Ijumaa, 16 Novemba 2012

MWAKA MMOJA BAADA BAADA YA KIFO CHA GADDAFI FAMILIA YAKE IKO WAPI?


Mwaka mmoja baada ya kifo cha Gaddafi, familia yake iko wapi?
 22 Oktoba, 2012 - Saa 08:57 GM 

Muamar Gaddafi
Mwaka mmoja baada ya kukamatwa na kuuwa kwa kiongozi wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi tarehe 20 mwezi Oktoba mwaka 2011, familia yake iko wapi?
Watoto watatu wa Gaddafi waliuawa wakati wa harakati za mapinduzi akiwamo aliyekuwa mshauri wake wa usalama wa kitaifa Mutassim Gaddafi, aliyefariki mikononi mwa waasi siku moja na babake.

Jamaa za Gaddafi wanaosalia wamekumbwa na hali tata tangu kifo cha Rais huyo mwezi Oktoba, huku mjane wake akitafuta hifadhi katika nchi jirani ya Algeria, mwanawe na aliyeonekana kama mrithi wa wake Saif al-Islam yuko gerezani nchini Libya akisubiri kusikilizwa kwa kesi yake kuhusu uhalifu wa kivita.
Safiya Gaddafi (Mjane wa gaddafi)
Safiya Farkash, mama wa watoto wanane wa Gaddafi amekuwa akiishi nchini Ageria alikopewa hifadhi kwa sababu za kibinadamu.
Pamoja na wanawe Ayesha na mwanawe wa kambo kutoka kwa mke wa kwanza wa Gaddafi, waliingia nchini Algeria wakati waasi walipoudhibiti mji mkuu Tripoli.
Amepewa hifadhi nchini humo na kuwekewa vikwazo na serikali vya kutotoa matamshi yoyote ya kisiasa wala kuingilia mambo ya Libya
Muhammad Gaddafi (Mwanawe)
Ikiwa mambo yangekwenda vinginevyo Muhammad angehudhuria michezo ya Olimpiki 2012 kama mkuu wa kamati ya michezo hiyo nchini Libya.
Badala yake, Muhammad mwanawe wa kwanza Gaddafi, amekuwa nchini Algeria kwa mwaka mmoja sasa tangu kukimbilia huko wakati waasi walipovamia mji wa Tripoli.
Ni mtoto wa mke wa kwanza wa Gaddafi, Fathia, pia alikuwa mwenyekiti wa kampuni ya taifa mawasliano ya simu za mkononi nchni Libya.
Hatakikani na mahakama ya ICC na hakuhusika pakubwa na kujaribu kuzima harakati za mapinduzi dhidi ya babake mwaka jana.
Saif al-Islam Gaddafi (Mwanawe Gaddafi)
Alionekana na wengi kama ,mrithi wa babake, alikamatwa mwezi mmoja baada ya kifo cha babake, na amekuwa akizuiliwa mjini Zintan tangu hapo.
Alihitimu kutoka chuo cha mafunzo ya uchumi mjini London, na amekuwa sababu ya mvutano kati ya mahakama ya kimataifa ya ICC ambako anakabiliwa na tuhumza za uhalifu wa kivita na maafisa wa sheria nchini Libya ambao wanasisitiza kuwa lazima kesi yake iendeshwe nchini humo.
Idara ya sheria nchini Libaya kwa sasa inaonekana kushinda katika mvutano huo, lakini hakuna tarehe rasmi ya kusikilizwa kwa kesi yake, inaarifiwa kuwa jela ya kifahari ikiwa na uwanja wa mpira wa vikapuni na mpishi wake binafsi vimeandaliwa kwa Saif mjini Tripoli
Saadi Gaddafi (Mwanawe Gaddafi)
Saadi Gaddafi, aliyekuwa mkuu wa shrikisho la soka nchini Libya pamoja na kuongoza vikosi maalum, amepewa hifadhi nchini Niger ambako anaishi katika makao makuu baada ya kutoroka kupitia jangwa la Sahara.
Saadi ana sifa tata ambapo alikuwa akicheza soka katika ligi ya Italia ingawa safari yake ilikatizwa baada ya kuhusishwa na madawa haramu pamoja na maisha yake ya anasa.
Niger imekataa ombi la Libya kumpeleka nchini humo huku waziri wa sheria akisema kuwa huenda akahukumiwa kunyongwa.
Mnamo mwezi Septemba, shirika la Polisi wa kimataifa Interpol lilitoa onyo ambalo litawaruhusu nchi wanachama kamkamata Saadi.
Mwezi Disemba mwaka jana polisi nchini Mexico walisema wana taarifa za kijasusi kuwa magenge ya wafanyabiashara haramu ambao wanajaribu kumhamisha Saadi nchini Mexico kwa kutumia stakabadhi bandia.

Hannibal Gaddafi (Mwanawe Gaddafi)
Hannibal ni mtoto wa tano wa Gaddafi na Safiya Farkash. Inaamini alikuwa kwenye msafara wa magari ya Gaddafi uliokuwa unaelekea nchini Algeria mwaka Jana .
Alikuwa anaongoza majeshi kulinda eneo la Gharyan, Kusini mwa Tripoli, kabla ya waasi kudhibiti Tripoli.
Alisifika kwa tabia zake za anasa na aliwahi kukamtwa akiwa amelewa wakati akiendesha gari aina ya Porsche mjini Paris.
Alizua mgogoro wa kidiplomasia na Uswizi baada ya kuwashambulia wafanyakazi wawili wa hoteli nchini humo na kusababisha babake kuwafunga jela wafanyakazi kutoka nchini humo, na hata kuiwekea nchi hiyo vikwazo.
Aisha Gaddafi (Mwanawe Gaddafi wa kike)
Mwanawe pekee wa kike alipewa hifadhi nchini Algeria pamoja na mamake na ndugu yake.
Siku tatu baada ya kuwasili Algeria, alijifungua mtoto msichana na kumuita Safiya, jina la mamake.
Licha ya kuwekewa ulinzi mkali na serikali ya Algeria, aliripotiwa hivi karibuni kuwataka watu nchini Libya kupindua serikali ya sasa. Kwa usaidizi wa wakili wake Muisraeli, aliitaaka mahakama ya ICC kuchunguza kifo cha babake
Aisha pia aliripotiwa kuunga mkono Algeria katika mechi moja kati yake na Libya akisema kuwa serikali mpya ya Libya haimwakilishi kivyovyote.
Hanaa Gaddafi (Mwanawe wa kuasiliwa)
Kanali Gaddafi alikuwa kwa muda mrefu akidai kuwa Hanaa aliuawa katika shambulizi la Marekani mwaka 1986 wakati akiwa na mwaka mmoja na nusu. Lakini tangu mapinduzi kufanyika, kumekuwa na taarifa kuwa Hanaa yuko hai ingawa hajulikani aliko.
Moussa Ibrahim (aliyekuwa msemaji wa Serikali)

Tarehe 20 mwezi Oktoba, mwaka mmoja baada ya kifo cha Gaddafi, taarifa kutoka kwa ofisi ya waziri mkuu zilisema kuwa Ibrahim alikamatwa na waasi mjini Tarhouna, maili arobaini kutoka mji mkuu.Maafisa wengine hata hivyo walishuku habari hizo.
Kumekuwa na taarifa nyingi kuhusu kukamatwa kwake lakini baadaye ikasemekana kuwa uongo.
Alikuwa mwsemaji wa serikali na kujulikana na vyombo vya habari vya kimataifa, alionekana mwisho mjini Tripoli kabla ya waasi kuudhibiti mji huo.

Kila siku alitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuwahakikishia kuwa serikali itaendelea kuwa imara na kwamba waasi hawatafanikiwa kuiangusha.Alitoka kabila moja na Gaddafi na alijigamba kuishi nchini Uingereza kwa miaka 15 kabla ya kurejea nyumbani.

JE WANASAYASI WANASEMA UKWELI KUHUSU MWANZO WA MWANAADAMU?



Mada ya Yasinta aliyoipa kichwa cha habari kisemacho,Je Binadamu na Nyani ni jamii moja? imenifanya na mimi nifungue mjadala mpya.

Kuna wakati nilisoma habari iliyoandikwa na Bwana
Bwaya juu ya sayansi ya viumbe aliyoipa kichwa cha habari kisemacho;
Viumbe na mabadiliko ya “kubahatisha”

Naomba ninukuu maelezo ya makala hiyo hapa chini;
‘Marehemu Darwin amejaribu kuonyesha kwamba viumbe vilitokea kwa bahati, vikapitia mabadiliko ya uasili wao kufanya asili nyingine iliosababisha kugeuka na kuwa viumbe vya aina nyingine kabisa.Ili kufafanua anachosema Darwin na rafiki zake, tuchukulie mfano wa viumbe kama samaki.

Samaki, kwa mujibu wa kanuni ya “natural selection”, walipitia mageuzi kadhaa yaliyosababisha tofauti katika kundi lao la samaki. Tofauti hizi ziliendelea kuwa kubwa kiasi cha kusababisha kutengenezeka kwa aina fulani ya samaki waliokuja kufanya kundi la viumbe tofauti kabisa na samaki wengine waliobaki.

[Kundi hili linafahamika kama amphibia lenye mifano ya viumbe kama mamba na vyura].

Maana yake ni kwamba katika samaki, walitokea samaki waliokataa asili yao na kufanya asili nyingine iliyosababisha kutokea kwa viumbe vingine. Utetezi wa mabadiliko haya yanayosemwa na akina Darwin, ni mazingira. Kwamba samaki hawa, kwa mfano, waliishi katika mazingira yanayotofautiana kiasi cha kugeuka kwa asili yao.

Kwamba asili hugeuzwa na mazingira kwa maana ya samaki kubadili tabia zake ili kuendana na mabadiliko ya mazingira alimo, ni jambo ambalo linatupasa kufikiri kwa tahadhari.Kwamba asili ya kiumbe ndiyo inayomsaidia kugeuka ili kukabidili mabadiliko katika mazingira yake na kwamba asili yake ilibadilika, ikimtenga na wenzake, ili kufanya kundi lingine linalojitegemea la viumbe jamii nyingine, hilo si jambo rahisi’.

Kisha akaendelea kusema katika makala nyingine aliyoipa kichwa cha habari kisemacho:
Fossil kwa sababu gani?

Katika makala hiyo alisema, naomba kunukuu:

‘Kwa mfano inavyoonekana, maisha hasa ya viumbe yalianzia baharini. Kwa maana hii, viumbe wa kwanza waliishi majini wakibadilika badilika na kuishia kufanya aina nyingine ya maisha yasiyotegemea maji, yaani maisha ya nchi kavu. Sasa katika kuangalia mlolongo huu, tunaambiwa viumbe walijikuta wakijiongezea “viungo” (adaptive features) vilivyowawezesha kukabiliana na aina vyingine ya maisha’

Kisha akaendelea kuandika:

’Kwa ule mfano wetu wa samaki, ni kwamba baadhi ya samaki walianza kupoteza uwezo wao wa kupumua kwa kutegemea maji, na badala yake, wakaanza kuwa na vitu kama mapafu vilivyowasababisha kugeukia maisha nje ya maji. Baadae makoleo yao yaliyotumika kuogelea (fins) yakatengenezeka kuwa (miguu?) ili waweze kuishi vizuri nchi kavu. Na mlolongo kama huo unaotufikisha kwa viumbe kama binadamu.’
Mwisho wa kunukuu.

Labda ningependa kuweka bayana kuwa wakati nasoma habari hii sikuwa mwanablog lakini nilivutiwa sana na habari hiyo ambayo aliiandika kwa kirefu sana.


Hivi karibuni nilikuwa nasoma habari moja juu ya nadharia ya hayati Charles Darwin juu ya wanasaikolojia kutumia Panya katika tafiti zao .

Je Darwin anasemaje kuhusu hili?

Kwa mujibu wa utafiti wake anasema kuwa Binadamu na panya ni viumbe wenye asili moja wanaofanana kitabia,. Wote ni mamalia wanaofanana kisaikolojia.
Mfumo wa viungo vyao vya ndani vinafanana na pia mfumo wao wa ubongo katika mawasiliano unafanana vile vile.

Chembe chembe za kwenye ubongo wa binadamu zinazotumika katika kutoa taarifa unafanana na mfumo wa panya.
Kwa mfano majaribo yoyote ambayo yameshindikana kufanyika kwa mwanaadamu kutokana na sababu mbalimbali za kiusalama yamefanyika kwa panya.

Kwa kawaida Ubongo wa mwanaadamu ni mkubwa kuliko wa panya, lakini ukubwa unapolinganishwa na mwili ni dhahiri kuwa tofauti hiyo itatoweka

Ukweli ni kwamba ukubwa wa ubongo wa binadamu ukilinganisha na wa panya ni kutokana na ukubwa wa kitu kinachoitwa Neocortex.
Hili ni eneo linalohusiana na kuona na kusikia.

Darwin anaendelea kubainisha kuwa mwanaadamu, nyani na panya wana asili moja (common ancestors)

Kwani wanafanana kitabia kwa asilimia kubwa sana kwa sababu wote ni mamalia na wana mfumo wa viungo vya mwili vinavyoshabihiana, na ndio maana ikasemekana kuwa binadamu anatokana na nyani.

Je kuna ukweli juu ya jambo hilo?


Hapa naomba msaada wa bwana Bwaya.

Je Samaki walianza kuwa nyani katika hatua ya kuelekea kuwa wanaadamu, au walibadilika moja kwa moja na kuwa wanaadamu?

Je kama ni hivyo panya wanaingiaje kwenye mkumbo huu?

Nilikuwa najaribu kupitia vitabu mbali mbali vya kisayansi katika maktaba yangu nikakutana na na ndharia nyingi za kuchekesha, kiasi kwamba ziliniacha nimechanganyikiwa.

Kama Bwaya alivyowahi kusema katika mfululizo wa makala zake za kisayansi kuhusiana na nadharia hizi za akina Darwin hata kufikia kumwita Fyatu,

Katika makala yake ya ‘
Sayansi na ghiliba zake

Naweza kukubaliana na yeye.

Lakini ninayo maswali ambayo najaribu kuyatafutia majibu

Hivi nadharia hizi zina ukweli kiasi gani?

Kwa kuwa nadharia hizi ni za miongo kadhaa iliyopita, Je hakuna wanasayansi wapya wanaoweza kutupa jibu sahihi?

Kwa nini tuendelee kuaminishwa na kukaririshwa na nadharia hizi zenye utata?

Je dini nazo zinasemaje kuhusu jambo hili?

Je tusimamie wapi?

Naomba kufungua mjadala.
Shabani Kaluse

Jumatatu, 12 Novemba 2012

SURA YA NNE KUABUDU NA MAOMBI


Katika maombi ya dhati na ya kweli, mtu hujiachia akawa wazi kujieleza na kutoa siri za moyo wake akijua Mungu ndiye msaada wake na kimbillio lake. (Zab. 46:1-3),

“Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoneekana tele wakati wa mateso. Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari, maji yake yajapovuma na kuumuka, ijapopepesuka milima kwa kiburi chake”.

Kwa kutambua ukuu wa Mungu na uwezo wake ndipo ibada ya kweli toka vilindi vya moyo huanza, na mtu hushuka chini sana katika ufahamu wake kumtambua Mungu ni nani na kumwabudu na kumpa sifa katika maombi.

-     Katika hali hiyo ya maombi humfanya mtu ajione si kitu bali astahiliye ni Mungu,
-     Ndipo wengine huanguka chini na kugaragara kuonyesha upendo mbele za Mungu.
“Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke, walakini si kama nitakavyo mimi bali kama utakavyo wewe”. (Mathayo 26: 39)

Hata malaika wanaabudu na kuanguka mbele za Mungu.
Yesu naye aliabudu hata akalia na kutoa machozi ya damu akiomba.
“Naye kwa vile alivyokuwa alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba, hali yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini” (Luka 22: 44)

Ayubu aliomba na kujiachia mikononi mwa Mungu akisema, najua mtetezi wangu yu hai na pasipo mwili huu nitamwona Mungu.

“Lakini mimi najua mteteaji wangu yu hai, na kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, lakini pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu Nami nitamwona mimi nafsi yangu Na macho yangu yatamtazama wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu” (Ayubu 19: 25 -27)


Maombi huvuka mipaka ya mazingira ya mwili wa nyama na kumleta mtu mahali alipo Mungu katika Roho kiasi kwamba muombaji anakuwa na mazungumuzo na Mungu ana kwa ana.
Kama Paulo asemavyo ABA yaani Baba aliye karibu naye kama mwana.

“Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba”. (Warumi 8: 15)

Maombi kama haya yanafanyika katika dhana ya kumtambua Mungu mwenyezi na ukuu wake, uweza wake, mamlaka na nguvu. Kisha moyo wa mtu huyu huzama ndani ya ibada kwa maombi na kumwabudu, na kumpa sifa yeye aliye juu Mungu mkuu. Ufahamu huu unamfanya mtu amheshimu Mungu na kumwabudu kwa mshangao mkuu, na kumvuta kumpenda na kuichukia dhambi, kama Isaya asemavyo,

“Mimi ni mtu mwenye midomo michafu na ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu”. (Isaya 6:1-5)

Petro naye akasema,
“Ondoka kwangu Bwana mimi ni mtu mwenye dhambi”. (Luka 5:8-9).

Heshima hii kwa Mungu huona utukufu wa Mungu ulivyo mkuu na utakatifu wake ulivyo wa ajabu, na kushindwa kustahimili mbele ya Mungu kisha kusema maneno hayo ya unyenyekevu katika maombi.