Jumatatu, 17 Februari 2014

USHUHUDA MKUBWA WA KHOSROW



Alipokuwa mtoto mdogo Khosrow alijiuliza “maana ya maisha”. Vitu vyote vilivyokuwa vikimzingira vilizua maswali mengi. Kwa nini maua yana rangi? Kuna nini kwa juu ya nyota? Tunaenda wapi tukisha kufa? Ni akina nani wale “watu waliomo” ndani ya TV? Je wanaenda wapi baada ya kuzimwa kwa TV? Alipokosekana mtu wa kumpa majibu ya kumridhisha kwa maswali yake mengi, alisikitika sana na kubaki na mawazo mazito.
Siku moja kijana huyu alipita karibu na kanisa la Wakristo wa Kiashuru na akaamua aingie ndani, akifikiri kuwa ataweza kupata majibu kwa baadhi ya “maswali” yake. Kumbe kulikuwepo wanawake wachache tu na mchungaji kiongozi ambaye alimpatia box la vitabu aende nalo. Vitabu vyote vilikuwa katika lugha ya kifarsi na pia kulikuwa na nakala ya Agano Jipya, ambayo Khosrow aliisoma kuanzia jalada hadi jalada. Lakini hali ya kusoma peke yake haikuweza kumsaidia kugundua majibu ya maswali yake. Alipohangaika akakitupa kitabu kile chumbani mwake. Ndipo umbo la mtu alifika kwake katika maono. Mtu huyu alimnyoshea mikono yake na kumwambia: “Shika mikono yangu na kila kitu kitabadilika kwako hata milele.” Khosrow alichukua mikono ya mtu yule na aliona hali ambayo aliielezea kama “Umeme ” ilipita mwilini mwake. Alipiga magoti, akaanza kulia. Kwa kupiga kelele kitu ambacho kiliwafanya wazazi wake kumkimbilia chumbani kwake. Walishikwa na butwaa walipomwona kijana wao akilia, jambo ambalo walikuwa hawajaliona kwake kwa miaka mingi sasa.
Maono ya Khosrow hayakuwa mambo ya kubuniwa kichwani mwake! Alirudi tena kwa mchungaji yule aliyekuwa amempatia vitabu na akamwelezea yaliyomtokea. Ndani ya miaka iliyofuata Khosrow alikua kiimani akiwa mwanafunzi wa Bwana Yesu. Kisha hata yeye mwenyewe amekuwa Mchungaji!
Lakini mateso kwa Wakristo huko Iran yalimsababisha akimbilie Uturuki pamoja na mkewe na watoto wao wawili. Hata huko Uturuki kulikuwa na mateso na magumu pia, lakini Khosrow na familia yake waliwafika watu kwa uvumilivu na upendo. Khosrow alianzisha makanisa mengi huko, kabla yeye na familia yake walipolazimika kukimbia tena. Wakati huu walitafuta usalama kwenye makambi ya wakimbizi huko Austria. Walipanda ndege kutoka Uturuki hadi Bosnia na kisha kutoka pale walitembea kwa miguu kupitia milima mikali yenye hatari wakiipita usiku. Walipokuwa wakivuka mto, kijana wao aitwae Yusufu, alikosea na kutokukanyaga vizuri kwenye daraja lisolokuwa imara na hivyo kuangukia kwenye maji ya baridi sana, akimvuta baba yake pia mtoni. Mto ulikuwa umejaa maji mengi na kina kikawa kirefu, na Khosrow alihangaika gizani kwenye maji, alimtafuta bila kumpata kijana wake. Punde si punde, mkewe pia alirukia mtoni ili kuweza kusaidia, lakini alikuwa katika hatari ya kuzama majini. Ghafla Khosrow alihisi kama mtu fulani akimweka Yusufu katika mikono yake. Pia alihisi kama mtu fulani - asiyeonekana machoni pake - alikuwa akimsaidia kumbeba Yusufu kando ya mto. Wote kwa jumla kama familia walikuwa salama, waliendelea kuvumilia majaribu mengi zaidi, hatimaye waliweza kufika Austria kwa usalama.
Khosrow anailinganisha mikono isiyoonekana iliyomwokoa yeye na familia yake usiku ule na mikono ile jinsi alivyohisi siku ile alipomwona Yesu kwenye maono. Aliposimulia habari yake mtu alimdadisi na kumwuliza ikiwa maono yale aliyoyaona yamebuniwa tu kichwani mwake! Ndipo Khosrow alimwuliza mtu huyo ikiwa alikuwa amevaa nguo. Mtu yule alishtuka sana na kushangaa swali, lakini mambo yalieleweka. Maono ya Khosrow yalikuwa ya kweli.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni