Ijumaa, 21 Septemba 2012

WEKA UFAHAMU WAKO HURU


WEKA UFAHAMU WAKO HURU.

Mungu wetu ametuumba kwa namna ya kipekee kabisa na anatujua vizuri sana hata kwa majina yetu,na zaidi ya hayo ametupangia kila kitu katika maisha yetu. Kabla hajatuumba alikuwa ameshaandaa kila kitu katika maisha yetu. Lakini mipango mingi ya Mungu inashindwa kutimia katika maisha yetu kutokana na mawazo tuliyonayo yanavyoweza kuathiri na kuzuwia mapenzi Mungu juu ya mafanikio yako. Ni muhimu kujua jinsi ufahamu wa mwanadamu unavyofanya kai na jinsi ambavyo unaweza kuutawala na aina ya mawazo unayopaswa kuyawaza ukiwa kama kiumbe muhimu kwa Mungu. Zipo athari zinazopatikana kutokana na kuwaza vibaya. Kuna magonjwa na kutokufanikiwa kunakoandamana na sababu za kuwaza vibaya. Ni muhimu kujifunza namna ya kuukomboa na kuuweka huru ufahamu wako ili uwe unawaza yale yaliyo na umuhimu tu. Utabadirika katika maisha yako kutokana na jinsi utakavyobadilika katika kuwaza kwako kwa kuwa “Ajionavyo (awazazvyo) mtu nafsini (akilini) mwake ndivyo alivyo.”


UFAHAMU NI NINI?
Mwili wa binadamu hujiendesha kwa sehemu kubwa kwa kutumia akili (MIND) yake yaani ufahamu. Sehemu hii muhimu sana kwa binadamu inaratibu utendaji wa mwili na viungo vyote vya mwili kuanzia kichwani mpaka unyayoni. Huratibu kiasi cha damu kinachotakiwa kichwani na katika mwili mzima. Huratibu pia usagaji wa chakula muda wa kupumzika yaani kila kitu katika mwili wa binadamu. Katika ulimwengu wa sasa wenye shinikizo na mahangaiko mengi ya maisha wandamu wamekuwa wakiishi katika wakati mgumu sana. Watu wamekuwa wakisongwa na mawazo ya kila aina na mengi yakiwa ni mawazo hasi (negative). Mawazo hasi ni mawazo yasiyokuwa na uvumbuzi ni kuwaza shida, matatizo pamoja na masumbufu yanayomzunguka mtu. Kwa kutumia mawazo yetu adui anatuongoza katika kukata tama, kutojiamini na kutomwamini Mungu. Kuanzia mwanadamu alipoanguka katika bustani ya Eden uwanja wa vita kati ya Mungu na shetani kwa binadamu upo katika ufahamu (akili) MIND ya binadamu. Kwenye ufahamu huko ndiko ambako shetani hupigana vita na sisi binadamu. Iwapo atafanikiwa kukamata ufahamu wako sawasawa, basi itakuwa ni vigumu sana kwako kufanikiwa. Utakosa uhuru wa kuamua au kufuata mapenzi ya Mungu na mwishowe kuishia kwa waganga wa kienyeji. Lakini ukiweza kumwondoa na kufanikiwa kumshinda shetani katika ufahamu wako wewe utakuwa huru.

AKILI NI NINI?
Neno akili ukilitafiri kutoka katika neno la kiingereza MIND ambalo maana yke ni Nia,dhamiri,akili,ufahamu, kumbukumbu. Akili ni eneo muhimu sana ndani ya mwanadamu ambalo linaratibu shughuli zake zote ndani na nje ya mwili wa mwanadamu. Ubongo ni kama kompyuta kubwa ambayo inahifadhi vitu vingi na muhimu lakini akili ni zaidi ya ubongo. Baadhi ya kazi za akili ni kama zifuatazo. (1) kukumbuka (2)kuelewa(3) utashi (kufanya maamuzi) (4) uendeshaji wa mwili n.k. vilevile akili huwa inafanya kazi pamoja na uelewa na mazoea. Kuhisi vitu na kusafirisha kumbukumbu. Kuamini (kuhukumu) kutokana na tukio lililotangulia na la sasa. 

UMAKINI KATIKA MAAMUZI. 
akili si ubongo na wala akili haionekani wala haushikiki bali akili ipo na kila mtu anayo na anaitumia kwa viwango tofauti. Akili hutunza kumbukumbu za matukio yote kuanzia alitungwa mimba mpaka hapo ulipo. Japokuwa si rahisi kukumbuka matukio yaliyotokea wakati akiwa mtoto mchanga. Lakini bado yapo ndani mwako na yana athari ndani mwako. AKILI HUFANYA KAZI KWA KUAMINI NI LAZIMA UAMINI ILI JAMBO LITOKEE.(Mathayo 17:20) kwa mstari huu tunaona kuwa Yesu ametutaka tuamini,ndivyo tulivyoumbwa. Sisi tunaishi kwa imani ndio maana akili huamini hata kile inachopokea katika masomo au mafundisho mbalimbali. Vilevile Mungu ametujalia wanadamu uwezo wa hali ya juu wa kutumia akili kama chombo cha mafunuo katika hali isiyokuwa ya kimwili mfano maono ndoto n.k. watu wengine wamejaliwa kuota ndoto na baadae tukio linatokea kweli. Au anahisi kuwa kuna mgeni anakuja nyumbani na  baada ya muda mgeni huyo anatokea kweli. Hii ni kuonyesha kuwa ufahamu wa mtu huyo ulijua kuwa huyo atakuja kabla ya kumuona. Wakati mwingine unaweza kuimba wimbo fulani,mara hiyohiyo ukausikia wimbo huo kwenye radio unaanza kuimbwa.
 
JINSI AKILI INAVYOENDESHA YETU.
Kama tulivyojifunza kwamba akili hurtibu utendaji mzima wa mwili kama kusafirisha damu.kuamuru kutengenezwa kwa chembechembe zinazohitajika kwa wakati. Kuamua misuli ya kusaga chakula au mikono na miguu au aina yoyote ya misuli ya mwili ifanye kazi. Shughuli hizi hufanyika kwa namna mbili (a) ukiwa una uelewa yaani ukiwa na fahamu.(b) ukiwa hauna uelewa yaani umelala au umezimia. Mfano unaweza kukunja mkono wako na vidole mpaka kuwa mfano wa ngumi,kitendo ambacho unaweza kukifanya ukiamua. Lakini huwezi kula chakula na ukaamua kuwa sasa chakula hiki kisagwe, huwezi kuamua kupunguza kiasi cha damu inayoelekea mkono wa kulia na kuilekeza mkono wa kushoto au mguuni. 

HIVYO NDIO KUSEMA KUWA KUNA UTENDAJI MKUBWA SANA NA MUHIMU AMBAO HUFANYIKA NDANI MWETU BILA YA SISI WENYEWE KUJUA kazi mojawapo ya akili ambayo ambayo ningependa tujifunze sana ni hii ya kutunza kumbukumbu na mawasiliano. Eneo hilo ndilo lililo na umuhimu wa kipekee katika maisha yetu yajayo na linaloendesha mfumo mzima wa maisha yetu kiroho zaidi na kimwili.
SEHEMU KUBWA TATU ZA AKILI
SEHEMU YA KWANZA (Conscious Mind) sehemu hii huhusika na kufikiria na kuweka kumbukumbu za muda mfupi pamoja na kutambua vitu. Hutumia milango mitano ya fahamu kutambua na kuvipambanua vitu. Huwa inafanya kazi wakati mtu anapokuwa macho au hajalala,akiwa anajitambua.sehemu hii huwa haitunzi kumbukumbu bali huwa inazipokea na kuzipeleka sehemu ya pili. Eneo hili pia unaweza ukaliita sehemu ya nje ya akili au uelewa. Matukio yote unayoyafanya kwa kuelewa,kujitambua yanaratibiwa tayari kwa kukumbukwa mfano,sura ya mtu,rangi mbalimbali,mitaa,barabara n.k. eneo hili ndilo linalopambanua kila kitu,ndilo linaloratibu shughuli na utashi wa mtu wa kila siku kwa mfano avae nini,ale nini n.k. matukio maneno au mawazo yanapojirudiarudia na haswa maneno ya kujisemea mfano mimi nina shida,nateseka Napata taabu, nina amani,ninaweza nina akili ninaweza jambo. Mawazo ya aina hii yanapojirudiarudia ndani ya sehemu hii ya awali, akili huamini na inapoamini hupeleka imani katika sehemu ya pili kuhifadhiwa tayari wakati wa baadae.kwa kutumia sehemu hii mtu hutambua na kuelewa vitu vinavyotokea kwa kupitia ya fahamu mtu hupata kuelwa kwa kupitia sehemu hii. Tunaweza kuiita utashi au moyo,hutoa maamuzi madogo madogo ya mtu na huwa haihifadhi kumbukumbu ya muda mrefu. Hutambua vitu vya kawaida na vilivyozoeleka kuwepo hujishughulisha pia na mambo ya kila siku kama uchaguzi wa nguo,chakla maamuzi n.k.(mazuri na mabay ya kila siku hufanywa hapa.vilevile hufnya kazi ya kufikiri na wakati mwingine huwa na mjadala wa ndani ya mtu. Utakuwa unawaza na kujiuliza maswali na kupata majibu ya maswali unayojiuliza. Mjadala au mabishano ya mwanzo ambayo wakati mwingine inakuwa ni shida kupata majibu au suluhisho lake yanaanzia sehemu hii. Japokuwa mara nyingine suluhisho linapatikana lakini kwa uzoefu mawazo yanayodumu kwa muda mrefu hayapati suluhisho zuri katika eneo hili. Mawazo na majadiliano hayo yanayochukua muda mrefu yanapelekwa kuhifadhiwa katika sehemu ya pili (Sub conscious) kwa ajili ya kufanyiwa kazi baadae. Sehemu hii hufanya kazi mtu anapokuwa na ufahamu (akiwa macho) sehemu kubwa huacha kufanya kazi wakati mtu anapolala au anapokuwa amezimia. Mawazo yote huwa yanaanzia hapa yawe mazuri au mabaya mawazo haya huwa hayatokei hivihivi tu bali huwa chini ya mamlaka ya mtu mwenyewe. Mtu anao uamuzi wa kuwaz au kutokuwaza mawazo haya pia huwa yantokana na mazoea ya mtu mwenyewe. Mtu kama amezowea kuwaza mawazo uovu,mabaya,shida,taabu,hasi basi kila wakati atawaza hayo tu. Mawazo yenyewe huja kama vile yanajiendesha yenyewe (automatic) lakini kumbe sivyo. Vilevile kuna mtu amezowea kuwaza mema,mazuri,furaha,amani,mafanikio nayo vilevile huja yenyewe (automatic) na kila wakati alivyojizoesha. Baada ya kufanya kazi kutwa nzima na kupata vitu mbalimbali huyahifadhi yote hayo kwenye eneo la pili la akili ambayo ni Sub conscious) kwa ajili ya kufanyiwa kazi baadae. Sehemu hii hufanya kazi mtu anapokuwa na ufahamu yaani akiwa macho sehemu kubwa huacha kufanya kazi wakati mtu anapolala au anapokuwa amezimia. Mawazo yote huwa yanaanzia hapa yawe mazuri au mabaya.

SEHEMU YA PILI YA AKILI (Subconscious mind)
Hii ni sehemu katika akili ya mwanadamu iliyopo bila kujulikana kwa mwenye kuwa nayo. Ni sehemu ambayo inawea kumtawala mwanadamu japokuwa mwanadamu haioni wala kuitambua. Eneo hili ndilo hufanya kazi kubwa sana kwa binadamu kama vile kuhifadhi kumbukumbu zote na kuzileta baadae kuzifanya ziwe dhahiri. Mawazo yote awazayo mtu kwa muda mrefu,maneno ambayo mtu huyasema mara kwa mara huhifadhiwa hapa na baadae kuwa dhahiri, au hufanya mtu huyo awe kama jinsi anavyowaza. Huendesha viungo vyote vya mwili mfano hutawala mapigo ya moyo,mzunguko wa damu. Kiasi cha damu kinachotakiwa sehemu mbalimbali. Huendesha usagaji wa chakula,na kijamii viwango vya kemikali vinavyohitajika katika kusaga chakula au katika damu. Kwa kifupi sehemu hii ndio ndio iendeshayo mzima wa binadamu. Eneo hili hupokea kila kitu kinachotoka katika sehemu ile ya kwanza bila kujali kitu hicho ni cha kweli au cha uongo,kizuri au kibaya huyapokea na kuyafanyia kazi,yaani huyafanya yawe dhahiri angalia (Mithali 10:24) huhifadhi kila kitu kinachopelekwa huko na kukifanya kiwe halisi huanza kutunza kumbukumbu za matukio mbalimbali yaliyotokea tangu akiwa tumboni mwa mama. Hapo ni sawa na kusema huamini yote au kazi yake ni kuamini kupokea na kutoa kumbukumbu au tunaweza kuziita stoo ya binadamu na imani huhifadhiwa hapa. Kadri unavyojaza neno la Mungu ndani ya sehemu hii ya pili ndivyo imani yako inavyoongezeka na kuzidi kukua. Hufanya kazi kwa kuelewa(Intellegence_ kujiendesha yenyewe kwa kasi sana na kuweza kuratibu kila kitu ndani ya mwili kwa kasi ya ajabusio kwa maamuzi binafsi.huwezi kutawala kitu kilichoingia humo zaidi ya kuingiza mbadala wake yaani (opposite). Yaani kama umeingiza mawazo ya kuwa wewe ni wa shida sana huwezi kuyaondoa mpaka uingize mawazo mbadala kwamba wewe ni wa mafanikio na ushindi katika jina la Yesu. Tumejifunza kwamba huyafanyia kazi yote  iliyopokea yawe ni hasi,au chanya ndio maana tunapatwa na yote tunayowazia si yale tunayohitaji. Hupokea na kuyafanyia kazi mawazo yanayochukua muda mrefu au zile hisia kali Deep fearing  zilizotoka sehemu ya kwanza. Pia hupokea na kutoka sehemu ya tatu ya akili (Super conscious) yaani hupokea na kuhifadhi kumbukumbu zote zinazotoka katika ulimwengu wa Roho na hufanya yaeleweke yale yanayotoka rohoni au roho mafunuo na maono huhifadhiwa hapa . pia kinapotokea kitu cha kuogofya na ama mtu kushtuka inafanya mwili kutumia nguvu ya ndani Inner Power ambayo si rahisi kwa binadamu kuamua kuitumia anavyotaka. Zinakuja zenyewe mfano huamsha kinga Immune za mwili kumfanya mtu aweze kukimbia sana anapostuka ghafla na kurekebisha hali ya mwili mtu anapoumia n.k. kwa kweli tumeumbwa kwa jinsi ya ajabu na ya kutisha Zaburi 139:14
Sehemu hii huhusika katika kuhifadhi kumbukumbu,mambo yote yaliyofanyika au kutokea katika maisha yako yamehifadhiwa mahali hapa. Iwe unayakumbuka au umeyasahau bado yapo huendesha na kufanya kila kitu kinachofanyika katika mwili wa binadamu yaani kuratibu utendaji wa mwili

SEHEMU YA TATU YA AKILI (Super subconscious mind)
Hii ni sehemu ya juu sana ya akili ya mwanadamu ni eneo ambalo mwanadamu hana uamuzi nalo kabisa. Ni eneo ambalo ni muunganiko war oho ya mwanadamu na ulimwengu wa Kiroho. Ni roho ya mwanadamu inapoungana na nafsi ya mwanadamu . ni Universal lipo ndani ya akili ya mwanadamu lakini linaweza kutoka na kupokea ungamuzi pasipo kutumia milango mitano ya fahamu. Ni chanzo cha vitu vinavyotoka kwa Mungu yaani furaha,upendo,amani n.k. mambo yote yanayotoka kwa Mungu au kwa shetani kuja kwako huingia kupitia eneo hili. Kwa mfano unapotaka uwe na furaha na unapomuomba Mungu furaha,sehemu hii ya tatu hupokea furaha kutoka kwa Roho wa Mungu na kuiambia sehemu ya pili kwamba ipokee na kupeleka furaha ndani ya mhusika na mara mtu huyo anakuwa na furaha. Hii ni sehemu mojawapo inayotutofautisha na wanyama. Hata waganga wa kienyeji na wachawi hutumia sehemu hii ili kuwasiliana na mapepo na shetani,pamoja na kupokea nguvu kutoka kwa pepo na mashetani wao kwa kutumia eneo hili. Kama unavyojua kwamba shetani hajaumba kitu kitu chochote ila anatumia vitu vilivyoumbwa na Mungu kwa faida yake. sehemu hii huweza kuwasiliana nje ya mwanadamu,yaani huweza kuwasiliana na mtu mwingine wa mbali. Mfano wewe umekuwa mbali na familia yako na inatokea mtu mmoja wa familia yako anaugua au anakufa na wewe uliye mbali unajua  au unahisi kuwa hilo limetokea na baada ya muda unathibitisha tukio kwa kupata taarifa. Hata Roho Mtakatifu hutumia eneo hili kwa kutupa mambo ya kufanya maelekezo mbalimbali pamoja na tahadhari nayo mfano ajali,hatari ya wanyama,mashambulizi ya kiroho na hata mambo mazuri yajayo. Wakati kuna watu wamejaliwa kwa hali ya juu sana kutumia kipawa hiki wana uwezo wa ajabu kuna wengi wao ambao huutumia vibaya uwezo huu kwa kumika na nguvu za giza na mapepo. Naamini kuwa baada ya mafundisho haya hata wewe unaweza kuitumia eneo hili la akili kwa utukufu wa Mungu.

NAMNA YA KUTUMIA ENEO LA SUPER SUB CONCIOUS MIND KWA FAIDA.
Anza kwa kusoma sehemu fulani ya Biblia inavyoelezea tukio fulani. Rudia tena na tena kusoma na baadae funga macho na ujione kama upo katika tukio hilo. Jione ni mmoja wa wahusika wa tukio lenyewe. Kwa kufanya hii mara kwa mara utajikuta unakua hatua kwa hatua. Kumbuka ni muhimu sana kutumia neno la Mungu vinginevyo ni hatari sana kwako. Watu wengi wa mashariki ya mbali huwa wanatumia sana eneo hili la akili vibaya kwa uchawi. Lakini watu wa ulaya magharibi huwa hawalitumii kabisa kwa kuwa hawaamini sana mambo ya imani za kiroho. Wao mambo yao mengi wanayoamini ni lazima yawe na sababu Reasoning kupitia sayansi na teknolojia. Ni muhimu sana kumuomba Mungu akupe uwezo wa kulitumia eneo hili la akili naye atakupa. Atakupa uwezo wa kuona maono na kuota ndoto kwa maana hiyo ni ahadi yake biblia inasema vijana watapata maono(maono ni mipango) na wazee wataota ndoto si ndoto za kutisha au majinamizi bali ni ndoto za mambo yatakayokuja. Iwapo wewe ni muhudumu wa kazi ya Mungu ni vizuri sana kutumia eneo hili sana ili Mungu awe anakuonyesha na kukuelekeza jambo la kufanya wakati au kabla ya huduma. Fahamu kwamba shetani hupenda kutumia vitu vizuri vya Mungu kwa faida yake. hivyo hupenda sana kutumia eneo hili kwa kuleta maono ya uongo na utabiri(unabii) wa uongo. Ni lazima upime kila unabii na maono kwa kutumia neno la Mungu kwa kila kitu unachokipata.
MAWAZO NA MANENO YANAVYOATHIRI MAISHA YETU.
Kutokana na jinsi mtu anavyoamini, ndivyo jinsi anavyowaza na ndivyo jinsi anavyosema na jinsi unavyosema ndivyo jinsi ulivyo. Hapo ninaweza kusema kwamba uko jinsi ulivyo kutokana na mawazo uliyojiwazia na maneno uliyojisemea jana (Isaya 57:19). Akili ya mtu inanasa kila kitu anachowaza mtu kuhusu yeye mwenyewe na kwa namna ya pekee kabisa (Kwa uwezo wa Mungu). Akili inakifanyia kazi kile unachokiwazia na kukitamka kuwa kitu halisi. Hivyo basi kila wakati unapowaza kitu ni sawa na kupanda mbegu katika maisha yako. Ambayo itakuja kumea siku za usoni ziwe mbaya au nzuri. Mfalme Daudi alimwambia mwanawe  Sulemani kwamba Mungu huchunguza mawazo (1Nyakati 28:9-10). Sisi tumeumbwa kama watawala (Mwanzo 1:26) kwa maana hiyo tunatakiwa kuishi kama watawala lakini pia tunatakiwa kuwaza kama watawala Mungu hapendi tuwaze mabaya (Mithali 6:16-19) na wala usiyakumbuke mambo ya nyuma ambayo ulikosea (Isaya 43:18) unapongangania kuyakumbuka mambo ya nyuma na kuyatafakari kila wakati. Ni sawa na gari lililokwama kwenye matope mchanga haliwezi kwenda. Hivyo ni lazima ujinasue hapo ulipo katika fikra. Sisi tumeumbwa kwa ajili ya leo tu na tunatakiwa kuitumia jana katika kujifunza na si katika kujuta. Ukianza kujuta na kujihukumu au kuhukumu wengine kwa yale ya jana utakuwa unajiletesa mwenyewe na kukwamisha maendeleo yako.

CHUKUA HATUA YA KUBADILIKA.
Usipoamua kubadilika mwenyewe hakuna atakayeweza kukubadilisha. Uamuzi na ufunguo wa kubadilika unao wewe. Ukibadilika unavyowaza utabadilika unavyoishi. Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya mawazo yako na jinsi ulivyo. Kuna wale wanaoumia kwa ajili ya mawazo ya kesho. Si vibaya kuwaza na kupanga mambo ya kesho yaani siku zijazo,vilevile ni vyema na haki kujiandaa kwa maisha yako ya baadae kwa kuanzisha miradi na kuweka akiba n.k. tunachoshauri hapa kwamba hakifai ni kusikitika kwa jambo ambalo bado halijakupata au kukutokea kwa mfano unaanza kuhofu jinsi utakavyofukuzwa kazi au jinsi utakavyoshindwa masomo au mitihani yako. Mtu mwingine anaona labda baada ya miezi mitatu kodi ya nyumba itaisha badala ya kufikiria jinsi atakavyoipata yeye anafiri jinsi mwenye nyumba atakavyomfukuza na kumtukana usisahau kwamba Yesu Kristo alituonya.(Mathayo 6:34) kumbuka hakusema tusijipangie mipango ya baadae wala hakusema tumia vyote unavyopata leo. Mungu anajua hayo tunayoyafanya na tunatakiwa tuyafanye (Mt 6:26) kwa  kujisumbua na mawazo na mawazo ya kesho ndio adui anapata nafasi ya kukushambulia. Akili zetu hazijaumbwa ili kukaa na hasi, sasa unapokuwa mtu wa hasi, yaani unawaza hasi,unasema hasi ile sehemu ya pili ya akili huyahifadhi hayo. Baada ya kuwaza kwa muda mrefu mawazo hayo huhamishwa sehemu ya pili ili kuhifadhiwa kwa ajili yatokee dhahiri. Sasa yanapofika sehemu ile ya pili hutokea mambo 3 ambayo ni.
(a)  Kwa kuwa hatujaumbwa ili kuwaza hasi,basi mfumo mzima wa uendeshaji wa mwili huvurugika. Damu itaenda kasi au itapunguza kasi na hapo kuna hatari ya kupatwa na shinikizo la damu BP. Nyongo itamwagika tumboni wakati isipohitajika na hapo kusabababisha hatari ya kupatwa na vidonda vya tumbo na maradhi ya tumbo. Pamoja na chakula kutokusagika vizuri zaidi hayo figo,bandama na viungo vingine vingine vya mwili vinaweza kushindwa kufanya kazi inavyotakiwa na kusababisha magonjwa mengi mwilini. Pia ubongo huvurugika na kuanza kuchanganyikiwa na kuwa na msongo (depression)kali ya maisha.
(b) Tukio lingine ambalo hutokea na ambalo pia ni baya ni kwamba ndani ya kumbukumbu zako kutajaa akiba mbaya (hasi) na kama kukijaa akiba mbaya utakuwa ni mtu wa kuwaza hivyo tu maisha yako yote kwa kuwa umepanda mahindi utavuna mahindi tu na wala si vinginevyo. Kila siku utakuwa mtu wa huzuni hata kama utataka ziondoke hazitaondoka kwa kuwa zina mizizi ndani kabisa ya akili yako.
(c)  Jambo jingine ambalo litatokea ni kwamba yale yaliyojaa katika sehemu hiyo ya pili yanapelekwa sehemu ya tatu ili yaandaliwe mazingira ya kuwa kuwa dhahiri kama eneo hilo limejaa hasi basi shetani atachukua hatamu na kuanza kutengeneza mazingira ya kuteseka kwako. Wingi wa mawazo hasi ndani ya akili ya mtu huleta “tension” hali ya kuwa na mchecheto au mashaka na wasiwasi wa mambo yajayo. Ukitaka kujua athari ya mawazo hasi yanavyoleta uharibifu utaona mambo yafuatayo na jinsi yanavyotokea mwilini mwako.
·        Kulala sana au kukosa usingizi.
·        Shinikizo la damu BP.
·        Kupungua uzito mara kwa mara.
·        Kukosa hamu ya kula chakula.
·        Kutokuhisi njaa au kula kupita kiasi.
Haya ni mambo ya awali kabisa yanayoashiria kuwa mwili wako umeathirika na mawazo hasi.

ITAENDELEA...










Maoni 1 :

  1. KAIZA nzuri sana mpendwa.
    Wasomaji wanaweza pia kupitia Kitabu cha WEKA UFAHAMU WAKO HURU. kilichoandikwa na John f. Paul.

    JibuFuta