Wanasema watu wengi wamechipusha vimelea vya magonjwa si kutokana na bakteria halisi bali mfadhaiko wa mioyo yao.
 
Kwa maana hiyo wataalam hao wameibuka na ushauri kuwa ni bora watu wakajibidisha kutafuta furaha katika maisha yao kuliko kudumu katika uhangaikia tiba ghali za dawa zinazotolewa na vituo vya afya na hospitali, ilhali mzizi wa magonjwa yao unatokana na wao wenyewe kuishi bila kicheko ambacho kinatafsiri furaha aliyonayo mtu husika (kumbuka sizungumzii kicheko cha kebehi).
 
Kwa mujibu wa wasomi hao imegundulika kuwa kicheko ni tiba na kinga bora ya magonjwa yanayomkabili mwanadamu yakiwemo magonjwa ya moyo ambayo ni hatari sana kwa uhai. Mtu ambaye anaweza kutumia dakika 20 kwa siku kwa kucheka, anaweza kutibu maradhi yake hata bila kumeza vidonge. Inatajwa kuwa kicheko huweza kukuza mara dufu uzalishaji wa 'Immuni' ambazo ndizo zenye kazi ya kuukinga mwili usishambuliwe na bakteria.
 
Kwa maana hiyo, mwili wa mtu ambaye anaishi kwa kucheka kwa kiwango hicho nilichokitaja unaelezwa na wataalam hao kuwa, utakuwa na uwezo wa ajabu wa kuua na kusisafisha kemikali za hatari zinazozalishwa mwilini. Kama hilo halitoshi, upo pia uwezo wa kuzalisha kiwango sahihi cha sukari kwa mwili wa mtu mwenye furaha inayoambatana na kucheka mara kwa mara.
 
Uzoefu uliopatikana kutoka katika Hospitali ya watoto ya Manchester nchini Marekani ambayo hutumia katuni na filamu za kuchekesha kwa wagonjwa wanaolazwa hapo, umebaini kuwa kuna kiwango kikubwa cha nafuu wanachopata wagojwa hata kabla ya kuanza kwa tiba za magonjwa yanayowakabili.
 
Kutokana na faida zinazopatikana kutokana na kucheka ikiwemo hiyo tiba ya ajabu ya magonjwa, Dr Madan Kataria wa India mwaka 1998 aliitangaza Mei 6 ya kila mwaka iwe ni siku ya kicheko duniani, ambapo zaidi ya nchi 50 zilikubali kuiadhimisha, ikiwa kama ishara ya kumuunga mkono Dr Madan katika hamasa yake ya kujenga familia, urafiki na ujamaa wenye furaha.
 
Kwa mantiki hiyo ni jambo la busara kwa kila mtu ndani ya familia na sehemu za kazi kutafuta uhusiano wenye furaha, ili uweze kuchochea kicheko ambacho ni muhimu sana katika maisha ya mwandamu. Lakini kinachoshangaza na ambacho kimetajwa pia na wataalam hao ni kuwa watu wengi siku hizi wanaishi maisha yaliyo mbali na furaha jambo ambalo ni hatari kwa afya.
 
Inasikitisha kuona kwamba kadili miaka inavyosonga mbele familia nyingi zimekuwa na maisha ya yaliyojaa kununiana na kutofurahishana. Si ajabu mtu akawa ni mwenye kukunja uso tangu asubuhi mpaka jioni kiasi cha kutoona maana ya kukaa na kufurahi na wenzake ndani ya nyumba. Ifahamike kuwa mtu wa tabia hiyo anakuwa katika mazingira ya hatari ya kufariki mapema (utafiti sio hali halisi) au kuonekana mzee ilhali umri wake ni mdogo.
 
Kwa kuzingatia hayo mimi pia natoa ushauri wangu kuwa kila mmoja wetu ajitahidi kubadili mfumo wa maisha yake kwa mwaka huu kutoka katika mifarakano inayoondoa furaha katika jamii na kutafuta kuishi kwa furaha inayotajwa kuwa na faida katika afya zetu. Mbali na hilo tunaweza kujikuta tunatafuta pesa na hatimaye kushindwa kuzitumia kwa raha kutokana na kuandamwa na magonjwa ambayo tunaweza kuyaepuka kwa kujifurahisha wenyewe.
Hatuna budi pia kwa mwaka huu kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa anakuwa na jukumu la kumsaidia jirani au rafiki yake ili awe mbali na msongo wa mawazo. Hata pale inapopatikana fursa ya kwenda kuwaona wagonjwa tunatakiwa kuwatazama huku tukionesha tabasamu na kuwatia moyo. Kinyume

CHANZO CHA MAISHA YA WASIWASI UNAYOISHI UNAKIJUA?


Unafahamu chanzo cha maisha ya wasiwasi unayoishi?

·          
UKICHUNGUZA kwa makini utabaini kuwa watu wanaoishi katika hali ya umaskini ndiyo wanaoongoza katika maisha ya wasiwasi, tofauti na wale waliofanikiwa kimaisha.Kwa maskini fikra za kuuguza ni nzito maradufu kwa sababu huambatana na maswali: “Nitafanyaje mwanangu akiugua na mimi sina fedha za matibabu?”
Kwa msingi huo, maisha ya wasiwasi ni kipimo kikuu cha udhaifu wa mtu katika kushughulikia changamoto zinazomkabili kwenye maisha yake ya kila siku.
Ni rahisi mtu kujua anawajibika kwa kiwango gani katika kukabiliana na matatizo kwenye maisha yake kwa kujitathmini ni mwoga wa maisha kwa asilimia ngapi!
Ukimsikia mtu anasema naogopa hili na lile likinikuta ujue amekosa au hajajenga nyenzo za kulivuka tatizo husika. Kisaikolojia si rahisi mwanadamu kuhofu kitu ambacho anaweza kukabiliana nacho na kukishinda.
Wamasai hawamuogopi mnyama simba si kwa sababu ni mpole bali pamoja na ukali wake wanajiamini katika kumkabili na kumshinda, hivyo ndivyo ilivyo katika matatizo yanayotukuta kila siku kwenye maisha yetu.
Katika hali ya kawaida hakuna wasiwasi unaoshinda ujumla wa wanadamu wote isipokuwa kifo. Nacho ni kwa sababu moja tu kwamba hajatokea mwenye kukabiliana nacho na kukishinda, lakini mambo mengine yanatofautiana kati ya mtu na mtu.
Wapo wanaoogopa kufungwa jela lakini kuna wengine wanatamani waishi huko milele na milele. Kama hilo ni nusu fikra, yapo mengi ya kujilinganisha, kwa mfano, wasiwasi wa kuugua hauwatishi watu wote kwa sababu kuna wanaojiamini kuwa wana uwezo wa kwenda nchi mbalimbali za Ulaya na kujitibu kwa gharama yoyote wakapona.
Miaka michache iliyopita nilikuwa na wasiwasi wa kuishi maisha ya peke yangu. Nilijiuliza nitakula nini? Nitapata wapi fedha za kulipa kodi ya chumba? Nitawezaje kufanya hili na lile kwenye maisha yangu binafsi? 
Bila shaka mawazo hayo yalitokana na uwajibikaji wangu mdogo katika kupata majibu niliyokuwa najiuliza.
Baada ya kujituma katika kutafuta majibu ya changamoto zilizokuwa zinanikabili, hofu ya maisha ya kupanga haipo tena, najiona niko salama hata kama nikimkuta mwenye nyumba amenuna naamini nitaweza kutafuta mahali nikaishi na familia yangu.
Karne hii ni ya kila mtu kuachana na maisha ya wasiwasi ambayo ni hatari sana katika afya zetu. Mwanzo wa kuishinda hofu ni kupambana na kile tusichokuwa nacho ambacho kwa namna moja ama nyingine ndicho kinachotutia hofu.
Msomaji wangu, chukua muda ujiulize una wasiwasi juu ya nini kwenye maisha yako? Kile unachokiogopa tambua kuwa hujakitafutia nguvu ya kukishinda. Njia pekee ya kuondoa hofu ni kutafuta kinga thabiti itakayokufanya ujiamini kuwa tayari kwa mapambano.
Yawezekana unaogopa uchawi; lakini njia za kuushinda uchawi si zipo? Kwa nini usizifuate? Jenga imani yako kwa kufuata misingi ya dini au jiamini mwenyewe kuwa huwezi kudhurika kwa uchawi. Ukifanya hivyo kikwazo cha wasiwasi huo utakivuka na utaishi kwa amani.
Ninapofundisha somo hili kuna baadhi wanaweza kujiuliza kwamba mtu maskini anawezaje kuishi mbali na wasiwasi ilhali hana kitu? Ukosefu wa kitu ndiyo chanzo cha tatizo, tafuta njia ya kufanya ili upate mafanikio yatakayokukinga na wasiwasi usiokuwa na sababu.
Akiba ya 100,000 ni kubwa kwa mtu ambaye maisha yake ni ya kawaida kwa sababu atakuwa ameweka wazi jibu la nitafanyaje mtoto akiugua usiku? Kwake yeye jibu litakuwa nitakwenda benki na kuchukua 50,000 kisha nitampeleka mwanangu zahanati. 
Bila shaka jibu hili ni la matumaini, tofauti na mtu ambaye hana kitu kabisa.
Nimefundisha kwenye semina na kwenye vitabu vyangu kuwa maisha ya kutafuta, kuweka akiba ni muhimu sana. Naomba msomaji wangu utafute vitabu vyangu uendelee kujifunza masomo haya ambayo naamini yatakuweka mbali na maisha ya huzuni unayoishi sasa. 


MBINU ZA KUFANIKIWA KIMAISHA.




Watu wasioweza kufanikiwa hujaa fikra za kutofanikiwa na mara nyingi hulalamikia sana matatizo yao. Wakati mwingine wasioweza kufanikiwa hugeuza mambo mema na kuyafanya yaonekane mabaya, jua likiwaka watalalamika joto, likipoa watalaumu baridi, watalaumu foleni za barabarani, yaani kwao kila jambo wataligeuza na kulipa sababu mbaya. Hata wanaposhindwa kutekeleza jambo hutoa sababu, yote ni kuzilinda fikara zao za kutofanikiwa.
Tabia hii hukua mpaka kufikia hatua wanapowatazama wenzao hudhani kuwa wanawasengenya, kuwafanyia mambo mabaya, kuwasaliti, ilimradi tu ni kuwa kinyume na mambo mema. Watu wa namna hii hata kama watasaidiwa namna gani hugeuza misaada hiyo kuwa ya kujipendekeza na mara nyingi hupuuza wema haraka na kueneza mabaya ya mtu. Lakini pamoja na yote kutokana na fikra zao kuwa za kushindwa watu wa tabia hii hukata tamaa mapema, pale wanapofanya jambo na kuonekana lina ugumu kidogo.
Hutenda kabla ya kufikiri
Tabia ya pili ya watu wasioweza kufanikiwa kimaisha ni hii ya kutenda jambo kabla ya kufikiria. Watu wa aina hii, kuwa wepesi sana kununua vitu barabarani mara tu wanaposhawashiwa na macho au wauzaji. Utakuta mtu bila hata kujiuliza faida za kitu hicho anaamua haraka kukipata. Ataamua kwa haraka kuoa, kuolewa, kukubali kujiingiza katika mapenzi na hata kufanya jambo lo lote bila kujiuliza atanufaika vipi?
 
Hupenda kuzungumza zaidi ya kusikiliza

Watu ambao wako katika hatari ya kutofanikiwa ni wale ambao daima ni wazuri katika kuzungumza kuliko kusikiliza. Wao huwa ni wajuajia wa kila kitu, hawako tayari kupokea ushauri. Siku zote wanapokuwa kwenye makundi ya watu pengine wajuzi zaidi yao wao huwa hodari kujenga hoja kutetea mambo yao hata kama hayafai. Unaweza kumkuta mtu ni kiongozi wa ngazi za juu, amefanya kosa na watu wote wameona kuwa kakosea lakini mhusika hujiona si mikosaji.
Mtu anapokuwa muongeaji sana huwa mgumu kupokea ushauri wa ye yote, anachoamua yeye hukifanya kwa imani kuwa kinafaa. Ukiwa mtu mwenya tabia ya aina hii huwezi kufanikiwa kabisa katika maisha yako. Watafiti wa masuala ya biashara ulimwengini waliwahi kushauri kuwa mipango mizuri ya kibiashara hutoka kwa watu masikini, ambao walisema hufikiri zaidi namna ya kujikomboa kuliko matajiri wanavyofikiri katika kujiendeleza, hivyo wakasema kama mtu anataka kufanikiwa kibiashara lazima asikilize mawazo ya masikini si kuwapuuza kwa kujiona ni bora zaidi yao.
Hukata tamaa mapema
Watu wanaotaka kufanikiwa huchukulia ushindwa kama hatua ya kuelekea kwenye mafanikio, lakini watu wasioweza kufanikiwa wanapojaribu mara moja au mbili kuvuka kikwazo fulani cha kimaisha na kushindwa hukata tamaa na kutotaka kujaribu tena kusonga mbele. Wanye tabia ya kushindwa kimaisha hawako tayari kudumu na jambo moja linaloonekana kushindikana kwao kwa muda mrefu. Akiona mwanamke ambaye ni mkorofi kidogo, haraka hukimbilia kumwacha na kutafuta mwingine, mara nyingi si watu wavumilivu.
Akijaribu biashara ya vitumbua kwa wiki moja na akaona havinunuliwi, anaaza kupika maadazi, wiki moja baadaye yuko kwenye mihogo, basi ilimradi ni kuhangaika kusikokuwa na tija katika maisha. Ukitaka kuwa mmoja kati ya watu wasiweza kufanikiwa kimaisha, basi jaribu kuishi maisha ya kukata tamaa mapema unapofanya mambo.
Hujaribu kuwarudisha nyuma wengine
Wasioweza kufanikiwa katika maisha huwa na tabia moja ya ajabu ambayo ilianzishwa na Hawa mwanamke anayetajwa katika Kitabu cha Biblia kuwa ni mtu wa kwanza kufanya dhambi. Mwanamke huyu alipodanganywa na nyoka na kuchuma tunda hakutosheka na dhambi zake, bali alimpelekea na mumewe Adamu naye akala. Mara nyingi watu walioshindwa kimaisha kuwa na tabia za kuwashawishi watu wengine wawe kama wao katika mawazo na matendo.
Tabia za watu wa aina hii huwa si za kimaendelezo kwa vile wao hudhani kuwa njia zao ni sahihi na hivyo hujaribu kwa nguvu zao kuwarudisha wengine nyuma ili wawe kama wao. Ni watu wenye wivu wa ‘kijinga’ wakiona mwingine anaendelea katika hiki na kile humpiga vita ili afilisike. Ni wingi wa fitina, uchonganishi. Wenye tabia za kutofanikiwa hudhani kuwa kukwama kwao hutokana na vikwazo vinavyoletwa na wengine. “Kwa sababu jamaa kanikwamisha hiki na kile, nimkwama kwa sababu ya kaka yangu”
Hupoteza muda mwingi
Watu ambao hawawezi kufanikiwa ni wale ambao hupoteza muda mwingi kufanya mambo yasiyokuwa na tija, kwa kuangalia Tv, kusengenya watu, kunywa pombe, kufanya starehe na kutumia muda hovyo kwenye kazi ambazo hazina msaada kwao. Wapo watu mahodari kutembelea kwenye nyumba za wengine na kuongea huko kutwa nzima bila kujali kama muda waliopoteza wangeweza kufanya kazi na kujipatia kipato.
Huchagua mambo rahisi
Wakati mwingine mafanikio huhitaji kufanya kazi ngumu zenye kuchosha, lakini watu wasiokuwa na uwezo wa kufanikiwa wanapoletewa mambo mawilii huwa wepesi zaidi kuchagua jepesi kulifanya. Kama ni kazi, basi zisiwe ngumu sana ziwe nyepesi nyepesi ambazo watazifanya bila jasho. Watu wasiokuwa kwenye njia ya mafanikio hawapendi kujituma, wepesi kuchoka na mara nyingi hupenda sana kufanya kazi kidogo na kulala sana.
Tabia za watu wasioweza kufanikiwa huwa ni za kukwepa kuwajibika. Hata kama kuna mtu anataka kumpatia kitu na akamwambia awahi kesho yake asubuhi, huchelewa kwa vile hawezi kujihimu asubuhi na kuacha raha ya usingizi, wakati mwingine hata akiambiwa asubiri mpaka muda fulani huwa hayuko tayari kusubiri.
 
Leo naomba niishie hapa, tukutane tena wiki ijayo kwa mada nyingine nzuri zaidi.
Labels: SAIKOLOJIA
Chanzo: Sasali blog

WANAWAKE HUISHI UMRI MREFUZAIDI YA WANAUME


POSTED BY MANYOTABLOGSPOT.COMON FRIDAY, MAY 21, 20100 COMMENTS


Inaweza ikawa ni mada ngumu kuikubali kutokana na sababu kadha wa kadha, lakini ukweli unabaki kuwa wanawake wamebainika kuwa na uwezo wa kuishi miaka mingi zaidi ya wanaume, hii ni kwa mujibu wa tafiti nyingi zilizofanywa hivi karibuni ulimwengu, ukiwemo ule ulioendeshwa na wanasayansi wa Chuo cha Liverpool John Moores (LJMU) nchini Uingereza.

Profesa David Goldspink wa LJMU anayejihusisha zaidi na seli za binadamu alieleza matokeo ya utafiti wa jopo lake kuwa “tumebaini kwamba nguvu za moyo wa mwanaume hupungua kwa asilimia 20 – 25 kutoka miaka 18 hadi 70, lakini nguvu ya mioyo ya wanawake wenye umri wa miaka 70 haitofautiani na ya vijana wenye umri wa miaka 20.”


Kwa maana hiyo mwanaume kadili anavyozidi kupata umri mkubwa, nguvu za moyo wake hushuka na hivyo kupunguza kiwango cha msukumo wa damu mwilini na kusababisha madhara ya kiafya na hatimaye kifo. Lakini kwa mujibu wa utafiti huo huo ambao ulihusisha zaidi ya wanawake na wanaume wenye afya 250, ulibaini kuwa mioyo ya wazee wa kike huwa haipunguwi nguvu kutokana na umri wao.


Ifahamike kuwa ukimchukua mwanamke mwenye umri wa miaka 20 ukampima msukumo wa moyo wake ukalinganisha na mzee wa miaka 80 utapata nguvu sawa. Kibaiolojia ni kwamba wanawake wameumbwa tofauti na wanaume, ndiyo maana wanatajwa kuishi miaka 5-13 zaidi ya wanaume na kwamba kiwango hiki kimekuwa kikiongezaeka kutoka karne moja hadi nyingine.



Mazingira ambayo yanashibisha hoja hii ni pamoja na mfumo mzima wa masuala ya kujamiina ambayo huwahusisha watu wa jinsia mbili tofauti. Hata ukiangalia utofauti ulioanishwa mara nyingi na watafiti umewashirikisha zaidi wanawake wenye umri kati ya miaka 18 na kuendeleza, umri ambao kwa kawaida wasichana wengi huwa tayari wamevunja ungo na wengine kuanza kushiriki tendo la ndoa.


Randolph Nesse, mwanasaikolojia wa Marekani aliwahi kueleza faida anazopata mwanamke wakati wa tendo la ndoa na kipindi cha siku zake ambazo zinatajwa pia kumsaidia katika kusafisha kemikali za mwili wake na kwamba upo ushihidi kuwa mwanamke asipoingia kwenye siku zake afya yake huyumba.
 

Maelezo haya na mengine yahusuyo mwanamume kutoa mbegu wakati wa tendo la ndoa yanaweza kuwa sababu ya kuweza kutofautisha umri wa kuishi kati ya mwanaume na mwanamke na kuzidi kuweka hatari kubwa ya umri wa wanaume kuendelea kupungua kama elimu ya kujihami na tatizo hili haitatolewa kwa wahusika.

Kumekuwa na hoja nyingi kuhusu tatizo la wanaume kupungukiwa na umri wa kuishi, wapo wanaosema kuwa wingi wa majukumu ya kifamilia huwapunguzia umri wanaume, hata hivyo njia pekee zinazotajwa kuwasidia mwanaume kuweza kuimarisha mapigo ya moyo wake ni hizi zifuatazo:

KWANZA- Ili mwanaume aweze kuusaidia moyo wake kuwa na nguvu katika kipindi chake cha maisha ni lazima afanye mazoezi ya mwili. Wanaume wengi wamekuwa wakipuuza ufanyaji wa mazoezi, jambo ambalo ni hatari kwa afya zao. Ufanyaji wa mazoezi unaweza kuusadia mwili wa mwanaume kuongeza msukumo wa damu na kumuwezesha kutoa kemikali hatari mwilini kwa njia ya jasho ambalo haliwezi kutoka kama mtu atakuwa amekaa na kuendekeza starehe.

PILI- Mwanaume anashauri kupunguza kiwango cha kufanyaji mapenzi. Upunguzaji huu utasaidia kuufanya mwili wake uwe na seli za kutosha kulingana na lishe anayopata, hata hivyo kama mwanaume anataka kufanya mapenzi kwa kiwango cha mara tatu au nne kwa siku lazima azingatie mlo wenye nguvu. Lakini kwa wanaume ambao ni dhaifu, wakiwemo wenye virusi vya UKIMWI hawashauriwi kufanya ngono mara kwa mara.

TATU- Kucha kutunza hasira kifuani. Wanawake wengi hufanikiwa kupumzisha miili yao kwa sababu ni wepesi wa kukasika na kumaliza mambo tofauti na wanaume ambao hutajwa kutumia muda mwingi kufuga chuki moyoni. Inashauriwa kuwa kama kuna jambo ambalo limetokea ni vema kulimaliza na kuachana nalo, ili kuufanya mwili uwe huru. Kitendo cha kuweka hasira mwilini huchangia moyo kupungukiwa na nguvu za kufanya kazi sawa sawa.

NNE – Kuzingatia lishe bora, kupata muda wa kupumzisha mwili, kuepuka matumizi ya kemikali kama pombe kali na vinywaji vyenye nikotini pamoja na kupata vipimo vya kitabibu hasa vya moyo kila baada ya miezi mitatu ili kufahamu mapema matatizo ya moyo wake na kuweza kuyatibu mapema.

Pamoja na ukweli kwamba wanawake wanaishi umri mkubwa zaidi ya wanaume, Daktari Carol . J . Hogue wa Marekani anawashauri wanawake wote kuzingatia afya ya uzazi salama, anaseme miongoni mwa mambo ambayo yanawapunguzia umri wa kuishi wanawake ni pamoja na suala la uzazi. Anasema ili mwanamke aweze kuishi zaidi ya mwanaume ni vema akapanga uzazi. Inaelezwa kuwa kipindi cha mwanamke kujifungua ndicho kinachotajwa kuhatarisha maisha ya wanawake wengi.
 

Makala haya yanazingatia ukweli wa vifo vitokanavyo na hitilafu za udhaifu wa mwili si ajali na majanga mengine kwamba wenye hatari ya kufariki dunia ni wanaume peke yao.
Labels: SAIKOLOJIA