Jumamosi, 23 Juni 2012

KUMBUKUMBU YA MIAKA 27 YA NDOA

Mara kadhaa nadhani umekuwa ukisikia habari au hata kuhudhuria sherehe za kumbukumbu za ndoa za wanandoa waliodumu kwenye ndoa zao kwa kipindi fulani. Kila ulipopata kuhudhuria "shughuli hizi" umekuwa ukitafsiri vipi? unazipa uzito wowote?
Katika tukio linaloonekana hapa pichani ni picha za Wachungaji na ambao pia ni waangalizi wa makanisa ya KLPT.Wakimtukuza Mungu kwa kutimiza miaka 25 ya ndoa bila ya migogoro na mimi ninawatakia maisha mema ya heri na baraka tele.

Wachungaji George na Christina Nywage wa kanisa la KLPT Parishi ya Tanga wakiwa katika sura za furaha na shukrani kwa Mungu kwa kutimiza miaka 27 ya ndoa yao. kumbukumbu hii ilifanyika katika kanisa wanaloliongoza lililopo majani mapana Tanga.
Washirika wa kanisa la KLPT majani mapana Tanga wakienda kuwapongeza wachungaji wao kwa kutimiza miaka ishirini na tano ambayo si kidogo.
ni wazi kuwa kuna umuhimu wa kubadlisha pete sasa maana zile za kwanza ni wazi kwamba zitakuwa zimechakaa kwa sababu hiyo zinahitajika pete mpya katika pendo ambalo kila siku linazidi jana na hii ni mfano mwema wa kuigwa kwa washirika na watu wa Mungu wa Tanga.
Hapa wanapongezana baada ya kuvalishana Pete. hakika inapendeza sana kwako mtazamaji wangu,lakini je wewe umewahi kufikiria kumtukuza Mungu kwa jambo lolote? au unaona kila kitu ni haki yako.
washirika wa KLPT hawakuwa nyuma bali walikuja na zawadi za kuwapongeza baba na mama mchungaji kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwalea watoto wao wa kimwili katika maadili mema ya kuigwa lakini pia kwa kuwatunza watoto wa kiroho waliokabidhiwa na Yesu kristo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni