Jumamosi, 14 Januari 2017

SOMO: MAANA YA WOKOVU SEHEMU YA PILI



MAANA YA WOKOVU (2)
UHAKIKA WA WOKOVU
Kwa hiyo katika sehemu ya kwanza tumeona kwamba kumbe KUOKOKA ni KUNUSURIKA, KUSALIMIKA, KUKOMBOLEWA, KUFUNGULIWA au KUPONA kutoka katika JANGA au HATARI fulani.
Yesu alikuja kuleta wokovu (kuokoa) na Biblia inataja mistari mingi sana juu ya koukoka au wokovu.
Kwa mfano:-
  • Yoh 3:16-18; Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanae wa pekee ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyehamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la mwanawe wa pekee.
  • Luk 9:59; Kwa maana mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, balikuziokoa,

  • Yoh 12:47; Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi si mhukumu, maana sikuja niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu.
  • 1Tim 1:15; Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa ya kwamba, Kristo Yesu alikuja ulimwenguni awaokoe wenye dhambi; ambao wa kwanza wao ni mimi.
  • 1Tim 2:14; Mungu … hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yalio kweli.
  • Efe 2:5,8; Hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo, yaani, mmeokolewa kwa Neema, Kwa maana mmeokolewakwa Neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;
  • 1Kor 1:18; Kwa sababu neno la Msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi, bali kwetutunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
  • Mdo 4:10-12; Jueni nyote na watu wote wa Israel ya kuwa, kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulubisha, na Mungu akamfufua katika wafu … kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. Yeye ndiye jiwe lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limekuwa jiwe kuu la pembeni. Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina lingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Mdo 2:22-24, 36-40, 43-44, 47; Enyi waume wa Israel, sikilizeni maneno haya: Yesu wanazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua; Mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulubisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua; ambaye Mungu alimfufua, akifunga uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao…
Basi nyumba yote ya Israel nawajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulubisha kuwa Bwana na Kristo. Walipoyasikia hayo wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akamwambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa watu wote watakao itwa na Bwana Mungu wetu wamjie. Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi …
Kila mtu akaingiwa na hofu; ajabu nyingi na ishara zikafanywa na mitume. Na wote walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika … Wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwawakiokolewa.
(Mdo 2:22-24, 36-40, 43-44, 47)
Rumi 10:9-10; Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, nakuamini mioyoni mwako yakuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Mdo 16:30-31; Kisha akawaleta nje akasema. Bwana zangu, Yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, mwamini Bwana Yesu nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.
2Kor 6:2; Kwa maana asema, wakati uliokubalika nalikusukia, siku ya wokovunalikusaidia; Tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; Tazama, siku ya wokovu ndio sasa.
Ebr 2:1-3; Kwa hiyo, imetupasa kuangalia zaidi hayo yaliyosikiwa, tusije tukayakosa, kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika, lilikuwa imara, na kila kosa na uasi, ulipata ujira wa haki. Sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukadhibitika kwetu na wale wanaosikia.

SOMO: KUNENA KWA LUGHA SEHEMU YA TATU

Mwl : Furaha Amon







KUNENA KWA LUGHA NI KUJIJENGA NAFSI
Yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake, bali ahutubuye hulijenga kanisa. Na mimi nataka ninyi nyote mnene kwa lugha lakini zaidi sana mpate kuhutubu maana yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha, isipokuwa afasiri ili kanisa lipate kujengwa (1Wakorinto 14:5)
Mkristo anayenena kwa lugha hujijenga nafsi yake na yeye ahutubuye ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha kuhutubu maana yake ni kuhutubia au kuhubiri.
Tafsiri nyingine za Biblia neno kutabiri. Hapo ina maana kuwa wakorinto wakati huo baada ya kujazwa Roho Mtakatifu na kunena kwa lugha kama mkristo angesimama kuhubiri kusanyiko, badala ya kuhubiri kwa lugha inayoeleweka kwa wale anaowahubiria ili waelewe mahubiri anayohubiri au kama alikuwa anafundisha neno la Mungu wale wanaomsikiliza waelewe kilichofundishwa, wakorinto baada ya kuhubiri kwa lugha inayoeleweka wao walianza kunena kwa lugha.
Hili jambo huwa linatokea hata leo, tumeona wakristo wamejazwa Roho Mtakatifu wakafurika sana na wakati huo wakatoka kanisani wakaelekea majumbani kwao na walipokutana na watu njiani walishindwa kuongea lugha zinazoeleweka bali kila alipofungua midomo walianza kunena kwa lugha, lakini pia tumeona wakristo wamejazwa Roho Mtakatifu wakaanza kucheka, wengine wakaanza kuimba.
Wakristo wa jinsi hii wanahitaji mafundisho ili wajue kunena kwa lugha matumizi ya hadhara na matumizi ya faragha. Wasipofundishwa wanaweza kuendeleza unenaji wa lugha usiokuwa na utaratibu na hivyo kuleta makwazo.
Ni kweli kabisa Roho Mtakatifu wakati mwingine huwavuvia watu kwa nguvu sana kiasi analazimika kunena kwa lugha tumeona hata wahubiri mbalimbali wanapohubiri mikutano mikubwa ya injili, wakati mwingine wanajikuta wananena kwa lugha japokuwa huithibiti hali hiyo kutokana na kwamba wao wanajua matumizi ya kunena kwa lugha.
Tumeona hata viongozi wa sifa katika ibada mbalimbali wengine wameshindwa kuongoza sifa wakaanza kunena kwa lugha, tumeona hata waumini wanaochaguliwa kuomba sala mbalimbali kanisani kwa niaba yaw engine, wanaomba lakini lakini katikati ya sala zao wameshindwa kuendelea kuomba kwa lugha inayoeleweka badala yake wamenena kwa lugha.
Paulo ilibidi awafundishe wakorintho kwa sababu hali hii ilizidi sana huko korinto. Wakorinto wao waliona sawa tu kwa vile walikuwa hawajafundishwa matumizi ya kunena kwa lugha. Neno la Mungu linasema, yeye anenaye kwa lugha anajijenga nafsi yake, anayehutubu analijenga kanisa. Anayejenga kanisa analifundisha kanisa neno la Mungu, kwa maana hiyo anayehutubu ni mkuu kuliko yeye anayejijenga nafsi yake peke yake. Anayehutubu anafundisha watu wengi wamjue Mungu. Hapa ina maana kuwa wewe umetakiwa kuhutubia badala yake umenena kwa lugha.
Maandiko yamezungumza  vitu vitatu, kuhutubu,kuomba kwa akili na kunena kwa lugha. Maandiko yanaposema yeye AHUTUBUYE ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha. Haina maana kusema yeye AOMBAYE KWA AKILI ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha. Maandiko yanasema ahutubuye ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, wakristo wengi wanachanganya sana eneo hili. Anayeomba kwa akili hawezi kuwa mkubwa kuliko anenaye kwa lugha. Anayenena kwa lugha anajijenga nafsi yake mwenyewe na anenaye kwa lugha anasema mambo ya siri kati yake na Mungu. Anayeomba kwa akili hawezi kunufaika na Baraka zinazopatikana katika kunena kwa lugha.
“Nami nataka ninyi nyote mnene kwa lugha” (Wakorinto 14:5)
Kuna mafundisho potofu yasemayo kunena kwa lugha si muhimu kwa kila muumini kunena. Viongozi wengine wa dini wamekuwa wakiwazuwia wakristo wanapojazwa Roho Mtakatifu wasinene kwa lugha.
Maandiko yanawakataza wale wanaozuia wakristo kunena kwa lugha, wasizuwie kwa sababu kunena kwa lugha ni muhimu. Mkristo anayeomba kwa akili hawezi kujijenga nafsi yake, wala hawezi kusema mambo ya siri kati yake na Mungu. Hivyo maandiko yanasisitiza kuwa;-
“Wala msizuwie kunena kwa lugha” (1 Wakorinto 14:39)
Kunena kwa lugha ni muhimu sana kwa kila muumini, Wakristo ambao wamekataa kuliwekea kipaumbele jambo hili wana hasara kubwa. Biblia inasema
Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu,kusema Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu (1 Wakorinto 12:3)
Kwa maana hiyo katika kunena kwa lugha hakuwezi kumfanya mnenaji kulaani badala ya kubariki.
HATUJUI KUOMBA
“Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo: lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa” (Warumi 8:26).
Kama tulivyotangulia kusema kwamba Roho Mtakatifu anazifanya kazi zake zote kupitia karama tisa. Roho mtakatifu hutuombea kupitia karama hii ya kunena kwa lugha. Roho Mtakatifu hutuombea kwa sababu sisi hatujui hatujui kuomba, wakristo wengi husema kuwa wao wanajua kuomba sana. Lakini Mungu anajua kuwa sisi hatujui kuomba ndiyo maana Mungu akaweka kazi mojawapo ya Roho Mtakatifu iwe ni kutuombea. Paulo alijua hili ndiyo maana alikuwa ananena kwa lugha kuliko wengine maana yake alikuwa anampa Roho Mtakatifu muda mwingi wa kumwombea.
Wanadamu tuna mipaka ya kuelewa mambo yanayotukia hapa duniani. Huwezi kuelewa mambo yote yanayotokea hapa duniani kwa wakati huo; wanadamu tuna ukomo wa kuelewa. Huwezi kuelewa mambo yatakayotokea wakati ujao; huwezi kuelewa mambo yaliyotokea huko nyuma kabla ya kuzaliwa, huwezi kuelewa mambo yaliyoko katika ulimwengu war oho; huwezi ukaelewa mambo ambayo shetani amekupangia katika ulimwengu wa roho.
Ufahamu wa binadamu una mipaka kutokana na mwili. Mwili ndiyo unaotuwekea mipaka. Roho Mtakatifu yeye hana mipaka. Yeye ni Roho anao uwezo wa kujua mambo yajayo; yanayotendeka wakati huu duniani kote na anajua yaliyotendeka duniani huko nyuma. Kutokana na hili wewe ukiomba kwa ufahamu wako kwa akili zako. Hutaweza kuombea zile shida za muhimu kulingana na uhitaji wako.
Mfano unapoombea siku ya kesho unaombea mambo yaliyo katika ufahamu wako. Hivyo hutajua mambo mengine mengi ambayo shetani ameyapanga kukufanyia siku hiyo ya kesho. Lakini Roho Mtakatifu anajua mitego yote ambayo shetani amepanga kukufanyia siku hiyo ya kesho. Lakini Roho mtakatifu anajua mitego yote ambayo shetani amekutegeshea, ukiomba katika Roho Mtakatifu, atakuombea kwa ajili ya mitego hiyo ya shetani ili Mungu atume Malaika wake ili aitegue mitego hiyo ya shetani. Biblia inasema;-
“Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu” (Warumi 8:27)
Maombi ya Roho Mtakatifu ndiyo maombi ambayo yanampendeza Mungu, Roho mtakatifu yeye anamjua Mungu,maana ametokana na Mungu, hivyo anajua ni jinsi gani Mungu anapenda. Ili maombi yako yawe na uhakika kwa asilimia mia 100% kwamba yamempendeza Mungu basi ni katika kuomba kwa Roho Mtakatifu. Najua unafahamu kwamba kuna aina saba za maombi kwa watakatifu ambayo ni
1.  Kuomba kwa imani
2.  Kuomba kwa jina la Yesu
3.  Kuomba kwa ahadi za Mungu
4.  Maombi ya mapatano
5.  Maombi ya Roho Mtakatifu
6.  Maombi ya kufunga
7.  Kuomba bila kukoma
Kila aina ya kuomba inatakiwa tuitumie, kwa sababu kuna shida nyingine haziwezekani katika aina fulani ya maombi bali inawezekana katika milango mingine. Hivyo kuna mahitaji mengi sana ambayo hayawezekani kwenye milango mingine isipokuwa kwenye mlango huu wa kuomba katika Roho.
KUTUBU DHAMBI
Hakuna dhambi kubwa wala dhambi ndogo, kwa Mungu dhambi ni dhambi zote ziko sawa. Wakristo wengi wanapofikiria kuhusu dhambi wao huzungumzia juu ya dhambi zinazoonekana wazi, ama zile amri kumi za Mungu. Yesu alipokuwa anawaosha wanafunzi wake miguu, Petro alikataa kuoshwa. Yesu akamwambia kama hutaki kuoshwa na mimi basi, basi wewe sio mwenzetu. Petro aliposikia hivyo alisema basi kama ni hvyo basi si miguu tu, nioshe mwili mzima. Aliyeoga si wa kurudiwa kuoga bali kuoshwa vumbi miguu.
Hatujui kuomba jinsi itupasavyo. Roho Mtakatifu hutuombea hata dhambi ambazo tumezitenda tukasahau kuzitubu. Hakuna dhambi ndogo wala kubwa, dhambi ni dhambi tu. Mtu akivaa nguo ya rangi nyeupe safi halafu abebe gunia la mkaa kwenye mabega yake, baada ya dakika tano alitue lile gunia, atajikuta ile nguo nyeupe safi sio safi tena, tena haitamaniki kuvaliwa tena, itakuwa imechafuka hadi ifuliwe. Huo ni uchafu umeingia mara moja, lakini kuna mtu mwingine anafanya kazi ofisini kwenye kiyoyozi naye pia ana nguo nyeupe akienda kazini kwa gari pia lenye kiyoyozi akirudi nyumbani ile nguo inakuwa bado iko safi na anweza kuivaa na siku nyingine, lakini baada ya siku chache inakuwa haiwezi kuvaliwa tena inakuwa imechafuka na kutoa harufu. Hi nguo inakuwa imechafuliwa na uchafu unaoingia kidogo kidogo lakini mwisho umeichafua nguo sawa na Yule aliyeichafua kwa mara moja kwa dakika tano tu. Wakristo wengi wanaona dhambi ni zile kubwa zinazoonekana na watu, dhambi ndogondogo hawazijali wala hawazitubu wanapozitenda. Pamoja na kuokoka kwao hizo dhambi ndogondogo ndizo zinzopeleka watu jehanumu. Dhamb ndogo ndogo ndizo zinaweka kutu kwenye nyaya za simu ya mawasiliano yako na Mungu. Ndipo unakuta mtu wa Mungu pamoja na kuomba sana kwake lakini hapati mpenyo wala hapati majibu. Mawasiliano na Mungu yalishakatika siku nyingi. Mtu wa Mungu unapokuwa unanena kwa lugha, Roho Mtakatifu anakuombea hata dhambi ambazo wewe hujui kuwa hii ni dhambi lakini unazitenda, Roho Mtakatifu yupo kwa ajili ya kukuombea hata hizo dhambi.
Kuna msemo ambao unapenda kutumiwa na Wakristo ambao hawaamini katika kujazwa Roho Mtakatifu na ishara ya kunena kwa lugha kuonekana, kabla ya kuomba hupenda kusema kuwa tujitakase, kwa mtu anayemjua Mungu kujitakasa ni kugeuka na kuacha njia mbaya. Sawa Mungu aliwaambia wana wa Israeli katika mlima wa Sinai kuwa jitakase siku tatu; lakini tunakuta kwenye agano jipya maandiko yanatuambia kuwa sisi baada ya kumpokea Yesu tunakuwa watakatifu.
“Watakatifu walioko dunian ndio walio bora. Hao ndio niliopendezwa nao” (Zaburi 16:2)
Neno la Mungu halisemi tujitakase bali linasema tuzidi kutakaswa. Wakristo wengi msemo huu umewapotosha hivyo wanakuwa bado wanaendelea kutenda dhambi wakitegemea kujitakasa. Haya ni mapokeo yanayotoka kwenye dini yakimtaka mkristo baada ya kutenda dhambi aende kwenye chumba cha kitubio akatubu dhambi mbele ya kasisi, baada ya hapo dhambi zinaondolewa na anapewa malipizi ya kufanya hapo hapo. Sasa mtindo huu umeingizwa kwenye wokovu na baadhi ya watu wasiojua vizuri neno la Mungu. Sasa kwenye wokovu kwa kuwa hakuna kutubu mbele ya wakuu wa dini, bali kwenye wokovu kila mtu anatubu mbele za Mungu, wakristo ambao hawataki kubadili njia zao, hata baada ya kuokoka wamen’gang’ania madhaifu fulani fulani ambayo wanayatenda kila siku, hivyo wanapofikia suala la kumwomba Mungu wanaanza na kujitakasa. Sisemi kwamba kutubu kabla ya maombi hakutakiwi, bali toba hiyo haitakusaidia kama huwezi kugeuka na kuacha kabisa.
Hapa kinachofundishwa hapa ni kukuondoa kwenye wazo la kuendekeza kuwa hata nikitende  dhambi nitajitakasa, hata nikitenda dhambi nitatubu. Inatakiwa kujitakasa kwako kuendane na tendo la kugeuka na kuacha hilo kosa ndipo kujitakasa kwako kutakapokuwa na maana, kujitakasa au kutubu lakini huku unaendelea kuishi kwenye kosa hakutakusaidia. Baada ya kuokoka unatakiwa ujifunze kwa bidii sana neno la Mungu, neno ndilo litakuchonga na kukubadilisha uishi sawa na ulivyojifunza na kutenda sawa na mafundisho siyo kuhusiana na dhambi tu, lakini kuhusiana na maeneo yote ya wokovu, kama kuomba, kushuhudia, kumtolea Mungu, upendo, utakatifu, n.k. mtu akijua neno asipotenda kwake hiyo ni dhambi. Hivyo neno la Mungu ndiyo linalotutakasa, basi kama ni neno la Mungu basi Mungu mwenyewe ndiye anayetutakasa.
“Mtakatifu na azidi kutakaswa” (ufunuo wa Yohana 22:11)
Inatakiwa tujitakase; tutubu lakini huku kusitufanye tukavunja uwezo wa kupambana na dhambi, hivyo tukawa hatuna juhudi katika kuacha kutenda dhambi kwa sababu tunatumainia kuwa tutajitakasa.
Hata hivyo kujitakasa kwa kuomba kwa akili hakutoshelezi, makosa tuliyoyafanya bila ya sisi kujua hatuwezi kuyaombea kwa akili maana akili zetu tayari haiyajui. Kunena kwa lugha ndiyo njia pekee ya kutakaswa. Unajijenga nafsi, mtu anayenena kwa lugha hutakaswa kwa kiwango kikamilifu.
“Unikumbushe; na tuhojiane; eleza mambo yako upate kupewa haki yako” (Isaya 43: 26)
Biblia inasema, nikumbusheni mpate kupewa haki zenu. Mungu amechagua mwenyewe njia ya sisi kumkumbusha ili tuweze kupewa haki zetu. Kuna maombi ambayo umeomba miaka mingi iliyopita lakini maombi hayo hadi 

SOMO: KUNENA KWA LUGHA SEHEMU YA PILI

UMUHIMU WA KALAMA YA KUNENA KWA LUGHA


Pamoja na kwamba Roho Mtakatifu hugawa karama kama apendavyo yeye mwenyewe, kwamba huyu anapewa hii na Yule anapewa ile. Lakini karama ya kunena kwa lugha Roho Mtakatifu amekuwa akiigawa kwa kila mkristo aliyejazwa Roho Mtakatifu. Biblia inasema;-
“Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio: kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;” (Marko 16:17)
Hivyo kutokana na agizo hili, maana yake ni kwamba kila mkristo anayejazwa Roho Mtakatifu amepewa karama ya kunena kwa lugha kama kitu cha lazima.
Kunena kwa lugha ni karama muhimu sana kwa mtu aliyeokoka. Na kwa sababu hii, ndio maana Mungu kupitia  Roho Mtakatifu amekuwa akimgawia kila mkristo. Kwa maana hiyo kila mtu aliyejazwa Roho Mtakatifu, pamoja na karama zingine atakazojaliwa na Mungu kuwanazo lakini karama hii ya kunena kwa lugha ni ya lazima iwe kwa kila mtu aliyejazwa Roho Mtakatifu.
Hivyo kwa mkristo ni lazima kuokoka na kujazwa Roho Mtakatifu, hapo ndio utapewa karama hii ya kunena kwa lugha.
Hii inaonyesha jinsi karama ya kunena kwa lugha ilivyo muhimu sana  katika utendaji kazi kazi wa Roho Mtakatifu ndani ya mtu wa Mungu mmojammoja. Kukosekana kwa karama hii ndani ya mkristo, kutazuwia baadhi ya kazi za Mungu ambazo Roho Mtakatifu anatakiwa kuzifanya kwa kila mkristo mmojammoja, katika maeneo fulani fulani ya kiroho.
Hii itasababisha mkristo asipate baadhi ya huduma za msingi na ambazo ni muhimu sana za Roho Mtakatifu zilizokusudiwa zifanyike kupitia karama hii ya kunena kwa lugha.
Huduma hizi muhimu kiroho ndizo ambazo zimemfanya Roho Mtakatifu ampe kila mtu wa Mungu karama hii ya kunena kwa lugha.
UMUHIMU WA MAFUNDISHO YA KUNENA KWA LUGHA
Wakristo wengi siku hizi wamejazwa Roho Mtakatifu na wakanena kwa lugha. Lakini kutokana na kukosekana kwa mafundisho kama haya wengi wao hawajui madhumuni ya wao kunena kwa lugha, na utendaji kazi wa karama hii ndani yao. Na bahati mbaya sana watu wanaowasimamia pia hawajui umuhimu wa kalama hii.
Hii imesababisha wakristo kuwa hawana nguvu ya kiroho ya kupambana na dhambi na majaribu mbalimbali ya shetani yanayowakabili. Shetani anawaweza na kuwashinda wakristo ambao wamejazwa Roho Mtakatifu, sambamba na anavyowaweza na kuwashinda wakristo ambao hawataki ujazo wa Roho Mtakatifu. Hii imesababisha kutoonekana umuhimu wa kujazwa Roho mtakatifu.

BIBLIA IMETOA NAFASI KUBWA
Maandiko yanaonyesha jinsi kunena kwa lugha kulivyo muhimu sana.  Ukisoma katika Biblia kitabu cha Wakorinto wa kwanza sura yote ya kumi na nne inazungumzia habari za kunena kwa lugha tu.
Karama zingine zote zimeelezwa kwa sentensi moja au neno moja tu. Lakini karama hii imeelezwa kwa kirefu katika sura nzima. Hii ni kuonyesha jinsi ambavyo karama hii ilivyo muhimu na ya lazima katika maisha ya kila siku ya mkristo.
Unaweza kusoma sura yote ya kumi na nne, lakini mimi nachukua mstari mmoja katika sura hiyo unaosema;-
Maana yeye anenaye kwa lugha hasemi na watu bali husema na Mungu maana hakuna asikiaye lakini anena mambo ya siri katika roho yake (1Wakorintho 14:2)
Biblia inasema mtu anapokuwa ananena kwa lugha huwa anasema mambo ya siri katika roho yake. Kwa maana nyingine ni kwamba, hii ndio njia pekee ambayo Roho Mtakatifu huitumia ili mkristo amweleze Mungu mambo ya siri kati yake na Mungu.
Sasa hapa ni rahisi sana kwa mtu mwenye mafunzo ya kivita kujua umuhimu wa mawasiliano katika mapambano yeyote. Ndio maana majeshi yote ni lazima yawe na mfumo wa mawasiliano ambao mtu mwingine hawezi kuelewa hata kama anasikia! Hata katika mapambano ya kiroho ni hivyohivyo pia, adui huwa anataka kujua unaongea nini na Mungu. Na hivyo anaweza akakupiga au akajihami kulingana na habari alizopata. Kwa maana hiyo kama hujui kunena kwa lugha unakuwa umepoteza fursa ya kuongea mambo ya siri baina yako na Mungu.
Maandiko hayo tuliyoyasoma yametupa maana ya kunena kwa lugha. Hivyo tumeona kuwa, kumbe kunena kwa lugha ni kuongea na Mungu. Kuongea na Mungu maana yake huko ndiko kuomba. Roho Mtakatifu huitumia midomo ya muhusika kuzungumza na Mungu kwa niaba ya muhusika. Hii ndio njia ambayo Roho Mtakatifu huitumia kuwaombea watu wa Mungu, kama tulivyoainisha baadhi ya kazi mojawapo ya Roho Mtakatifu ni kutuombea. Na hutuombea kwa njia hii, kwa watu ambao hufikiri kwamba Roho Mtakatifu huweza kumuombea mtu bila muhusika kunena kwa lugha wanajidanganya wenyewe. Huwezi ukamwabudu Mungu kwa kutumia taratibu za kubuni mwenyewe, nimetanguliza kukueleza kuwa Roho Mtakatifu huzifanya kazi zake zote kupitia mojawapo ya karama tisa. Kazi mojawapo ya Roho Mtakatifu ni kukuombea. Roho mtakatifu huifanya kazi hii kwa kupitia karama ya kunena kwa lugha nje ya hapo hakuna.

KUOMBEWA NA ROHO MTAKATIFU
Wakristo waliojazwa Roho Mtakatifu na ishara ya kunena kwa lugha ikaonekana hata wao pia hawawezi kuombewa na Roho Mtakatifu wakati hawaneni kwa lugha. Roho Mtakatifu huwaombea watu wakati wakinena kwa lugha pekee. Kutokana na hili wakristo wengi waliojazwa Roho Mtakatifu, na ishara ya kunena kwao kwa lugha hawaitumii ipasavyo, inakuwa haina maana kwao. Wala huwezi kuwatofautisha na wakristo ambao hawajajazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu wao nao wamekosa kuitumia fursa na Baraka zinazotokana na kunena kwa lugha, sawasawa na ambavyo wamekosa wakristo ambao hawajajazwa Roho Mtakatifu.

TATIZO LA WAKORINTO
Kanisa la korinto lilikuwa limebarikiwa sana na karama hii. Lakini, hata hivyo hawakujua matumizi na madhumuni ya karama hii ya kunena kwa lugha. Ndipo Paulo alipowaandikia waraka akiwafundisha. Kanisa la Korinto lilibarikiwa kwa karama zote tisa zikifanya kazi. Lakini  kanisa la leo karama hazionekani, kwa sababu ya upeo mdogo wa kulijua neno la Mungu.
Wakristo hawafundishwi kwa undani kuhususiana na karama na jinsi zinavyofanya kazi, pia wakati mwingine karama zinazuiwa zisifanye kazi kanisani kwa makusudi, pengine tu kwa viongozi kutokuwa na ujuzi Paulo anasema;-
Wala msizuie kunena kwa lugha (1 Wakorinto 14:39)
Kunena kwa lugha ni muhimu sana kusizuiwe bali waumini wafundishwe jinsi ya kuitumia karama hii ili isilete makwazo bali ilete Baraka.
Mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu (1 Wakorinto 14:40)
Paulo ilibidi awafundishe wakorinto. Baada ya kujazwa Roho Mtakatifu na ishara ya kunena kwa lugha kuonekana. Wakorinto walifurahi sana, lakini hawakujua matumizi ya kunena kwa lugha, kutokujua matumizi ya karama hii kulileta makwazo.
Waumini hawakutaka tena kuomba kwa akili, Kila walipotaka kuomba wao walinena kwa lugha. Hata kama mmoja wao alitakiwa kuomba sala kwa niaba ya wengi, aliomba hiyo sala kwa kunena kwa lugha.
Mfano ndugu fulani ameombwa kuombea chakula wanachotaka kula, yeye aliombea chakula hicho kwa kunena kwa lugha na baadaye kusema amina.
Ndugu fulani anaombwa kwa ajili ya kufunga ibada au kwa kufungua ibada, huyu ndugu anaomba kwa kunena kwa lugha. Kumbuka kuna matumizi ya aina mbili ya kunena kwa lugha, aina ya kwanza ni matumizi ya hadhara na aina ya pili ni matumizi ya faragha. Unapoomba kwa niaba ya wengine au unapoomba kwa kuwakilisha wengine, unaomba kwa niaba yao ni muhimu wasikie yale unayoomba na wayaelewe. Hivyo unatakiwa uombe kwa kutumia akili zako na kwa lugha inayoeleweka kwa hao unaowawakilisha ili nao waelewe ulichoomba. Haya ndiyo matumizi ya hadhara ya kunena kwa lugha, Paulo anasema,
Nashukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote; lakini katika kanisa napenda kunena maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno elfu kumi kwa lugha. (1Wakorintho 14: 18 – 19).
Paulo anatuambia anapoomba kanisani kwa niaba ya wengine alikuwa anaomba kwa akili yaani kwa lugha inayoeleweka kwa wengine. Inapobidi kunena kwa lugha alinena maneno matano, lakini zaidi alikuwa anaomba kwa akili zake ili wengine waelewe ni nini ambacho anaomba.
Pamoja na hilo Paulo anasema yeye ndiye alikuwa ananena kwa lugha kuliko waumini wote. Sasa hapo ni lazima tujiulize swali na kujijibu. Swali je? ni wakati gani ambapo Paulo, aliweza kuhakikisha kuwa amenena kwa lugha kwa kutumia muda mwingi sana hadi ahakikishe kwamba yeye ananena kwa lugha kuliko wengine wote. Jibu ni kwamba, huu ulikuwa ni wakati wa maombi yake mwenyewe binafsi, maombi ambayo sio ya kuomba sala fulani kwa niaba ya wengine. Maombi haya hata kama utakuwa unayaomba ukiwa katikati ya waumini lakini ni maombi ambayo mtu mwingine hana umuhimu wa kuelewa kuwa unaomba nini.
Maombi haya pia unaweza kuwa katikati ya waumini wengi sana kila muumini anaomba kivyake. Maombi ya jinsi hii yanaitwa maombi ya faragha, maombi binafsi. Maombi ya faragha ndiyo unayotakiwa ujenge nafsi yako, pia ndiyo unatakiwa uyatumie ili uongee mambo ya siri kwa Mungu, haya ndiyo maombi unayotakiwa unene kwa lugha. Maombi haya ambayo Paulo anasema;-
Nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote (1 Wakorinto 14:18)
Matumizi ya hadhara ya kunena kwa lugha maandiko matakatifu yanasema ni ishara ya kuonyesha kuwa wewe umeokoka na umejazwa Roho Mtakatifu. Biblia inasema,
Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio watasema kwa lugha mpya (Marko 16:17)
Pamoja na ishara zingine zilizotajwa katika Marko 16:17 na 18 ambazo ni kwa jina langu watatoa pepo watasema kwa lugha mpya watashika nyoka hata wakinywa kitu cha kufisha hakitawadhuru kabisa na wataweka mikono juu ya wagonjwa nao watapata afya. Tunaona ishara ya kunena kwa lugha ni mojawapo.
Kunena kwa lugha ilitumika kwa matumizi ya hadhara katika siku ile ya pentekoste wakati wanafunzi wa Yesu mia moja na ishirini walipojazwa Roho Mtakatifu na wakaanza kunena kwa lugha. Tukio hili lilipelekea watu wengi kukusanyika na kuanza kushangaa.
Wakristo wengi kwa kukosa mafundisho wanakutumia kunena kwa lugha kwa Matumizi ya hadhara pekee ambayoni ISHARA. Kususdi la Mungu kuiweka karama hii ya kunena kwa lugha ni zaidi ya ishara, karama hii ipo ili Roho Mtakatifu aweze kutusaidia kuomba maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo kuomba. Kupitia somo hili tunahitaji watu wajifunze kazi kubwa ya karama hii ili ufaidike na Baraka nyingi sana zipatikanazo katika karama hii. Wakristo kwa vile hawajui matumizi ya faragha na ya hadhara ya kunena kwa lugha wanachanganya matumizi. Hili limewafanya kuzikosa Baraka zilizoko kwenye kunena kwa lugha. Biblia inasema;-
Yeye anenaye kwa lugha na aombe kutafsiri. Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; nitaimba kwa roho tena nitaimba kwa akili pia;kwa maana wewe ukibariki kwa roho yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikiaje, amina baada ya kushukuru kwako, akiwa hajui uyasemayo? Maana ni kweli wewe washukuru vema, bali Yule mwingine hajengwi (1 Wakorinto 14: 13 – 17)
Maandiko haya, Paulo anawafundisha wale wakristo waliokuwa wanataka kunena kwa lugha wakati wwa sala za hadhara. Paulo anasema iwapo kunena kwa lugha kutatumika katika sala ya hadhara basi uhakikishe unatafsiri hiyo sala ili na wenzako unaoomba kwa niabayao nao wasikie unayoyaomba. Hivyo wewe kama unapenda kutumia kunena kwa lugha katika matumizi ya hadhara ni sawa lakini uombe Mungu akupe karama ya kutafsiri lugha. Lakini unapokuwa unanena kwa lugha maombi yako wewe binafsi hapo hakuna haja ya kutafsiri.
Karama za uvuvio yaani unabii, kunena kwa lugha na tafsiri za lugha. Karama hizi mtu anayetumiwa anakuwa na uwezo wa kunena kwa lugha mahali popote na unao uwezo wa kutokunena kwa lugha.
Japokuwa umejazwa Roho mtakatifu. Kama unayo karama ya unabii unao Roho Mtakatifu anayo hekima sio dikteta hivyo utendaji wake katika karama ya kunena kwa lugha kutategemea na wewe unavyomruhusu, wakristo weni wasiojua sana habari za kunena kwa lugha hufikiri kuwa unaponena kwa lugha Roho Mtakatifu ni lazima aje kwa nguvu kubwa ambayo itamfanya anayenena kwa lugha anene kwa nguvu na kwa sauti kubwa sana. Hii sikatai inakuwa hasa kwa mkristo ambaye ndio amejazwa Roho Mtakatifu katika siku zake za mwanzo za kunena kwa lugha mkristo huyu kwa vile hajazowea mdomo wake kutumiwa na Roho Mtakatifu inabidi Roho Mtakatifu atumie nguvu kubwa ili kuufanya mdomo uongee anayotaka Roho mtakatifu. hii pia inatokea kwa wakristo ambao hawana mazoea ya kunena kwa muda mrefu kila siku. Pia hutokea kwa waristo ambao walikuwa wananena kwa lugha hapo zamani baadae wakamzimisha Roho Mtakatifu sasa inapotokea wameanza kunena kwa lugha tena Roho Mtakatifu huja kwa nguvu kubwa.
Mkristo ambaye ni mnenaji kwa lugha wa kila siku au mara kwa mara na katika unenaji wake kwa lugha anaponena kwa lugha ananena kwa masaa mengi, Roho Mtakatifu hahitaji kutumia nguvu kubwa kwa mkristo huyu. Hivyo mkristo wa 
Mwl: Furaha Amon

namna hii anaweza kunena kwa lugha kwa ulaini na anaweza hata kutumia sauti ndogo kiasi chochote anachotaka yeye hivyo anaweza asiwakwaze kwa kuwapigia kelele watu waliomzunguka.
Hapa nataka kuzungumza kuwa mkristo anaweza akanena kwa lugha kwa kutumia sauti ndogo au kwa kutumia sauti kubwa kutegemeana na maamuzi yake mwenyewe hivyo hata kama mahali ulipo uhuru ni mdogo usiache kunena kwa lugha kwa sauti ya kunon’goneza basi iwapo kuna uhuru omba kwa sauti yeyote unayoweza.

usikose kufuatilia sehemu inayofuata ya somo hili na kama unahitaji msaada zaidi tunaweza kuwasiliana kwa simu 0677 609056