Ijumaa, 1 Agosti 2014

MAPAMBANO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO SEHEMU YA TATU




 

Watu wasiomjua Mungu unajimu unaweza kuwasaidia kujua wakati unaofaa wa kushiriki katika utendaji fulani au kuanza kufanya mambo fulani.


Inasemekana kwamba habari hizi zinaweza kujulikana kwa kutazama mpangilio wa nyota au sayari fulani na kuchunguza uhusiano kati ya nyota na sayari hizo, na pia uhusiano wake na dunia.


Inasemekana kuwa uvutano wa nyota na sayari juu ya maisha ya mtu binafsi unategemea mpangilio wake wakati wa kuzaliwa kwa mtu huyo.


Wanajimu wa kale walifikiri kuwa dunia ndiyo kitovu cha ulimwengu, na kwamba sayari na nyota zilikuwa zimefungiwa katika miviringo ya kimbingu ambayo iliizunguka dunia.


Lakini pia walifikiri kwamba jua linasafiri angani likiwa kati ya makundi ya nyota likifuata njia fulani hususa katika mzunguko wa kila mwaka.


Waliigawanya njia hii ya jua ya kila mwaka katika sehemu au maeneo 12. Sehemu hizo zote zilikuwa na makundi ya nyota, na kila sehemu ilipewa jina kulingana na kundi la nyota ambamo jua lilipitia.


Sehemu hizo zikawa zile ishara 12 za nyota na kuitwa “nyumba za mbinguni,” kwa sababu zilionwa kuwa makao ya miungu ya kipagani. Hata hivyo, wanasayansi waligundua baadaye kuwa jua haliizunguki dunia bali dunia ndiyo inayozunguka jua.


Uvumbuzi huo mpya ulithibitisha kuwa unajimu si sayansi yenye kutegemeka bali ni uchawi sawa na kupiga ramri.


Bado hata sasa  katika nchi nyingi duniani watu hawatoki majumbani kwao bila kujua nyota yake inasemaje kuhusu siku hiyo, kwa hiyo ni lazima wapate magazeti yenye kurasa maalumu za watabiri wa nyota.


UNAJIMU HAUWEZI KUFUNUA SIRI ZA MUNGU


Wakati wa utawala wa Mfalme Nebukadneza wa Babiloni, makuhani na wanajimu walishindwa kufasiri ndoto ya mfalme. Danieli, nabii wa Mungu wa kweli, alionyesha sababu zilizofanya washindwe kufasiri ndoto hiyo aliposema:


“Siri ambayo mfalme anauliza, watu wenye hekima, wala wafanya-mazingaombwe, wala makuhani wenye kufanya uchawi wala wanajimu hawawezi kumwonyesha mfalme. Hata hivyo, kuna Mungu mbinguni ambaye Ni Mfunuaji WA siri, naye amemjulisha Mfalme Nebukadneza mambo yatakayotokea katika siku za mwisho.” (Danieli 2:27, 28)


Danieli alimtumaini Mungu ambaye ni “Mfunuaji wa siri” bali si katika jua, mwezi, au nyota, na akamweleza mfalme maana ya kweli ya ndoto yake.


Danieli 2:36-45. Kwa maana nyingine ni kwamba Mamlaka ya Mungu katika ulimwengu wa roho ilikwisha kaa kikao na  kuamua juu ya hatma ya ufalme wa Nebukadneza, kwa hiyo Nebukadneza hata angejitahidi kupambana wakati anguko lake linatokea angekuwa anapigana katika damu na nyama.


Hapo ndipo mtume Paulo anakataa kwamba hatutakiwi kupigana katika damu na nyama, kwa kufanya hivyo ni sawa na kutapatapa kwa sababu, watu wameshamaliza katika ulimwengu wa roho.


Baada ya kujua machache kuhusu ulimwengu wa roho naamini utakuwa umepata ufahamu kidogo utakaokusaidia kwenda sambamba na somo hili. Mtume Paulo bado anaendelea na kutuingiza katika chumba cha silaha na kutushauri katika mstari wa kwamba;


SOMO LITAENDELEA


Tunaweza kuwasiliana


Furaha Amon Mob: 0713 461593