Jumamosi, 26 Julai 2014

NAMNA YA KUISIKIA SAUTI YA MUNGU YA NDANI KWA URAHISI ZAIDI SEHEMU YA TATU





Mungu huzugumza na watu wake,kwa njia mblimbali kama vile ndoto, maono,sauti ya dhahiri masikioni, au sauti ya ndani kama mawazo ambayo tunajifunza n.k. vyovyote itakavyokuwa lakini Mungu huhakikisha kuwa anaongea na watu wake.
Njia ya Mungu kuongea na mtu mmoja inaweza ikatofautiana na mwingine lakini Mungu anahakikisha ameongea na watu wake.
Wakristo wengi husikia sauti ya Mungu kutokana na uzoefu wa kuishi na Mungu, lakini kwa kupewa mafundisho inakuwa ni nadra sana.
Hii inawafanya wakristo hata wanaposikia sauti ya Mungu wanakuwa na mashaka mashaka kuitekeleza. Hivyo wanaisikia kwa kubahatisha. Hawajui kanuni kamili ya jinsi kuisikia sauti ya Mungu.
Biblia inasema;
“Basi imani, chanzo chake ni kusikia: na kusikia huja kwa neno la Kristo” (Warumi 10:17).
Kwa kigriki maandiko yanaitwa grapha. Hii ni andiko la aina yoyote ile, liwe na maana au lisiwe na maana. Wagiriki wakatofautisha maandiko ya kawaida na maandiko ya neon la Mungu.
Maandiko ya neno la Mungu wakaita Logos. Logos ni neno la Mungu ambalo tayari lipo tumepewa kama vile Biblia na vitabu mbalimbali vya neno la Mungu vinavyoandikwa  na watumishi wa Mungu mbalimbali.
Wagiriki wakaona neno la Mungu ni pan asana. Hivyo wakaona watofautishe Logos na neno la Mungu linguine wakaita Rhema. Rhema ni neno la Mungu ambalo Mungu anazungumza na mtu moja kwa moja saa hiyo (live).
Unaweza ukawa unasoma  andiko katika Biblia msitari fulani,ukawa unaendelea kusoma kila siku. Huo msitari utaendelea kuwa Logos lakini siku moja unaweza ukausoma mstari huo na Mungu akazungumza na wewe moja kwa moja kupitia mstari huo akakupa ujumbe fulani. Siku hiyo huo mstari utakuwa Rhema.
Rhema ni sauti ya Mungu au ni neno la Mungu analozungumza na mtu moja kwa moja. Inaweza kuwa wazo fulani,hata kama Mungu atazungumza na wewe kwa njia nyingine ya ndoto,maono, nk.
Baada ya maelezo hayo, hebu turudi kwenye andiko letu Basi imani, chanzo chake ni kusikia: na kusikia huja kwa neno la Kristo (Warumi 10:17). Sasa tujiulize swali je tusikie neno lipi kati ya Logos na Rhema ambalo ukilisikia litazaa imani?.
Neno ambalo ukilisikia huzaa imani ni Rhema siyo Logos, Logos haizai imani. Hii ndio maana watu wengi wanasoma Biblia lakini haijawasaidia wala kuwafanya waokoke.
Wakristo wengi wameshindwa kuwa na imani ya kutenda miujiza kwa sababu hawajui kanuni hii ya miujiza kutendeka. Kwa maana hiyo tumeona ili uwe na imani yenye kutenda miujiza ni lazima usikie Rhema (usikie kutoka kwa Mungu anakuagiza kutenda jambo).
Hakuna mtu wa Mungu yeyote ambaye Mungu hazugumzi naye, tatizo ni uhakika wa kujua kuwa hii ndiyo sauti ya Mungu, kwa sababu neno la Mungu linasema kondoo wanaijua sauti ya mchungaji wao.
Mungu huongea na watu wake na kuwongoza na kuwaelekeza nini wafanye. Lakini wakristo huwa hawatii hiyo sauti ya Mungu. Kwa hiyo Mungu huamua kutoendelea kuongea nao tena.
Unapokuwa mtii Kwa sauti ya Mungu ndipo Mungu anakuwa anazungumza na wewe na baadae unaizowea sauti na inakuwa dhahiri kabisa kwako bila mashaka mashaka. Mkristo ambaye sio mwombaji wa kuomba maombi marefu sauti ya Mungu itampa shida kidogo kuitambua.
Mungu anazo njia nyingi za kuongea na watu wake, anaweza kuongea kwa ndoto, maono,sauti ya masikioni na sauti ya ndani kama wazo, nk. Hata kama Mungu amezungumza na wewe kwa njia kati ya hizo, hiyo ndio rehma.
Wakristo wengi wanafikiri kuwa ktika agano la kale, manabii huenda Mungu alikuwa na njia maalumu sana ya kuongea nao tofauti na sisi. Hao watu walikuwa kama sisi,waliishi hapahapa,walikula chakula hikihiki n,k. hawakutofautiana na sisi. Mungu alizungumza nao kwa njia hii hii ambayo ndiyo anazungumza na sisi leo,hakuna tofauti.
Kwa hiyo ndugu yangu usipoweza kumtii Mungu katika mambo ya kila siku ya kawaida na hata katika mambo madogomadogo, Mungu hawezi kuendelea kuongea na wewe, Mungu anaposema tuishi kwa imani yaani maana yake tuishi kwa kumsikiliza yeye.
Biblia inasema,
Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani: naye akisita sita Roho yangu haina furaha naye” (Waebrania 10:38).
Tumeona kuwa, imani chanzo chake ni kusikia. Sasa andiko hili linasema Ataishi kwa imani. Maana yake ni kwamba, ataishi kwa kusikia kutoka kwa Mungu (kwa sababu imani chanzo chake ni kusikia).
Kuishi ni nini?
Kuishi ni kule kuwa hai kila sekunde inayopita. Uhai ukisimama sekunde moja mtu atakufa. Hivyo kila sekunde,dakika,saa,siku,wiki,mwaka, unapokuwa bado uko hai huko ndiko kuishi.
Mungu anataka uishi kwa kumsikiliza yeye. Mungu anataka yeye ndiye akuongoze akuagize nini cha kufanya kila sekunde katika maisha yako ya kimwili na kiroho.
Wakristo wengi wanajiendea tu na kujifanyia mambo yao wenyewe bila ya kuongozwa na Mungu. Hii imekuwa hivi kwa sababu hawajui nini maana ya kuishi kwa imani.
Kuishi kwa imani wanafikiri ni kuishi maisha ya shida, kubahatisha kupata riziki, maisha ya kubangaiza yasiyokuwa na uhakika. Kuishi kwa imani ni kuishi maisha ya kumsikiliza Mungu anakuagiza kufanya nini.
Wakristo wengi wanaishi kwa kujionoa wenyewe,ndio maana wamejaa shida,dhiki na kukosa mafanikio. Wengi wanafanya mambo ambayo Mungu haja waagiza na wengi wapo mahali ambapo Mungu hajawaagiza kuwa pale. Wanafanya na wapo pale kwa mapenzi yao wenyewe si kwa mapenzi ya Mungu.
Watumishi wa Mungu wengi wana wito lakini wanafanya wito ambao hawakuitiwa. Ni sawa wameitwa kumtumikia Mungu, lakini je ni Mitume, nabii, mwinjilisti, mchungaji au mwalimu na je kituo au mji walipo ndipo Mungu anataka wawepo? Shida ni kwamba wengi hawajui kuisikia sauti ya Mungu
Sauti ya Mungu inapokuja kwako inakuwa ina mambo mawili. Ni kama kifurushi chenye vitu viwili ndan yake  ambayo ni maagizo ya kufanya na nguvu ya Mungu ya kuyatekeleza maagizo hayo. Hivyo ukitenda uliyoagizwa na Mungu unafanikiwa.
Ukitenda maagizo ya shetani kunatokea uharibifu. Hakikisha unatenda maagizo ya Mungu na pia hakikisha uko mahali ambapo Mungu amekuagiza uwe.
Sisemi uache kufanya lolot sababu Mungu hajazungumza na wewe, wewe endelea kufanya mambo kama kawaida yako,hata kama Mungu hajazungumza na wewe, na wakati huouo ukimsikiliza Mungu, endapo Mungu atasema na wewe basi fanya lile aliloguagiza.
SAUTI YA MUNGU KATIKA KUTENDA MIUJIZA.
Hakuna mtu yeyote anayeweza kutenda muujiza kwa maamuzi yake mwenyewe, hata kama ni mtumishi wa Mungu anayetumiwa kwa kiwango cha juu sana. Miujiza yote inayotendwa, Mungu huzungumza na watakaotenda huzungumza nao kwa njia ya Rhema.
Katika kitabu cha waebrania sura ya kumi na moja yote inazungumzia watumishi wa Mungu waliotenda miujiza mukubwa enzi za agano la kale,wakristo wamezowea kuwaita watu hao mashujaa wa imani. Mambo hayo hawakuamua yatendeke kwa mawazo yao wenyewe, bali Mungu aliwaagiza kuitenda miujiza hiyo.
Tofautisha mawazo yako na imani. Mawazo yako hayawezi kutenda miujiza hata siku moja. Bali kama  Mungu akikuagiza kutenda kwa kutumia sauti ya ndani. Wakristo wengi hawalijui jambo hili,hivyo wanapokuwa wanapenda jambo fulani litendeke hufikiri imani itakuja kutokana na kutamani kwao.
Baada ya hapo mawazo hayo huamua kuyakiri kwamba yamekuwepo. Baada ya hapo wanayangojea yatokee wakisema wanayangoja kwa imani huku wakisema kuwa maana imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo.
Kwa maana hiyo hata wao wako katika kuyatarajia. Pia wanaendelea kusema kuwa imani ni bayana na mambo yasiyoonekana, hivyo wanayatamani yatokee
MUNGU AKUBARIKI TUKUTANE KATIKA SEHEMU YA TATU
Mob: Furaha Amon 0713 461593.