Ijumaa, 18 Machi 2016

SOMO : KUFUNGA


Kufunga ni tendo la hiari la kuacha kula chakula na kinywaji,   au kuacha kinywaji,kwa kipindi fulani. Biblia imeandika mifano mingi ya watu waliofunga wengine waliacha kula vyakula vya aina fulani tu kwa muda wa mfungo wao.

Mfano wa hili la mwisho ni ule mfungo wa Daniel wa majuma matatu ambao Biblia inasema;-
 hakula chakula kitamu...nyama wala divai (Daniel 10:3)  

Vilevile kuna mifano michache katika maandiko yawatu waliofunga kula chakula na maji,lakini aina hii ya mfungo kamili si wa kawaida na unatakiwa uhesabiwe kuwa wa ki Mungu ikiwa utazidi siku tatu. 

Kwa mfano wakati Musa alipokaa siku arobaini bila kula wala kunywa chochote,alikuwa mbele za Mungu mwenyewe mpaka uso wake uling'aa (ona kutoka 34:28-29).

alirudia mfungo wa siku arobaini tena,muda mfupi tu baada ya ule wa kwanza (ona kumbu 9:9-18) 

kwa maana hiyo mifungo yake haikuwa ya kawaida. na si vizuri kwa yeyote kujaribu kuiga bila ya msaada wa Mungu. kwa hali ya kawaida haiwezekani mtu kukaa zaidi ya siku chache bila maji. unaweza ukaishiwa maji mwilini na hatimaye kusababisha kifo.  

hatari kwa afya sio kukaa bila maji muda mrefu tu, bali hata kuacha kula chakula kwa vipindi virefu huweza kuwa hatari pia, hasa kwa watu ambao wana matatizo yanayohusu vyakula.

lakini pia hata wenye afya nzuri wanapaswa kuwa makini kuwa makini ikiwa wanapanga kufunga kwa muda mrefu zaidi ya wiki moja.

                           KWA NINI WATU WAFUNGE
Kusudi la msingi la kufunga ni kujipatia muda wa ziada ili kuomba na kumtafuta Bwana, ukisoma Biblia hakuna mahali ambapo kufunga kunatajwa bila kuhusisha maombi. hivyo inatufanya tuseme kwamba kufunga bila kuomba ni sawa na kazi bure.

kwa mfano katika kitabu cha matendo tunasoma sehemu mbili kuhusu kufunga na kote maombi yanatajwa, sehemu ya kwanza (ona matendo 13:1-30) manabii na waalimu katika kanisa la Antiokia walikuwa wakimfanyia Mungu ibada ya kufunga. 

walipofanya hivyo wakapokea mafunuo ya kinabii, na kwa sababu hiyo wakamtuma Paulo na Barnaba kwenda safari yao ya kwanza ya kimisheninari. katika sehemu ya pili Paulo na Barnaba walikuwa wanaweka wazee wa kusimamia mapya huko Galatia.

Tunasoma hivi,na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa na kuomba na kufunga,wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini (Matendo 14:23)

pengine katika mfano huu wa pili, Paulo na Barnaba walikuwa wanafuata mfano wa Yesu,maana yeye aliomba usiku kabla ya kuchagua wale thenashara.(ona Luka 6:12)

Maamuzi muhimu kama kuchagua viongozi wa kiroho yanahitaji kuombewa mpaka mtu awe na uhakika kwamba ameongozwa na Bwana. Kufunga kutatoa nafasi nzuri zaidi ya kuomba kwa habari hiyo.

Ikiwa Agano Jipya linashauri wanandoa kuacha kushirikiana kimwili ili kuongeza muda wa kuomba (ona 1Wakor.7:5) basi ni rahisi kuelewa jinsi ambavyo kuacha chakula kwa muda kuna fanikisha kusudi hilo.

kwa hiyo tunapohitaji kuomba ili Mungu atuelekeze kwa maamuzi muhimu ya kiroho,kufunga ni kitu cha kufanya. Maombi kwa ajili ya mahitaji mengine yanaweza kufanywa kwa muda mfupi sana. (mfano hatuhitaji kufunga ili kuomba sala yaBwana)

                      SABABU MBAYA ZA KUFUNGA.

 Kwa kuwa nimetoa sababu sababu za kimaandiko za kufunga katika agano jipya.hebu tutazame sababu zisizo za maandiko za kufunga.
 Kuna watu wanafungakwa matumaini kwamba itaongeza uwezekano wa Mungu kujibu maombi yao,sivyo,maana Yesu alituambia kwamba msingi wa kujibiwa maombi ni imani,si kufunga (ona Mathayo 21:22). tukumbuke kwamba kufunga hakumbadilishi Mungu hata kidogo.
 Yeye yuko vilevile kabla hatujafunga,na tunapofunga na hata baada ya kufunga.
 kufunga si njia ya kumbana Mungu au namna ya kumwambia lazima ujibu maombi yangu au la sivyo nitafunga mpaka nife!
 huko si kufunga ki Biblia- huko ni kugomea chakula wakuu!
 Kumbuka Daudi alifunga na kuomba kwa siku kadhaa ili yule mtoto wake mgonjwa waliyezaa na Batsheba asife. lakini mtoto alikufa kwa sababu Mungu alikuwa anamwadhibu.
 Kufunga kwa Daudi hakukumbadilisha Mungu kwa sababu hakuwa anaomba kwa imani,hakuwa na ahadi yeyote ya kusimamia.alikuwa anafunga na kuomba kinyume na mapenzi ya Mungu kama matokeo yalivyoonyesha.

Kufunga si sharti la kupata uamsho,kama wengine wanavyofikiri katika Agano Jipya hakuna mfano wa yeyote ambaye akifunga kwa sababu ya uamsho.

Badala yake tunawaona mitume wakimtii Yesu kwa kuhubiri injili. Kama mji haukupokea injili walikung'uta mavumbi miguuni pao na kusafiri hadi mji uliofuata (ona Luka 9:5 Matendo 13:49-51) hawakuketi mahali na kufunga wakisubiri uamsho.

Vilevile kufunga si njia ya kutiisha mwili maana shauku ya kula chakula ni kitu halali na si dhambi (ona Wagalatia 5:19-21) uone orodha ya tamaa za mwili ila kufunga ni zoezi la kujitawala -au kiasi- na hiyo ni sifa inayohiyajika ili kuenenda katika Roho,si katika mwili.

Kufunga kwa kusudi la kuboresha kiroho chako au kutangaza jinsi unavyompenda Mungu ni kupoteza wakati na ishara ya unafiki hiyo ndio sababu iliyowafanya mafarisayo kufunga na Yesu aliwasema kwa hili (ona Mathayo 6:16;23:5)

Watu wengine hufunga ili kumshinda shetani hilo nalo si maandiko. maandiko yanatuahidi kwamba tukimpinga shetani kwa imani katika neno la Mungu naye atatukimbia (ona Yakobo 4:7; 1Petro 5:8-9) hapo kufunga hakupo.

LAKINI NI YESU ALISEMA KWAMBA KUNA MAPEPO MENGINE YASIYOTOKA ISIPOKUWA KWA KUFUNGA NA KUOMBA.
 maneno haya yalisemwa kwa habari ya kumweka mtu huru kutokana na pepo lililokuwa limempagaa,si kwa habari ya mwamini anayehitaji kupata ushindi juu ya mashambulizi ya shetani kinyume chake.
 SWALI? 
Jee maneno ya Yesu hayaonyeshi kwamba tunaweza mamlaka makubwa zaidi juu ya mapepo kwa kufunga kumbuka kwamba baadhi ya wanafunzi wa Yesu walipomuuliza kwa nini wao walishindwa kumtoa pepo.

kwanza alijibu ni kwa sababu ya imani yao ndogo (ona Mathayo17:21), na pengine aliongeza. Namna hii haiwezekani isipokuwa kwa kufunga na kuomba.(Mathayo 17:21 

mimi bado naamini kwamba kufunga hakuwezi kuongeza wala kupunguza mamlaka ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake (ona Mathayo 10:1) 

kama Yesu alitupa mamlaka kufunga hakuwezi kuyaongeza ila kufunga kunatoa muda zaidi wa kuomba na kutafakari na kwa njia hiyo kunaongeza imani katika mamlaka tuliyopewa na Mungu.

            MKAZO KUPITA KIASI KUHUSU KUFUNGA.
Kwa bahati mbaya sana, baadhi ya Wakristo wameunda dini kwa habari ya kufunga,na kufanya kuwa jambo la kawaida sana na hivyo kutotoa matunda yanayotakiwa.

kufunga kunatakiwa kufanyike katika kutafuta jawabu la jambo mahsusi sio kufunga tu bila mpango inakuwa ni sawa na kutumia nguvu kubwa bila sababu sawa na kuua mbu kwa nyundo.

namshukuru sana Mungu kwa uaminifu wake,mara nyingi amekuwa akinionyesha hatari ambazo ziko mbele yangu ama katika familia, kazini au kanisani na amekuwa akinielekeza namna ya kufunga. 

ninayo mifano mingi sana ambayo nafasi haitoshi kukuelezea lakini kila tatizo kabla halijatokea nilikuwa naambiwa funga ama siku moja, mbili au tatu na jambo linapotokea unakuta halina nguvu kabisa  
kuna wakati watu walinitegea mtego mbaya kazini ili wanifunge kwa rushwa Mungu alinielekeza kufunga siku moja tu na usiku ule nilimuona Mungu kama moto unaoteketeza kile chuo nikamuuliza Mungu kwa moto huu kuna mtu atabaki hapa akanijibu hatabaki mtu. 

huu ni ushuhuda wa ajabu sana na ni mrefu lakini kwa kifupi kile Chuo hakubaki mtu wote walisambaratika na wengine kushitakiwa. na hapo nilifunga siku moja tu lakini kwa maelekezo.

nasisitiza tena kwamba kufunga ni moja ya silaha kubwa ya kuongeza imani ambayo haipaswi kuitumia hovyohovyo.inapaswa kutumiwa kama silaha ya mwisho yenye nguvu ambayo inapaswa kutumiwa kwa uangalifu sana.

Tatizo lingine ninaloliona ni kwamba hakuna mafundisho yanayotolewa kwa waamini kuhusu jinsi ya kufunga,au watu wafunge vipi. kwa kweli ukiangalia katika Agano Jipya habari za kufunga hazijatatiliwa mkazo na inawezekana ndio sababu 

mafundisho ya kufunga ni machache na watu wanafanya kama jadi tu, tofauti na Agano la kale kufunga kulikuwa na sehemu kubwa zaidi mara nyingi kuhusisha na wakati wa maombolezo au wakati wa toba kwa taifa na wakati wa maombi ya dhati katika vipindi vya matatizo kitaifa au kibinafsi.

ukiangalia Isaya 58:1-12 na Zekaria 7:1-14).inaonyesha kwamba watu wa agano la kale walitia bidii zaidi katika kufunga na kupuuza amri zingine muhimu zaidi kama vile kuwajali maskini.
 Bwana Yesu ambaye alifanya huduma yake wakati wa agano jipya hatuwezi kusema kwamba alitilia mkazo sana kufunga alishtakiwa na mafarisayo kwa kutotilia mkazo wa kutosha kuhusu kufunga (ona Mathayo 9:14,15) na aliwasema wao kwa kutilia mkazo kupita kiasi kuhusu kufunga (Luka 18:9-12)
 lakini pia Yesu aliwafundisha wanafunzi katika mahubiri yake ya mlimani aliwaagiza wafunge kwa sababu maalum kama kielelezo kwamba sio kila nyakati tunafunga bali kwa wakati maalumu na jambo mahsusi.
na pia aliahidi kwamba Mungu angewapa thawabu kwa sababu ya kufunga kwao na yeye mwenyewe alifunga kwa kiasi fulani (ona Mathayo 17:21)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni