Ijumaa, 28 Aprili 2017

JINSI YA KUFANYA MAMBO MAGUMU KUWA RAHISI




Ni rahisi kufanikisha jambo lolote, ikiwa jambo hilo utataanza kulifanya mara moja na kuacha kusubiri.

Ni rahisi kujifunza kitu kipya kwenye maisha yako, ikiwa utaamua kweli kujifunza kila siku.
Ni rahisi kutoka kwenye kushindwa, ikiwa kama utachukua jukumu la kujaribu tena na tena.

Ni rahisi kusogea hapo ulipo kimaisha, ikiwa utaweka nia na juhudi kubwa ya kutaka kutoka hapo ulipo na kwenda ngazi nyingine kimafanikio.

Ni rahisi kuwa na watu wanaokutia moyo, ikiwa wewe utaamua kuwa wa kwanza kuwatia moyo wengine kufanikiwa.

Ni rahisi kuweka akiba na kuanza kukuza utajiri, ikiwa kuanzia leo utaamua kuanza utekelezaji.
Ni rahisi kukamilisha lile jukumu ambalo linasemwa sana kwamba, haliwezekani, ikiwa wewe utaligawa jukumu hilo na kuanza kulifanyia kazi.

Ni rahisi kuongeza kipato chako, ikiwa utajifunza kuwekeza hata kama ni kidogo katika maisha yako.
Ni rahisi kuyafanya maisha yako yakawa na maana, ikiwa kila siku utachukua jukumu la kufanya mabadiliko kidogo kidogo.

Maisha yako yanaweza kuwa kama unavyotaka yawe wewe, ikiwa wewe kwanza utachukua jukumu la kuyafanya maisha yako yakawa rahisi.

Acha kufanya mambo au maisha yako yakaonekana magumu sana hasa kwa zile hali ambazo ulikuwa unaweza kuzibadili kabisa.

Kumbuka, Ni rahisi kuanza jambo jipya, ni rahisi kujaribu tena pale uliposhindwa, ni rahisi kufikiri jinsi utakavyofanya maisha yako yakawa bora zaidi, sasa jiulize ni wapi unaposhindwa?

Kwa jinsi unavyofanya kidogo kidogo kwa yale mambo yanayoonekana magumu, siku hadi siku, kuna wakati utakamilisha mambo hayo magumu na hutaweza kuamini.

Kila wakati Jifunze kufanya mambo magumu kuwa rahisi.
Endelea kujifunza kupitia furahisha.blogspot.com kila siku.

MBINU ZITAKOZOKUPA MAFANIKIO KWA WAKATI SAHIHI

 

 Asilimia kubwa ya maisha ya watu duniani midomo yao hutamka ya kwamba wanataka kufanikiwa. Lakini ni idadi ndogo sana kati ya idadi kubwa ambao wanapata mafanikio hayo. Ikiwa ni pamoja ya kwamba watu wote tunaishi katika mazingira ambayo yanafanana.

Tukiangalia wote tuna masaa 24 kwa siku,  wote tunatumia hewa safi ambayo hatulipii hata senti moja kwa ajili ya hewa hiyo,  watu wote tunaishi katika maeneo ambayo mazingira yake yana kila aina ya rasimali ambazo kama tutaamua leo kuzitumia vyema zina uwezo wa kubadilisha maisha yetu.

Swali linakuja sasa ni wapi ambapo panatutofautisha kati ya watu wenye mafanikio na wasio na mafanikio? Ikiwa wote tunaishi mazingira ya aina moja.

Kitu kikubwa ambacho kitakusaidia kupata aina hiyo ya mafanikio au kujua ni wapi panapotutofautisha ni kujitambua. Hapa ndipo ilipo siri ya mafanikio na ambayo unatakiwa uielewe.

Kujitambua ni sehemu ambayo kila msaka mafanikio lazima aijue vyema.  Kujitambua huwa na uhusiano  mkubwa uliopo kati ya kitu ambacho unahitaji kukifanya. Kujua ni kile unachokitaka ndo siri ya kupata mafanikio yako.

Watu wengi kutokana na changamoto za kimaisha wamekuwa wapo tayari kufanya jambo lolote, mfano hivi hajawahi kukutana na mtu anakwambia yupo tayari kufanya jambo lolote?

Bila shaka umewahi kukutana na mtu huyo,  ila ukweli ni kwamba kufanya hivi ni kuchelewa katika safari yako ya mafanikio na mafanikio. Kwani ukitaka kufanikiwa ni lazima ujue kila unachotaka kufanya kutoka nafsini mwako.

Unaweza kujiuliza maswali haya ili kuweza kujitambua na  hatimaye kupata mafanikio yako. 
1. Wewe ni nani?
2. Unataka kufanya nini?
3. Umetoka wapi?
4. Upo wapi?
5. Na unaelekea wapi?

Maswali hayo yote msingi wake wa mkuu ni kujiuliza lengo lako la kuja duniani ni nini?

Ukipata majibu ya maswali hayo tafadhari nakuomba uyaandike katika daftari lako na kuyachukulia hatua mathubuti, kufanya hivyo kila wakati ni hatua za kuweza kufanikiwa.

Endelea kujifunza kupitia furahisha.blogspot.com kila siku.




FANYA MAMBO HAYA, KUTENGENEZA MAISHA YA MAFANIKIO UNAYOTAKA.



Inawezekana una ndoto au mipango ya kuishi maisha ya namna fulani ambayo unayoyataka. Je, kitu cha kujiuliza, ulishawahi kujua utawezaje kushi maisha hayo unayoyataka?

Je, ni mikakati ipi ambayo umeweka hadi uweze kufikia hatua ya kuweza kutengeneza maisha unayoyataka? Kwa kawaida bila hata kuumiza kichwa, yapo mambo ya kuzingatia ili yakusaidie kuishi maisha unayoyataka.

Haya ni mambo ya msingi sana ambayo ukizingatia yatakusaidia uweze kutengeneza maisha bora unayohitaji. Unajiuliza ki-vipi, hapa nikiwa na maana maisha ya ndoto zako, ikiwa lakini utachukua hatua.

Ni mambo gani ambayo unatakiwa kufanya ili kutengeneza maisha ya mafanikio unayoyataka? Hebu fuatana nami katika makala haya ili tuweze kujifunza kwa pamoja.

1. Tambua kitu unachokitaka.

Ikiwa haujui kile unachotaka vizuri kwenye maisha yako, usije ukashangaa ukaendelea kuwa mtu wa kutokuwa na mafanikio karibu kila siku. Kabla hujapata kitu chochote kwenye haya maisha lazima uje ni kipi unataka.

Watu wengi wanakwama sana kwenye maisha kwa sababu ya kutokujua vizuri wanachotaka. Chukua muda wako kidogo ulionao na kisha kitambue kile unachokitaka kwenye maisha yako.

2. Tengeneza mfumo wa kufikia hicho unachokitaka.
Kwa kuwa umeshakijua hicho unachokitaka katika maisha yako, sasa hapa unatakiwa kutengeneza mfumo wa kuhakikisha unakikamilisha kitu hicho. Unatengeezaje huo mfumo? Ni kwa kufanya kila siku.

Acha kusimamishwa na kitu chochote. Weka nguvu za uzingativu na fanya kila siku mpaka malengo yako yatimie. Ikiwa utafanya kila siku, uwe na uhakika baada ya muda utafikia kile unachokitaka.

3. Weka juhudi sana.               
Wakati unapokuwa umejiwekea mikakati ya kudfika kule unakotaka kufika kuna ni rahii tu kujikta unashindwa kufanikisha adhima hiyo ikiwa huataweka juhudu sana.

Unatakiwa uweke juhudi kuhakikisha mpaka unafanikiwa. Hakuna kulala katika hilo jitahidi sana ufanye kila linawezekana mpaka kuona kila kitu kinakaa sawa.

4. Weka nguvu za uzingativu kwa hicho unachokifanya.
Usijiruhusu ukawa mtu wa tamaa, wakati upo kwenye harakati za kutengeneza maisha unayoyataka wewe. Kati ya kitu kinachowaangusha watu ni pamoja  na tamaa ya kutaka kufanya mambo mengi kwa pamoja.

Ni muhimu nguvu zako ukaziweka sehemu moja. Hata ikitokea jambo zuri vipi, kipindi ambacho unatengeneza maisha unayoyataka, ukishaweka nguvu ya uzingativu usilifanye jambo hilo. Kitu cha msingi ujifunze kutulia ili kufikia mafanikio yako.

5. Jifunze kila siku juu ya kitu hicho.
Njia ya kufikia mafanikio mara nyingi ni njia ambayo haijanyooka kabisa kama baadhi wanavyofikiri. Zipo changamoto nyingi zinazojitokeza. Kila zinapotokea changamoto hizo amua kujifunza na kujirekebisha kwa kufanya upya kila siku

Pale unapokutana na changamoto za aina yoyote ile hutakiwi kukata tamaa na kutaka kurudi nyuma. Kitu cha muhimu ni kujifunza na kufanya hadi uone umeweza kufikia lengo la kuishi maisha unayotaka.

Unatakiwa uamua kujifunza juu ya kitu ambacho umeamua kukifanya mpaka uwe mtaalamu kabisa tena uliyebobea. Kwa hali, hiyo itakusaidia sana kuweza kuishi maisha unayoyataka.

Mwisho, mtu kuishi maisha anayoyata sio ajali wala bahati. Unaweza ukaishi maisha unayoyataka ikiwa utatengeneza mfumo huo na kuzingatia mambo haya muhimu kama tulivyoyaangalia kwenye makala haya.

Usiendelee kusubiri sana leo, chukua hatua na tengeneza maisha unayoyataka.

MATAIFA 5 YANAYOPINGA UWEPO WA MUNGU



Utafiti Unaonesha kwamba 63% ya watu duniani wanaamini uwepo wa Mungu, yafuatayo ni Mataifa 5 yanayoongoza kwa idadi kubwa ya watu wasiyoamini uwepo wa Mungu (Atheism).

1. China. 
Ikiwa na wapagani asilimia 30%, huku asilimia 47% ya watu hawaamini kabisa kama Mungu yupo.

2. Japan. 
Ikiwa na asilimia 31% ya wapagani, huku asalimia 31% ya wajapani hawaamini kabisa kama Mungu yupo.

3. Czech Republic. 
Ikiwa na 48% ya wapagani, huku asilimia 30% ya wananchi wanasema kwamba Mungu hayupo.

4. France. 
Asimilia 29% ya wafaransa hawaamini kabisa kama Mungu yupo.

5. Korea Rep (South). 

Ikiwa asamilia 15% watu wasioamini kwamba Mungu yupo.

KWA NINI WAAJIRIWA WENGI HUWA MASIKINI ?


Umaskini ndani ya kundi la wasomi unazidi kuingia kwa kasi ya ajabu kadili siku zinavyozidi kwenda. Kundi la watu ambao wako kwenye hatari kubwa zaidi ni hasa wale walioko kwenye “ajira”. Ukweli ni kwamba watu wengi walioko kwenye ajira, kitu pekee wanachouza ili kupata kipato ni “nguvukazi” tena ambayo bado ni “ghafi”.  

Uzoefu unaotokana na tafiti zilizofanywa, unathibitisha kuwa zipo sababu nyingi zinazosababisha waajiriwa na hasa wasomi wengi kuwa maskini. Lakini kubwa zaidi ni utamaduni wa wasomi kuendelea kuuza nguvukazi ikiwa bado ni “ghafi” (nguvukazi ambayo haijachakatwa).

Katika ulimwengu wa “uwekezaji” nguvu kazi ghafi ni mtaji muhimu sana, ambao ukichanganywa na mitaji mingine kama vile mashine, una uwezo wa kuzalisha bidhaa na huduma zenye thamani kubwa kwa watu wengine.

Ukiuza nguvukazi ghafi unakuwa umeuza “mtaji” wako: Waajiriwa wengi wanaendelea kukumbwa na adha kubwa ya umasikini kutokana na kushindwa kutambua ukweli kwamba mara nyingi kwenye maisha ya ajira wamekuwa wakifanya zaidi biashara ya kuuza mtaji walionao (nguvukazi) kwa matajiri wenye hitaji la mitaji.

Ikumbukwe kuwa, ili uweze kuzalisha bidhaa na huduma unahitaji mitaji ya aina mbalimbali ikiwemo nguvu kazi ghafi. Ndiyo maana matajiri wengi wanapendelea zaidi kununua mitaji kwa ajili ya kuzalisha bidhaa na huduma, ambazo huwapatia faida kubwa sana. 

Katika biashara yoyote duniani, kuuza mtaji ni kufirisika jumla. Kwahiyo, umasikini tulionao umetokana na kuuza mtaji wetu kila siku tunapotumikia ajira zetu. Kwa maana nyingine waajiriwa wengi wanafirisika kila siku ya pale wanapokwenda kazini.

Watu wanaouza zaidi nguvu kazi ghafi wanabaki kuwa maskini kutokana na ukweli kwamba thamani ya nguvu kazi ghafi huwa ni ndogo sana, kwasababu inapatikana kwa wingi na haina usumbufu kuipata. 

Kwa mfano: ukijifanya kutoza bei kubwa nguvu kazi yako; waajiri wengi watakukimbia na chapuchapu watapata watu wengine wenye kuuza nguvu kazi ile ile kwa bei nafuu sana.

Hivi ndivyo unavyouza nguvu kazi ghafi: Unauza nguvu kazi ghafi pale unapotumia nguvu yako kufanyakazi ya kuzalisha bidhaa na huduma ambazo siyo mali yako bali ni mali ya mtu aliyekuajiri (mwajiri).

Unahitaji kufahamu kuwa, mwajiri amekuajiri ili umpatie (umuuzie) nguvu kazi ambayo ni mtaji wa kuzalisha bidhaa na huduma ambazo ni mali yake binafsi. 

Kwakuwa bidhaa zinazozalishwa ni za thamani kwa watu wengine, basi ni wazi kwamba watu hao watampatia pesa mwajiri wako ili kupata bidhaa; LAKINI hawatakupatia pesa wewe, kwa sababu wewe unayo nguvu kazi peke yake, ambayo siyo hitaji muhimu kwa wateja wenye pesa zao. 

Ukiuza nguvukazi ghafi unauza “muda” wako: Kwakuwa umeajiriwa kwa madhumuni ya kutoa nguvu kazi kwa mwajiri wako, basi thamani yako inapimwa kwa kuangalia muda unaoutumia kufanya kazi.

Ili uweze kulipwa ni lazima kila siku ufike kazini na kusajiri muda wako. Usipoonekana kazini hakuna malipo yoyote, kwasababu muda wako utakuwa hujauwekeza kwa mwajiri. 

Kwahiyo, unapouza nguvu kazi ghafi basi ujue umeuza “muda” na binadamu wa kawaida hawezi kufanya kazi zaidi ya masaa nane kwa siku. Masaa yote haya unafanya kazi bila kupumzika na kuzalisha vitu vyenye thamani kubwa kuliko mshahara unaolipwa na mwajiri wako. 

Haijalishi, thamani ya vitu vilivyozalishwa ni kubwa kiasi gani, mshahara wako unaolipwa unaendelea kubaki pale pale kila mwezi. Hali hii ndiyo inakufanya wewe mwajiriwa kukosa muda wa kufanya vitu vyenye kukuletea faida kubwa na mafanikio maishani, na hivyo kuzidi kuwa maskini kadiri umri wako unavyoongezeka.

Ukiuza nguvukazi ghafi huna cha kurithisha familia yako: Kama unauza nguvukazi ghafi siyo rahisi kuirithisha kwa watu wako wa karibu, kwasababu nguvukazi kama ilivyo haihamishiki kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Kama kitu hakihamishiki ni vigumu pia kukibadilisha kwa urahisi kuwa pesa.

Hali hii inazidi kutukumba wasomi na waajiriwa waliowengi kutokana na ukweli kwamba unakuta umeajiriwa kwenye kampuni kubwa na una cheo kikubwa lakini ukifukuzwa au kufariki, haitokei mke au mtoto wako akapewa nafasi kama uliyokuwa nayo na wala familia haiwezi kutumia vyeti vyako vya elimu kuomba kazi.

Lakini kama ungekuwa kwa mfano umeandika vitabu, hata ukifa hakimiliki ya kuendelea kuvichapisha na kuviuza inahamishiwa kwa warithi wako na wanaendelea kufaidi sawa na wewe ulivyokuwa ukifaidi.

Ukiuza nguvukazi ghafi unapata hasara: Hasara kubwa unayoipata kutokana na kuuza nguvu kazi ni pale unapoishia kuuza kitu kimoja tu! Nacho ni nguvu kazi.

Hali hii inakubana kiasi kwamba unajikuta unalazimika kumtegemea mteja mmoja ambaye ni “mwajiri” na inakuwa siyo rahisi kubadilisha mteja kadiri unavyotaka.

Endapo ukiamua kuchakata nguvukazi yako na hatimaye kuzalisha bidhaa na huduma za thamani ni rahisi kupata wateja wengi, ambao ndio huleta mapato makubwa.

Hasara nyingine unayopata pindi unapouza nguvu kazi ghafi ni kuendelea kubaki kwenye kundi la watu maskini ambao wanapata kipato hai (active income), yaani unapata pesa unapofanya kazi tu, ukiacha pesa hakuna. Endapo, ikitokea unaumwa au umesafiri basi ujue hakuna pesa itakayoingia.

Ndiyo maana unakuta mtu ni tajiri leo kwasababu anafanya kazi ya kibarua, lakini baada ya muda mfupi unakuta ni maskini na kwa waajiriwa ni hivyo hivyo wanakuwa na pesa wakiwa bado kazini LAKINI wanapostaafu ajira wanarudia kwenye hali ya umaskini jambo ambalo huwafanya watu wengi kufa miaka michache baada ya kustaafu.

Washindi dhidi ya umaskini ni wale walioamua kuchakata nguvu kazi yao: Ukweli ni kwamba kila mchakato wowote lazima utoe matokeo. Matokeo ya kuchakata nguvu kazi ghafi ni “bidhaa au huduma” zenye thamani kubwa kwa watu wengine.

Kitendo cha kuchakata nguvu kazi kinatokana na matumizi ya nguvu ya akiri pamoja na nguvu ya mwili kwenye rasilimali kama ardhi, maliasili, ujuzi, pesa n.k, kwa lengo la kupata mali au bidhaa kwaajili ya watu wengine. 

Ukishapata bidhaa zenye thamani (manufaa) kwa watu wengine, basi mara moja watakuletea pesa ili kujipatia bidhaa na huduma muhimu kutoka kwako. Kadiri utakavyotengeneza bidhaa nyingi na zenye thamani kubwa ndivyo utakavyopata pesa nyingi ambayo haina kikomo. 

Ni wakati sasa tuamke na tujibidishe sana kwa kuandaa mazingira yatakayotuwezesha hasa sisi wataka mafanikio kuuza “matokeo” ya nguvu kazi badala ya utamaduni wa sasa wa kuuza nguvu kazi ghafi.

Ukweli ni kwamba, unapokuwa mtu wa kuuza matokeo ya nguvu kazi ambayo ni bidhaa na huduma mbalimbali, tayari unakuwa umemaliza kazi, kinachofuatia ni kuendelea kuuza bidhaa hizo na wakati huo huo unakwenda kuwekeza muda wako huo kwenye kuzalisha vitu vingine, huku akiendelea kufaidi matunda ya kazi aliyoifanya mwanzo.

Kwa watu wote na hasa waajiriwa tunaotaka mafanikio makubwa, ni lazima kila mmoja wetu ajiwekee tarehe ya mwisho ya kuacha kuuza nguvu kazi ghafi.

Kila mmoja akifikia tarehe yake ya mwisho kuuza nguvu kazi ghafi, mara moja aanze kujikita katika kubadili nguvu ya akiri na hisia kuwa bidhaa na huduma zenye kuwa suruhisho la kudumu kwa matatizo na changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wengine.

Kwakuwa utazalisha bidhaa na huduma zenye kuwa na manufaa makubwa kwa watu wengine, basi na wao watakupatia zawadi ambayo ni pesa, ili kujipatia kila kilicho bora kutoka kwako. Tukiweza kufanikisha azima hii, basi tutatajirika kutokana na ukweli kwamba watu wengi kwasasa wanataka bidhaa na huduma ambazo ni suruhisho ya changamoto zao. 

Wateja ni wengi ambao wako tayari kununua kila kitu kitakachozalishwa ilimradi kina thamani kwao, kwa hiyo soko ni kubwa. Nchi yetu inapokaribia kuingia uchumi wa kati, mahitaji ya bidhaa na huduma zitokanazo na nguvu ya akiri/fikra zitazidi kuongezeka. 

Bidhaa zenyewe ni kama vile muziki, sanaa, vitabu, program za mafunzo ya ujasiriamali/biashara/afya/kilimo/majengo pamoja na machapisho juu miongozo mbalimbali ya uwekezaji katika mambo ya utalii, uwindaji, gasi, mafuta, madini, kilimo n.k.


Uchumi wa watanzania ukizidi kuongezeka na idadi ya wasomi ambao ndio wahitaji wakubwa itazidi kuongezeka huko tuendako ~ Kwa hiyo ewe mtanzania mwenzangu, anza kuchukua hatua leo, wakati ni sasa.

MAMBO 6 YATAKOYO KUSAIDIA KUANZA KUJITEGEMEA


Uchunguzi unaonesha kuwa kila mtu anapenda kujitegemea, lakini wengi wanashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya kukosa kitu wanachokiamini, nacho ni kutokuwa na uwezo wa kufanya hivyo!

“Napenda sana kujitegemea lakini sina uwezo,” wengi hutamka hivyo unapowauliza kwa nini wanazeekea kwenye maisha ya utegemezi. Sababu ya kukosa uwezo imewafanya baadhi ya watu kuwa tayari kupokea kila aina ya manyanyaso na mwisho wa yote wanajipoza kwa kulia.

Swali la kujiuliza: Ni nani aliyezaliwa anajitegemea? Jibu ni hakuna, hapa ndipo penye msingi wa mada hii ambayo naamini kupitia vipengele vifuatavyo msomaji wangu utajifunza jinsi ya kuanza maisha ya kujitegemea.

1. Mtazamo
Kikwazo cha kwanza kinachowafanya watu waishi maisha ya utegemezi ni mtazamo. Wengi wanaamini wana haki ya kulelewa na wazazi/ndugu, lakini wanashindwa kujiuliza wataishi katika utegemezi mpaka lini na wanaowategemea wakifariki dunia wataishije?

Kazi ya kwanza katika kuyaelekea maisha ya kujitegemea ni kubadili mtazamo wa maisha tegemezi na kuona umuhimu wa kujitegemea. Maana yangu hapa ni kuyachukia maisha ya kumtegemea mtu na kutamani maisha ya kujitegemea ambayo ni huru na yenye raha.

2. Kujitegemea ndani ya utegemezi
Baada ya kubadilisha mtazamo, mhusika ni lazima aanze maisha ya kujitegemea ndani ya utegemezi. Msingi wa kipengele hiki ni huu; kuna baadhi ya watu wanabweteka mno na kutaka wafanyiwe kila kitu na walezi wao ambapo hata andazi la shilingi 100 wanataka wanunuliwe! Kisingingizio ni kilekile, kwamba hawana uwezo ingawa fedha kama shilingi mia mbili wanazipata.

Kujifunza kujitegemea lazima kuanzie ndani ya maisha ya kutegemea, mfano kama jukumu la baba ni kununua mboga na wewe umebahatika kupata kiasi cha fedha kwa njia yoyote hata ya kupewa, usizifiche, badala yake lichukue jukumu la baba na kulifanya wewe. Tabia hii inajenga msingi wa uwajibikaji ambao ndiyo nguzo ya maisha ya kujitegemea.

Chukia maisha ya kufanyiwa kila kitu, jihangaishe kwa kazi ya aina yoyote, jiwekee utaratibu wa kuhudumia familia yako, weka msingi wa kuheshimu fedha, usiendekeze tabia ya kupata fedha na kuacha kufanya jambo la maana nyumbani kisa unamtegemea mtu atakununulia hiki na kile na kuzifanya fedha zako ziwe za kutapanya ovyo. Ukijizoesha hivyo hutaweza kujitegemea.

3. Kujiamini

Vikwazo au shaka juu ya kuweza kumudu maisha ya kujitegemea vimewafanya wengi wasijiamini. “Kwa kipato hiki nitaweza kweli kuendesha maisha yangu, nilipe kodi ya nyumba, chakula, mavazi na mahitaji mengine?” Maswali ya aina hii mara nyingi yamekuwa na majibu ya haitawezekana!

Tabia ya akili hasa katika kufikiria mambo yajayo ni kujenga hofu ambayo wakati mwingine haihitajiki; wenye kujiamini pekee ndiyo ambao hutupilia mbali hofu na kujiamini ndiyo walioofanikiwa katika maisha yao.

Kwa msingi huo, unapofikiria maisha ya kujitegemea usiwaze sana juu ya kuwezekana kwa mambo, jiamini kuwa utaweza, ukifanya hivyo utaweza; siku zote mwenye shaka havuki mto!

4. Kuchukua hatua
Hatua nyingine muhimu baada ya kupita vipengele nilivyoanisha hapo juu ni hiki cha kuchukua hatua. Watu wengi wamekuwa wakipanga kujitegeme, lakini kila mwaka wanaahirisha kufanya hivyo. “Nafikiri nitahama mwaka ujao.” Mwaka ukifika anapanga kufanya hivyo mwaka unaofuata matokeo yake anazeeka akiwa kwenye maisha tegemezi.

Ushauri wetu kama timheaven, baada ya kujiamini kuwa unaweza chukua hatua ya kutoka mahali ulipo, jambo kubwa la kuzingatia hapa ni kuhakikisha kuwa uchukuaji hatua lazima uambatane na ushauri mzuri kutoka kwa ndugu na jamaa na hasa wale uliokuwa unaishi nao kama wanakuunga mkono katika suala hilo.

5. Kutorudi nyuma
Uchunguzi unaonesha kuwa wapo watu ambao hupitia hatua zote za kuelekea kujitegemea, lakini wanapozikabili changamoto za maisha hayo huamua kurudi mahali wapokuwa wanaishi jambo ambalo huwaongezea fedheha na mara nyingine  kuwaathiri kisaikolojia.

Unapokuwa umeanza maisha ya kujitegemea suala la kurudi ulipotoka lisiwe la kawaida. Kumbuka unapokuwa na wazo la “nikishindwa narudi kwa baba,” huwezi kujituma, hutapambana na changamoto za maisha binafsi kwa vile kinga yako haitakuwa kwako bali kule ulikotoka, kushindwa itakuwa ni sehemu yako.

6. Ongeza marafiki
Unapokuwa kwenye maisha ya kujitegemea hakikisha kuwa unajitahidi kupunguza maadui. Fanya kila linalowezekana kuongeza marafiki ambao siku zote ndiyo nguzo muhimu nyakati za shida. Kumbuka kazi ya rafiki ni kufariji na adui kuangamiza

VIJANA 30 MATAJIRI ZAIDI DUNIANI 2017


1. Tajiri mmiliki wa ardhi ambaye pia amekuwa akisaidia wasiojiweza katika jamii, Mtawala wa Westminister Gerald Cavendish Grosvenor amefariki na kumwachia mwanawe Hugh Grosvenor urithi wa £9bn.

Alikuwa na binti watatu, na mwana mmoja pekee wa kiume, Hugh, mwenye umri wa miaka 25.

Hugh amerithi "nusu ya London" kwani ardhi nyingi maeneo mengi ya Belgravia na Mayfair, London ilimilikiwa na babake.

Yeye hufanya kazi katika kampuni ya Bio-bean, kampuni inayoangazia teknolojia isiyoongeza gesi zinazochangia ongezeko la joto duniani.

Kwa mujibu wa orodha ya jarida la Forbes ya mwaka 2016, kuna vijana wengine tisa wa chini ya umri wa miaka 30 ambao utajiri wao ni zaidi ya dola bilioni moja za Marekani.

Vijana wengine matajiri ni:

2 & 3: Alexandra, 20, na Katharina Andresen, 21

Ndio wachanga zaidi na wanamiliki kampuni ya Ferd.
Binti hawa walirithi utajiri hu kutoka kwa baba yao Johan, raia wa Norway mwaka 2007.

4: Gustav Magnar Witzoe, 23
Anatoka Norway pia na huonesha maisha yake ya kifahari kwenye Instagram.

Amerithi sehemu ya biashara ya babake ya kufuga samaki na sasa utajiri wake ni $1.1bn (£846m).

Gustav Witzoe, babake ambaye wana jina sawa, alimpa hisa kwenye kampuni hiyo kama zawadi. Lakini hana udhibiti au usemi wowote.

5 & 6: Ludwig Theodor Braun na dadake

Haonekani sana mtandaoni. Hayupo kwenye Twitter au Instagram lakini anatambuliwa kwa utajiri.

Familia yake ilianzisha kampuni ya dawa ya B. Braun Melsungen, Ujerumani 1839.

Kampuni hiyo ni maarufu sana kwa dawa na vifaa vya matibabu.
Ludwig humiliki 10% ya kampuni hiyo ambayo ni sawa na $1.8bn (£1.4bn).

Dadake Eva Maria Braun-Luedicke yuko nyuma yake kidogo lakini utajiri wake ni $1.4bn (£1bn).

7 & 8: Waanzilishi wa Snapchat

Evan Spiegel ni mmoja wa walioanzisha mtandao wa Snapchat ambao hutumiwa na mamilioni ya vijana duniani.
Majuzi, aliingia uchumba na mwanamitindo mashuhuri duniani Miranda Kerr.

Ana umri wa miaka 26 na utajiri wake ni $2.1bn (£1.6bn), Evan ndiye mchanga zaidi miongoni mwa waanzilishi wa Snapchat na ndiye tajiri zaidi miongoni mwao.

Mwenzake ni Bobby Murphy, 28, ambaye anamkaribia sana kwa utajiri.

Utajiri wa Murphy ni $1.8bn (£1.3bn).

9: Lukas Walton
Kwa mujibu wa Forbes, Lukas Walton, 29, ndiye anayemkaribia sana Hugh Grosvenor.

Utajiri wake ni $10.4bn, ambazo ni karibu £7.2bn kwa viwango vya sasa vya ubadilishanaji wa fedha vya sasa.

Anatoka katika familia tajiri inayomiliki Walmart (miongoni mwa kampuni nyingine), ambayo pia humiliki Asda nchini Uingereza.

10: Wang Han
Wang Han, raia wa China, anakamilisha orodha hii.
Chanzo cha utajiri wake ni urithi wa hisa za kampuni ya ndege ya Juneyao Air kutoka kwa babake Wang Junyao, aliyefariki 2004.

Junyao alikuwa mwanzilishi wa kampuni ya Juneyao Group. Wang Han humiliki 27% ya hisa za shirika hilo la ndege na 14% ya hisa za maduka ya jumla ya Wuxi Commercial Mansion Grand Orient.
Utajiri wake unakadiriwa na Forbes kuwa $1.34bn.

MBINU 10 ZA KUWAFANYA WATEJA WAENDELEE KUFANYA BIASHARA NA WEWE



Kazi kubwa sana unayohitaji kufanya baada ya kumpata mteja ni kuhakikisha anaendelea kuwa wako, yaani anaendelea kufanya biashara na wewe.

Wafanyabiashara wengi wamekuwa wakitumia nguvu kubwa kuwafikisha wateja kwenye biashara zao, lakini wateja wanapofika na kupata huduma huondoka na wengi kutokurudi tena.

Ni rahisi sana kumuuzia mteja ambaye ulishamuuzia awali, kuliko kumuuzia mteja mpya. Hivyo kama ukiweza kuiendesha biashara yako vizuri, wateja ambao wananunua kwako watakuwa wateja wako wa kudumu.

NAPENDA BIASHARA

Zifuatazo ni mbinu kumi unazotakiwa kuanza kuzitumia leo kwenye biashara yako ili kuhakikisha wateja wako wanaendelea kufanya biashara na wewe.

1. Tekeleza ulichoahidi.
Kama umemtangazia mteja kwamba akija kwenye biashara yako atapata kitu fulani, basi hakikisha anapata kitu hiko. Hakuna kitu ambacho watu hawapendi kama kudanganywa. Mteja anapoona kwamba amedanganywa hatorudi tena kwenye biashara yako na utakuwa umemkosa milele. Hakikisha unatimiza ulichomwahidi mteja wako.

2. Ahidi kikubwa na pitiliza(overpromise and overdeliver)
Najua hapa unaweza usielewe kwa sababu ulichozoea ni kuahidi kidogo na kupitiliza(underpromise and overdeliver). Hii ilikuwa unafanya kazi zamani, ila kwa sasa, haifanyi kazi tena. Kwa sababu kama wewe unaahidi kidogo, wenzako wanaahidi kikubwa na wanafanyia kazi. Hivyo kitu pekee cha kuhakikisha unawabakisha wateja ni kuwaahidi makubwa na kuyapitiliza hayo. Kama umejitoa kweli kwenye biashara yako, hili halitakushinda.

3. Imarisha mawasiliano yako na wateja wako.

Ni muhimu sana uwe na mawasiliano na wateja wako. Bila ya kujali ni biashara gani unafanya, kuna na mfumo w akupata namba za simu, au barua pepe za wateja wako. Mata kwa mara watumie ujumbe ukiwatakia heri na wakati mwingine kuwajulisha bidhaa au huduma mpya zilizopo kwenye biashara yako.

4. Fanyia kazi malalamiko ya wateja haraka.
Wateja wanapokuwa na malalamiko, yafanyie kazi haraka sana. Usisubiri mpaka yawe makubwa kiasi cha kuwafanya watafute mahali pengine wanakoweza kufanya biashara bila ya matatizo wanayopata kwako.

5. Toa huduma bora ambazo mteja hawezi kupata popote.
Huduma kwa wateja, mteja amepokelewaje, ameelezwaje kuhusiana na bidhaa au huduma anayohitaji, maswali yake yamejibiwaje, hivi ni vitu vinavyoonekana vidogo sana ila vina maana kubwa sana kwa wateja wa biashara yako. hakikisha wateja wako wanapata huduma ambazo zitawafanya wajisikie ufahari.

6. Wakumbuke wateja waliopotea.
Kama biashara yako imekuwepo kwa muda, kuna wateja waliokuwepo awali ila kwa sasa hawapo tena. Kuna wateja ulikuwa unafanya nao biashara zamani, ila kwa sasa huwaoni tena kwenye biashara yako. ni vyema kuwatafuta na kujua kwa sasa biashara wanafanya na nani na ni kitu gani limewafanya hawaji tena kwako.

7. Muuzie mteja baada ya kumuuzia.
Mara nyingi mteja atakuja kwako akitaka kitu fulani, lakini pia anaweza kuwa anataka vingine zaidi ya alichofuata hapo. Ni jukumu lako kujua mahitaji haya yote ya mteja wako na kuyafanyia kazi. Usiishie kumuuzia mteja kitu kimoja pekee, hakikisha kila anachohitaji ambacho kipo kwenye biashara yako, unampatia. Ataendelea kuja kwako kwa sababu anajua mahitaji yake yote anayapata kwako.

8. Pima thamani ya mteja ya muda mrefu.
Kuna wateja ambao wananunua mara moja na kuondoka na kuna wateja ambao wataendelea kununua kwako kwa muda mrefu. Wateja wanaonunua mara moja na kuondoka unaweza kupata faida kubwa, lakini ndio imeishia hapo. Wateja ambao wananunua muda mrefu unaweza kupata faida ndogo, ila utaendelea kuipata kwa muda mrefu. Jua wateja wale wa muda mrefu na endelea kuwapatia thamani nzuri.

9. Tumia mtandao wa intaneti na mitandao ya kijamii kuwa karibu na wateja wako.

Mtandao umerahisisha sana mfanyabiashara kuwa karibu na wateja. Hakikisha biashara yako ipo kwenye mtandao kwa kuwa na tovuti, kuwa na blogu na kuwa na kurasa kwenye mitandao ya kijamii. Utatumia mitandao hii kutoa taarifa muhimu kuhusiana na biashara yako.

10. Toa zawadi na motisha kwa wateja.
Kuwa na njia ambapo utatoa zawadi mbalimbali kwa wateja wanaorudi tena kwenye biashara yako. inaweza kuwa kuwapatia kuponi za punguzo kadiri wanavyonunua mara nyingi, au kutoa punguzo la bei kama mteja ananunua mara nyingi. Vyovyote vile hakikisha mteja anapata motisha pale anaponunua kwako kwa muda mrefu.

Anza kufanyia kazi mambo hayo kumi ili kuboresha uhusiano wako na wateja wako na uweze kukuza biashara yako.

HISTORIA FUPI YA FREEMASON



Ni shirika ambalo mambo yake ni siri kuu. Mimi nilifanya utafiki kwenye mitandao, nikafatilia historia yao kama inavyoonyeshwa mara kwa mara kwenye makala za historia katika televisheni za magharibi pamoja na kuongea na watu waliofuatilia kwa karibu mambo yao.
Kwenye maelezo yao kwa nje Free masons wanajitangaza kama shirika zuri tu.

Naomba niorodheshe mambo machache niliyoambiwa kuhusiana na Freemasonry.
1. Ni kweli Freemasonry kama ilivyo maana yake kwanza ilkuwa ni kundi la mafundi waashi (masons) au wajenzi kuwa lugha nyingine. Walikuwa ni wataalamu waliobobea kwenye masuala ya ujenzi wa mahekalu na mabenki ya zama hizo zinazoitwa kwa kizungu (medieval times).

Niliambiwa walikuwa ni watunzaji wa pesa za kanisa katoliki. Kwani walikuwa wanajenga mahekalu(cathedrals) za wakatoliki na mabenki/ mahandaki ya kuhifadhia pesa pamoja na kuzikia(catacombs).

Niliambiwa wanaweza kujenga hayo maandaki kwa utaalamu mkubwa kiasi kwamba ukiingia ndani ya hayo mahandaki bila ramani unaweza ukashindwa kutoka hata unaweza kupotelea humo humo ndani usiweze kutoka tena. Hicho ndicho kilichokuwa ni kiwango cha utaalamu wao.

2. Kwa kuwa walikuwa ni waashi ndiyo maana alama zao ni vifaa vya ujenzi, Pima maji n.k

3. Inasemekana mji mkuu wa marekani (Washington DC) ulisanifiwa na kujengwa na Freemasons. Na inasemekana ni mji makini ambao umejengwa ukizingatia pembe tatu zenye nyuzi zinazowakilisha u freemason.

4. Ikatokea kipindi ambapo hawa freemasons wakaasi kwa kuanza kujishirikisha na mambo ya nguvu za giza. Wengine wanasema walianza kuiba pesa za kanisa katoliki, lakini ukweli halisi haujulikani. Kutokana na sababu hizi na zinginezo ambazo ni siri kati ya kanisa katoliki na freemasons, Freemasons wakafukuzwa kutoka ukatoliki.

Ndio maana hakuna maelewano kati ya freemasons na wakatoliki. Wakatoliki wakaanzisha shirika jingine badala ya hao freemasons lijulikanalo kama Jesuits.

Jesuit Fathers ni mapadri wa katoliki wa daraja la juu sana wenye elimu ya juu zaidi ambao hufanya kazi za siri za utawala na udhibiti ndani ya kanisa katoliki.

5. Kuhusu imani yao (freemasons) nikaelezwa kwa kifupi kuwa wanaamini Yesu na Lucifer ni mtu na ndugu yake. wanaamini kuwa Lucifer ndiye mwema na mzuri lakini wanaamini kuwa Yesu ndiye mwenye mabaya. alimfanyia hila Lucifer aonekane mbaya.

6. Kinachoendelea ndani yake kuhusiana na ibada zake ni siri kwani kuna daraja ambazo muumini wa freemason anapanda kutokana na kubobea katika imani ikiwa ni pamoja na kutunza siri zao. Ninajua kuwa daraja ya juu kabisa ni nyuzi ya 33 (33rd degree)

7. Ni watu wenye nguvu mno na mambo yao ni makubwa mno na siri zao ni nzito mno. Ndiyo maana haziko wazi.

Wafuasi wa kiwango cha chini wala hawajui shirika hili linahusika na nini manake hata wao hawaambiwi kitu. Kwa wafuasi wa daraja ya chini wanakwenda ku socialize tu. Yaani kwa wasio jua kitu kule kwenye lodge zao ni kama ywca au wmca au club hivi. Kwenye nchi kama marekani watu wasio jua siri wanachukulia kama sehemu za kusocialize tu.

8. Freemasonry inawekwa pamoja na makundi mengine makubwa ya siri, yanayoendesha ulimwengu mzima kwa nguvu za kiuchumi, siasa na mambo ya utawala.

FANYA MAMBO HAYA, KUTENGENEZA MAISHA YA MAFANIKIO UNAYOTAKA



Kama Unabomoa Misingi Hi, Hutaweza Kufanikiwa Tena


Tumia kile ulichonacho kwa uhakika na vizuri kabisa. Acha kujidanganya kwamba unataka mafanikio makubwa wakati hata ile misingi ya kutengeneza mafanikio makubwa unaiharibu hovyo hovyo.

Haiwezekani eti unasema unataka mafanikio makubwa wakati unatumia muda, pesa na nguvu zako hovyo, ambapo vitu hivyo kwa pamoja vingekusaidia kufikia mafanikio makubwa kama ungevitumia vizuri na kwa busara.

Hata Pesa unazozipata hazijiamulii zenyewe kwamba ‘sasa mimi pesa ninakwenda kununua kitu hiki au kile.’ Wewe ndiye mwenye jukumu la kupanga pesa zako zitumike wapi na kwa sababu ipi.
Soma; Tabia Tatu (3)  Muhimu Unazotakiwa Kuziendeleza, Ili Kufanikiwa.

Sasa kama hiyo iko hivyo, kwa nini unafanya maamuzi mabovu ambayo yanakupotezea pesa nyingi na kwa kiasi kikubwa? Kuwa makini sana na matendo yako ili yasikupotezee pesa ambayo ni moja rasilimali muhimu kukusaidia kufanikiwa.

Hapo ulipo najua una pesa za kiasi fulani hata kama ni ndogo, najua una muda na nguvu fulani, sasa kwa nini hivi vitu usivitumie kwa uangalifu ili viweze kukusaidia kukupa mafanikio makubwa na badala ya kuvipoteza tu kiholela.

Watu matajiri, wanajua namna ya kutunza pesa zao vizuri, kwa nini wewe usiwe miongoni mwao? Huna pesa za kutosha si kwa sababu pesa zinakukimbia bali ni kutokana na matendo yako yanayofukuza pesa.

Kitu cha kufanya jiulize, ni hatua zipi utaweza kuzichukua ili kuweza kulinda hata zile rasilimali zako za kukusaidia kufanikiwa ambazo ni pesa, muda na nguvu zako. Kama hujui tafuta watu wenye mafanikio kisha wafatilie na ujue nini cha kufanya.

Lakini kitu ambacho nataka uelewe hapa jifunze sana kutumia kile kidogo ulichonacho kikusaidie kufanikiwa. Najua unaelewa wapo watu ambao wanadharau sana hasa ikiwa wanacho kile kidogo.
Watu hawa mara nyingi hawajui thamani ya kutumia kile kidogo walichonacho. Iwe ni pesa kidogo watazitumia hovyo mpaka zitakwisha. Iwe ni muda kidogo pia watautumia hovyo hata bila kupata faida ya muda huo.

Kwa kuwa wewe umeshalijua hili leo, amua kutumia kiasi kidogo cha pesa ulichonacho kwa busara ili kikusaidie kutengeneza pesa nyingi. Pia amua kutumia muda, nguvu zako au chochote ulichonacho ambacho unaona ni kidogo kikusaidie kufanikiwa.

Hata Musa wakati anawaongoza wana wa Israeli kuvuka bahari ya shamu, alitumia fimbo aliyonayo kupiga bahari na ikagawanyika, hapo ndipo wana wa Israeli wakaokolewa.

Leo hii ni kipi ambacho huna. Najua una kidogo ulichonacho ila hujaona sana kama kinaweza kukusaidia. Sasa hebu anza leo kukiangalia kwa jicho la tofauti ili kikusaidie kujenga mafanikio makubwa.

Kabla sijaweka kalamu yangu chini pengine nikwambie hivi, kama unabomoa misingi hii ya kushindwa kutumia kile angalau kidogo ulichonacho kwa busara na vizuri…kufanikiwa kwako itabaki kuwa hadithi.

Hiyo iko hivyo kwa sababu, mafanikio yanajengwa na vitu vidogo vidogo sana ambavyo mwanzo huonekana si kitu wala si chochote, lakini vitu hivyo ndivyo hatimaye vinavyofanya mafanikio yakaonekana kwa nje.

Sasa wewe ni nani hadi ufanikiwe wakati unajiona kabisa unavunja sheria za asili za mafanikio? Huwezi kufanikiwa. Ila kikubwa utakachofanya ni kujidanganya tu kwamba ipo siku lazima nitafanikiwa.

Mpaka hapo ulipo jiulize je, hicho ulichonacho unakitumia kwa vizuri ili kikusaidie kupata kingine kikubwa? Lakini ikiwa unataka kufika katika ngazi fulani ya mafanikio, huku hapo ulipo hujiwekei misingi imara hutaweza kufika huko.


Kila wakati jitathimi katika kila eneo unalotaka kufika kwa kujiuliza je, kile kidogo ulichonacho unakitumia ili kukusaidie kufanikiwa? Ukiweza kupangilia vizuri matumizi ya kidogo ulichonacho na kuhakikishia UTAFANIKIWA.

KUTENGENEZA MAISHA BORA


Inawezekana una ndoto au mipango ya kuishi maisha ya namna fulani ambayo unayoyataka. Je, kitu cha kujiuliza, ulishawahi kujua utawezaje kushi maisha hayo unayoyataka?

Je, ni mikakati ipi ambayo umeweka hadi uweze kufikia hatua ya kuweza kutengeneza maisha unayoyataka? Kwa kawaida bila hata kuumiza kichwa, yapo mambo ya kuzingatia ili yakusaidie kuishi maisha unayoyataka.

Haya ni mambo ya msingi sana ambayo ukizingatia yatakusaidia uweze kutengeneza maisha bora unayohitaji. Unajiuliza ki-vipi, hapa nikiwa na maana maisha ya ndoto zako, ikiwa lakini utachukua hatua.

Ni mambo gani ambayo unatakiwa kufanya ili kutengeneza maisha ya mafanikio unayoyataka? Hebu fuatana nami katika makala haya ili tuweze kujifunza kwa pamoja.

1. Tambua kitu unachokitaka.
Ikiwa haujui kile unachotaka vizuri kwenye maisha yako, usije ukashangaa ukaendelea kuwa mtu wa kutokuwa na mafanikio karibu kila siku. Kabla hujapata kitu chochote kwenye haya maisha lazima uje ni kipi unataka.

Watu wengi wanakwama sana kwenye maisha kwa sababu ya kutokujua vizuri wanachotaka. Chukua muda wako kidogo ulionao na kisha kitambue kile unachokitaka kwenye maisha yako.

2. Tengeneza mfumo wa kufikia hicho unachokitaka.
Kwa kuwa umeshakijua hicho unachokitaka katika maisha yako, sasa hapa unatakiwa kutengeneza mfumo wa kuhakikisha unakikamilisha kitu hicho. Unatengenezaje huo mfumo? Ni kwa kufanya kila siku.

Acha kusimamishwa na kitu chochote. Weka nguvu za uzingativu na fanya kila siku mpaka malengo yako yatimie. Ikiwa utafanya kila siku, uwe na uhakika baada ya muda utafikia kile unachokitaka.

3. Weka juhudi sana.              
Wakati unapokuwa umejiwekea mikakati ya kufika kule unakotaka kufika kuna njia rahisi tu kujikita unashindwa kufanikisha adhima hiyo ikiwa huataweka juhudu sana.

Unatakiwa uweke juhudi kuhakikisha mpaka unafanikiwa. Hakuna kulala katika hilo jitahidi sana ufanye kila linawezekana mpaka kuona kila kitu kinakaa sawa.

4. Weka nguvu za uzingativu kwa hicho unachokifanya.
Usijiruhusu ukawa mtu wa tamaa, wakati upo kwenye harakati za kutengeneza maisha unayoyataka wewe. Kati ya kitu kinachowaangusha watu ni pamoja  na tamaa ya kutaka kufanya mambo mengi kwa pamoja.

Ni muhimu nguvu zako ukaziweka sehemu moja. Hata ikitokea jambo zuri vipi, kipindi ambacho unatengeneza maisha unayoyataka, ukishaweka nguvu ya uzingativu usilifanye jambo hilo. Kitu cha msingi ujifunze kutulia ili kufikia mafanikio yako.

5. Jifunze kila siku juu ya kitu hicho.
Njia ya kufikia mafanikio mara nyingi ni njia ambayo haijanyooka kabisa kama baadhi wanavyofikiri. Zipo changamoto nyingi zinazojitokeza. Kila zinapotokea changamoto hizo amua kujifunza na kujirekebisha kwa kufanya upya kila siku

Pale unapokutana na changamoto za aina yoyote ile hutakiwi kukata tamaa na kutaka kurudi nyuma. Kitu cha muhimu ni kujifunza na kufanya hadi uone umeweza kufikia lengo la kuishi maisha unayotaka.

Unatakiwa uamua kujifunza juu ya kitu ambacho umeamua kukifanya mpaka uwe mtaalamu kabisa tena uliyebobea. Kwa hali, hiyo itakusaidia sana kuweza kuishi maisha unayoyataka.

Mwisho, mtu kuishi maisha anayoyata sio ajali wala bahati. Unaweza ukaishi maisha unayoyataka ikiwa utatengeneza mfumo huo na kuzingatia mambo haya muhimu kama tulivyoyaangalia kwenye makala haya.

MAMBO 6 YATAKAYO KUFANYA UKOSE HESHIMA KWENYE JAMII YAKO


Hakuna kitu kibaya maishani kama kuonekana upo katika daraja la chini na mtu wa kudharaulika kwenye jamii unayoishi. Kisaikolojia kuna madhara makubwa.

Ni imani yangu kuwa kila mwanadamu timamu anapenda kuheshimiwa lakini wengi wetu tunashindwa kupata heshima tunayoitaka kwa sababu hatufahamu jinsi ya kuishi mbele ya wenzetu.

Kitaalamu, hakuna jambo ambalo hutokea maishani bila sababu maalumu hivyo hata kudharauliwa kwako au kwetu ndani ya jamii tunayoishi kunatokana na jinsi tunavyoenenda.

Njia za kukusaidia kurejesha heshima yako kwa kuperuzi na wewe baadhi ya dokezo muhimu zinazoweza kukusaidia kujitambua na kuweza kuyaepuka maisha ya kudharauliwa.

1. Muonekano.

Kwanza kabisa ni jinsi unavyoonekana. Muonekano ninaouzungumzia hapa ni usafi wa mavazi na mwili kwa ujumla. Hata siku moja hakuna mchafu anayeheshimika katika jamii anayoishi hata kama ana kipaji kikubwa kiasi gani.

Kwa hiyo uchafu wa mavazi na mwili huchangia mtu kudharauliwa katika jamii anayoishi.

Linaweza kuwa jambo dogo sana lakini ni moja kati ya sababu kubwa inayochangia kuporomoka kwa thamani yako mbele ya wenzako.

2. Mazungumzo.

Hapa naomba nieleweke kuwa unachokizungumza kinaweza kukujengea heshima au kukubomolea heshima. Kauli zisizo na busara zitakufanya udharaulike kwa kila mtu. Uropokaji usiokuwa na mantiki huchangia kuporomosha heshima yako hasa kama utakuwa muongeaji zaidi. Biblia inasema penye wingi wa maneno hapakosi uovu.

3. Utendaji wako wa Kazi.
Ndugu zangu, siku zote heshima ya mtu ni kazi. Watu wengi hawapendi kufanya kazi kwa bidii huku wengine wakijiendekeza kwa tabia ya kuombaomba, jambo hilo halifai kwa vile huchangia kubomoa heshima yako mbele ya jamii. Fanya kazi usiishi bila kujishughulisha.

4. Kutotimiza ahadi.
Kama una tabia za kuahidi mambo halafu unashindwa kuyatekeleza, basi unajiweka katika nafasi mbaya ya kutunza heshima yako katika jamii unayoishi. Bora ukwepe kutoa ahadi kuliko kuahidi na kutotimiza.

5. Sifa zisizo na maana.
Nakumbuka msemo mmoja kutoka kwa mwandishi mwandamizi aliyekuwa mtaalamu wa falsafa za maisha, marehemu Adolf Balingilaki, ambao unasema kwamba: “Ukitafuta heshima kwa gharama ya juu, basi utalipwa dharau kwa bei nafuu.”

Msemo huu unamaanisha nini? Siku zote ukiwa unafanya mambo yako kwa ajili ya kusifiwa au mazungumzo yako kuwa ya kujiinua, watu watakudharau.

6. Kutokuwa mwaminifu.

Suala la uaminifu ni pana, kuna uaminifu wa fedha, siri, dhamana na mambo kama hayo, hivyo ni vema kila unachoaminiwa lazima ukitunze kwani ukiwa mtu wa kuvunja uaminifu fahamu kuwa utashusha heshima yako

HAYA NDIO MAKABILA 125 YA TANZANIA


Hii ni orodha ya makabila ya watu ambao wamekuwa wanaishi tangu zamani katika eneo ambalo sasa linaitwa Tanzania, pamoja na makabila yaliyogawiwa na mipaka baina ya Tanzania na nchi za jirani.

1.        Waalagwa (pia wanaitwa Wasi)
2.        Waakiek
3.        Waarusha
4.        Waassa
5.        Wabarabaig (pia wanaitwa Wamang'ati)
6.        Wabembe
7.        Wabena
8.        Wabende
9.        Wabondei
10.   Wabungu (au Wawungu)
11.   Waburunge
12.   Wachagga
13.   Wadatoga
14.   Wadhaiso
15.   Wadigo
16.   Wadoe
17.   Wafipa
18.   Wagogo
19.   Wagorowa (pia wanaitwa Wafiome)
20.   Wagweno
21.   Waha
22.   Wahadzabe (pia wanaitwa Wahadza na Watindiga)
23.   Wahangaza
24.   Wahaya
25.   Wahehe
26.   Waikizu
27.   Waikoma
28.   Wairaqw (pia wanaitwa Wambulu)
29.   Waisanzu
30.   Wajiji
31.   Wajita
32.   Wakabwa
33.   Wakaguru
34.   Wakahe
35.   Wakami
36.   Wakara (pia wanaitwa Waregi)
37.   Wakerewe
38.   Wakimbu
39.   Wakinga
40.   Wakisankasa
41.   Wakisi
42.   Wakonongo
43.   Wakuria
44.   Wakutu
45.   Wakw'adza
46.   Wakwavi
47.   Wakwaya
48.   Wakwere (pia wanaitwa Wanghwele)
49.   Wakwifa
50.   Walambya
51.   Waluguru
52.   Waluo
53.   Wamaasai
54.   Wamachinga
55.   Wamagoma
56.   Wamakonde
57.   Wamakua (au Wamakhuwa)
58.   Wamakwe (pia wanaitwa Wamaraba)
59.   Wamalila
60.   Wamambwe
61.   Wamanda
62.   Wamatengo
63.   Wamatumbi
64.   Wamaviha
65.   Wambugwe
66.   Wambunga
67.   Wamosiro
68.   Wampoto
69.   Wamwanga
70.   Wamwera
71.   Wandali
72.   Wandamba
73.   Wandendeule
74.   Wandengereko
75.   Wandonde
76.   Wangasa
77.   Wangindo
78.   Wangoni
79.   Wangulu
80.   Wangurimi (au Wangoreme)
81.   Wanilamba (au Wanyiramba)
82.   Wanindi
83.   Wanyakyusa
84.   Wanyambo
85.   Wanyamwanga
86.   Wanyamwezi
87.   Wanyanyembe
88.   Wanyaturu (pia wanaitwa Warimi)
89.   Wanyiha
90.   Wapangwa
91.   Wapare (pia wanaitwa Wasu)
92.   Wapimbwe
93.   Wapogolo
94.   Warangi (au Walangi)
95.   Warufiji
96.   Warungi
97.   Warungu (au Walungu)
98.   Warungwa
99.   Warwa
100.             Wasafwa
101.             Wasagara
102.             Wasandawe
103.             Wasangu (Tanzania)
104.             Wasegeju
105.             Washambaa
106.             Washubi
107.             Wasizaki
108.             Wasuba
109.             Wasukuma
110.             Wasumbwa
111.             Waswahili
112.             Watemi (pia wanaitwa Wasonjo)
113.             Watongwe
114.             Watumbuka
115.             Wavidunda
116.             Wavinza
117.             Wawanda
118.             Wawanji
119.             Waware (inaaminika lugha yao imekufa)
120.             Wayao
121.             Wazanaki
122.             Wazaramo
123.             Wazigula
124.             Wazinza
125.             Wazyoba