Alhamisi, 29 Novemba 2012

BOB MARLEY MHUBIRI WA AMANI NA UPENDO BILA YESU




Mcheza mpira wa miguu, Mhubiri wa amani na upendo, Mwanamapinduzi, Mwanaharakati, Mpiganaji, Mwanasiasa, Mwanamuziki wa Reggae na Nyota ya kwanza katika ulimwengu wa tatu Bob Marley.


Alizaliwa akiitwa Robert Nesta Marley na mama wa Kijamaica mwenye asili ya Afrika, bi Cedella Booker na baba mwanajeshi Mwingereza aliyefariki kijana Robert akiwa bado mdogo sana akiwaacha katika umasikini mkubwa.



Bob Marley alizaliwa panapo usiku wa kuamkia Februari 6, 1945, St Anns Parish kijiji cha Nine Miles (maili tisa) huko Jamaica.

Kumbukumbu zake za utotoni na ujanani zimejaa harakati za maisha na muziki. Harakati zilizomkutanisha na kijana machachari Peter Tosh na pia Bunny Livingstone (Wailer) na hatimaye vijana wengine kama Junior Braithwaite na Beverly Kelso. Panapo mwaka 1963, Bob akiwa na wenzake waliojiita Wailing Wailers waliweza kusaini mkataba na prodyuza maarufu wakati huo Coxsone Dodd na kutoa vibao kadhaa kikiwemo 'Simmer Down' kilichowatambulisha vema katika ulimwengu wa muziki wa Jamaica.



Bob na Rita Anderson walioana mwaka 1966 baada ya Bob kurejea Jamaica akitokea Marekani ambako alikacha kwenda vitani Vietnam. Aliporudi Jamaica, Bob alikuta imani ya Kirastafari ikiwa imepamba moto kufuatia ziara ya Mfalme wa Ethiopia Haile Sellassie (Ras Tafarr Makonen) hapo mwaka 1965. Hotuba ya Sellassie ndicho kibao cha Bob kiitwacho 'War'

Kundi la Wailing Wailers halikudumu sana. Lilivunjika mwaka 1974 na Bob kuunda kundi lake maarufu zaidi katika historia ya muziki wa reggae la 'Bob Marley and the Wailers' wakafanikiwa kutoa albamu ya 'Catch A Fire' panapo mwaka 1975 ikiwa na kibao maarufu kilichopatwa kuimbwa tena na wanamuziki wengi sana cha 'No Woman No Cry'



Mwaka 1976, Bob Marley alifanikiwa kuwapatanisha mahasimu wakubwa wa kisiasa nchini Jamaica, waziri mkuu na kiongozi mkuu wa upinzani, Michael Manley na Edward Seaga. Wajamaica walimwona Bob Marley kama shujaa halisi wa taifa lao. Bob na kundi lake walishambuliwa na risasi siku tatu kabla ya tukio hilo, lakini walipona.

Mwaka huohuo wa 1976, Bob Marley na kundi lake walitoa albamu ya 'Exodus' iliyovunja rekond ya mauzo na kukaa kwenye chati ya Billboard kwa majuma 52 ikikamata namba moja.



Bob Marley alizunguka mabara yote ya ulimwengu kupiga muziki wake uliokubalika sana. Maonesho makubwa zaidi aliyafanya Uingereza, Ujerumani, New Zealand, St. Barbara, California huku pia akishiriki kama mgeni mwalikwa muhimu katika sherehe ya uhuru wa Zimbabwe mwaka 1980.

Maradhi ya kansa iliyoanzia kidoleni mguuni kwake, yaliukatisha uhai wake panapo Mei 11, 1981 huko Miami Marekani akiwa angali kijana wa umri wa miaka 36. Katika kibao chake cha 'Rastaman Chant' alipata kusema, "One bright morning when my work is over, I'll fly away to Zion"
Hata hivyo aliiacha kazi yake kama mhubiri wa amani na upendo.

Serikali ya Jamaica, kwa kuutambua mchango wake, ilimtunukia nishani ya juu zaidi 'Order of Merit.'

Bob Marley aliacha watoto 12, wengi wao wanajihusisha na muziki wa reggae na hip hop.

Bob Marley atakumbukwa zaidi duniani kama balozi na shujaa halisi wa muziki wa reggae. Atakumbukwa kwa kuuweka muziki huu wenye nguvu katika ramani ya ulimwengu.



Muziki wake utaendelea kuishi vizazi na vizazi. Ni urithi muhimu sana kwa wanaoupenda muziki wake. Ama kwa hakika wanajivunia sana miaka 36 ya uhai wake.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi daima. Amina.

MKASA WA MELI YA TITANIC

Pichani, meli ya RMS Titanic ikiondoka Southampton Uingereza hapo Aprili 10, 1912


kwa meli ya Titanic kulitokana na tatizo la usukani


LONDON – Meli ya Titanic iligonga siwa barafu (iceberg) tarehe 14 Aprili 1912 mnamo saa 5.40 usiku kutokana na hitilafu ya usukani.  Lakini ikazama kwa kasi zaidi kutokana na Afisa mwandamizi wa meli hiyo kumwamuru nahodha aendelee na safari.  Hayo yameelezwa jana Jumatano na mwandishi wa Kiingereza alipohojiwa na shirika la habari la Reuters.


Louise Patten, mwandishi na mjukuu wa Afisa mwandamizi wa meli hiyo Charles Lightoller, ameamua kusema ukweli juu ya kile kilichotokea karibia miaka 100 iliyopita.  Ukweli huo ulikuwa umefichwa kwa makusudi kwa kiasi cha miaka 100 ili kulinda heshima ya babu yake aliyekuja kuwa shujaa wa vita kuu ya dunia.

Lightoller, afisa mkuu aliyesalimika katika ajali ile ya kihistoria aliuficha ukweli huo alipohojiwa mara mbili.  Alihofu kuwa ukweli huo ungeifilisi kampuni iliyoitengeneza meli hiyo na pia kuwapotezesha ajira wenzake walioajiriwa katika kampuni hiyo.


"Wangeweza kuikwepa barafu ile kama isingekuwa kasoro kwenye usukani," Patten ameiambia Daily Telegraph.


Mabaki ya meli ya Titanic kama yanvyoonekana katika picha hii iliyopigwa hivi karibuni.

"Badala ya kuuelekeza usukani wa Titanic kwa usalama kuelekea kushoto kwa siwa barafu lile, iligundulika kuwa usukani haufanyi kazi upande huo.  Aliyeushika usukani, nahodha  Robert Hitchins, alichanganyikiwa na kuuelekeza upande usio sahihi."


Patten, ameyafunua hayo ili kwenda sambamba na utowaji wa riwaya yake mpya "Good as Gold" ambayo ameitumia kuelezea mazungumzo ya manahodha hao.  Kwa mujibu wa mazungumzo hayo, kulikuwa na mifumo miwili tofauti ya usukani.

Jambo lililokuwa la muhimu sana, mfumo mmoja  ulikusudiwa kuuzungusha usukani kuelekea upande mmoja, na mfumo mwingine, kinyume chake.

Kosa hilo la usukani lilipofanyika,  Patten akaongeza, "walikuwa na dakika 4 tu za kuubadili mfumo huo.  Wakati afisa mkuu William Murdoch alipoligundua kosa la Hitchin na kujaribu kulirekebisha, alikuwa amechelewa."

Babu yake Patten hakuwa akiangalia wakati meli ikigonga siwa barafu, lakini alikuwepo wakati wa kikao cha mwisho cha maafisa wa meli ya Titanic kabla ya meli hiyo kuzama kabisa.


Babu yake Patten si tu alisikia juu ya makosa hayo, bali pia amri kutoka kwa J. Bruce Ismay, mwenyekiti wa White Star Line, kampuni iliyoitengeneza meli hiyo akimwamuru nahodha wa meli kuendelea na safari.  Tendo la kuendelea na safari lilisababisha meli kuzama kwa kasi kubwa sana.  Masaa saba tu hadi kufikia saa 2.20 asubuhi, meli ilikuwa imezama yote.

"Kama Titanic ingesimamishwa pale pale, isingezama kamwe kwani ingeweza kumudu kusubiri meli za uokoaji na pasingekuwepo vifo vile.," alisema Patten.

Meli ya RMS Titanic ilikuwa ndiyo meli kubwa zaidi duniani wakati ikiondoka Southampton, Uingereza, kuelekea New York katika safari yake ya kifahari zaidi melini panapo Aprili 10, 1912. Siku nne baadaye ikiwa safarini iligonga siwa barafu na kuzama.  Ajali hiyo kubwa zaidi ya meli katika historia, iligharimu maisha ya watu 1517 kati ya watu 2227 waliokuwa ndani ya meli hiyo ikijumlisha abiria na wafanyakazi.


Nimeiandika habari hii baada ya kuisoma kwenye mtandao wa Reuters kwa sababu moja.  Nimetaka tuone tofauti ya wenzetu wa Ulaya.  Miaka 100 sasa, wao bado wanajali juu ya chanzo cha ajali.  Sisi meli ya Mv Bukoba iliyozama miaka 14 tu nyuma, nani anajali tena kujua chanzo kilikuwa nini?  Wenzetu na rekodi nzuri ya watu waliokuwemo.  Sisi wala hatujawahi kuwa na idadi kamili ya wahanga

Hebu litazame hili jedwali juu ya rekodi za abiria wa Titanic.  Sisi hadi leo hatuna idadi kamili ya wahanga wa majanga makubwa.  

category
waliokuwa melini
waliopona
asilimia waliopona
waliokufa
asilimia waliokufa
1st class
329
199
60.5 % 
130
39.5 % 
2nd class
285
119
41.8 % 
166
58.2 %
3rd class
710
174
24.5 % 
536
75.5 %
crew
899
214
23.8 % 
685
76.2 %
Jumla
2,223 
706 
31.8 %
1,517
68.2 %

Chanzo jedwali:  wikipedia



 FA

JOSE CHAMELEONE BILIONEA ALIYEJARIBU WOKOVU



ninaweza kusema hivyo kwa sababu ilishawahi kutangazwa sana katika vyombo vya habari kwamba gwiji wa nyimbo za duniani mganda Jose chameleone ameokoka. hii ilikuwa ni baada ya kupata maradhi ya kuweweseka katika usingizi na hatimaye kujitupa chini kutoka katika ghorofa ya pili katika hotel aliyokuwa amepanga mjini Arusha. Baada ya tukio hilo bingwa huyu akatangaza kuja kwa Yesu. Lakini hakuendelea zaidi na sijui siri ya moyoni mwake,lakini Biblia inatufundisha kumtambua mtu aliye na Yesu,naamini bado muda upo na nafasi bado iko na Bwana anatamani amtumie wakati huu na sio wakati akiwa amechoka au amekuwa dhaifu kiafya. Najua unajiuliza kwa nini ninamwita Bilionea!




Ndiyo, kwa asiyeamini, hebu angalau baadhi ya mambo yanayothibitisha utajiri wa nyota huyo. 
Anamiliki jumba la kifahari katika vilima vya Sekuku jijini Kampala, pia ana nyumba huko Arizona, Marekani, achilia ile ya Kigali, Rwanda aliyoinunua hivi karibuni kwa mamilioni ya shilingi. 



Ukiachilia mbali gari la kisasa aina ya Cadillac Escalade lililomgharimu zaidi ya Sh milioni 100, Chameleone ambaye ni baba wa watoto watu, pia anamiliki Mercedes Benz, BMW na aina nyingine za magari. 
Kwa ujumla, anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia Sh bilioni 1.5 kwa fedha za Tanzania. Na anasema bado anazisaka, kwani bila ya kuwa na tamaa ya kusaka mafanikio zaidi, ndoto huenda zisitimie. 



Anayasema hayo akisisitiza kuwa, baada ya nyumba, magari na akaunti nono benki, sasa ana ndoto za kumiliki helikopta yake, baada ya kuwa amekuwa akikodi mara kadhaa ama kwenda katika matamasha au kama alivyofanya wakati anamuoa mkewe Daniela Atim.
pia ana jumba lipo karibia na ufukwe wa ziwa victoria kwa upande wa uganda,pia ana apartments kibao huko uganda,hilo cardillac ni zaidi ya million 250 za kitanzania,Ukija kina Bobby winne na Bebe Cool wanamiliki hadi meli na Hummer hizi wanazotembelea kina 50 cent.anakumbuka akiwa na Bebe Cool na Redsun alipata fursa ya kutumbiza katika shindano la kumsaka mrembo wa Kenya. Anakiri hapo ndipo milango ya neema ilipoanza kufunguka. anasema Dorotea ,baada ya kuzoeana alimshawishi ahamie nyumbani kwake badala ya kuendelea kulala studio,ushawishi ambao ulimchukua zaidi ya wiki moja kumkubalia.




 “Nilipohamia tulikuwa marafiki, lakini mengine yaliibuka tukiwa katika nyumba moja. Mara nyingi kila akitoka, alinikuta nimetulia naandika nyimbo, huku akihoji ni lini nitarekodi. Nilikosa jibu kwa kuwa siku wa na fedha. 

Siku moja akiwa safarini huko Afrika Magharibi aliniachia bahasha yenye dola za Kimarekani 1,000 (karibu Sh milioni 1.8 za Tanzania kwa sasa), akaniambia niingie studio ana. 


“Huo ukawa mwanzo wa kibao Mama Mia na sikuamini kama fedha ile ingebadilisha maisha yangu na kunifikisha hapa nilipo. Mengine yanabaki kuwa historia,” anasema. 

Pamoja na utajiri aliovuna kupitia muziki, nyota huyo anasema historia ya kushuhudiwa `Live’ na watu zaidi ya bilioni 9 akitumbuiza wakati wa Kombe la Dunia kwake ni kitu cha kipekee. 

“Mtoto wa Afrika tena Afrika Mashariki kupewa heshima ile haikuwa kitu kidogo. Najiona mwenye bahati na ni mastaa wachache wanaweza kuingia katika kundi la bahati hata wangeishi kwa miaka 1000.” 

Anasema kutokana na baraka alizopata maishani, ameamua kuanzisha taasisi ya Chameleone ili aweze kuwasaidia wasiojiweza. 

“Nikiwa mdogo sikuwa na maisha mazuri, sikutoka katika familia bora, kwa hiyo ninajiona mwenye wajibu wa kuwasaidia wengine wakianzia katika misingi mizuri ya kielimu. “Nimeshanunua eneo kwa ajili ya kujenga kituo. 

Nataka jamii siku moja inikumbuke kwamba niliwika na kuitangaza nchi yangu, lakini pia sikuwa mchoyo, bali niliyatumia vyema matunda ya muziki. 


Kwa kufanya hivi, naamini ipo siku nitawashawishi wengi kufanya mambo makubwa kwa ajili ya jamii wanayotoka.” 

Huyo ndiye Joseph Mayanja ambaye pamoja na misukosuko ya maisha tangu akiwa shule hadi sasa akiwa staa, bado nyota yake inang’ara. 


Je, atazidi kupata mafanikio? Bila shaka ni jambo la kusubiri na kuona, hasa ikizingatiwa kuwa, mwenyewe amejijengea falsafa ya kutolewa sifa, bali kazi kwa kwenda mbele. 

Pamoja na yote, Chameleone anapaswa mfano wa kuigwa kwa wasanii wengi wa Kitanzania ambao huvuma kwa muda mfupi, lakini 

wakishazikamata fedha hupotelea kwenye ulimwengu wa anasa na baadaye kujikuta wakiwa `choka mbaya’, tena wakiwa hawana akiba benki wala hawajawekeza.


Chanzo: kutoka katika mitandao mbalimbali