Jumatano, 1 Februari 2017

SOMO: ROHO MTAKATIFU NA MAMBO YAKE (4)


Mwl: Furaha Amon

Utangulizi:
Watu wengi mno ndani ya makanisa wana kiu ya kupata ujazo wa Roho Mtakatifu, lakini bado kuna tatizo kubwa sana linalohusiana na kutomwelewa vizuri Roho Mtakatifu. Kwa kuwa kiu hii ni kubwa, na tatizo la kutomwelewa Roho Mtakatifu ndani ya kanisa ni kubwa sana nimeona ni vema nitumie nafasi hii kutoa mchango kidogo wa kukusaidia kuelewa kwa kiasi habari za Roho Mtakatifu.

TOFAUTI YA HUDUMA YA ROHO MTAKATIFU KATIKA AGANO LA KALE NA KATIKA  AGANO JIPYA
Roho Mtakatifu hakuanzia wakati wa Agano Jipya, yeye kama nafsi ya tatu ya Mungu, hivyo hana mwanzo wala mwisho. Kwa maneno haya, napenda utambue kuwa Roho Mtakatifu alikuwa akihudumu kwa namna fulani hata wakati wa Agano la kale. Ijapokuwa ilikuwa tofauti sana ilivyo sasa katika Agano jipya. Zipo tofauti nyingi za huduma ya Roho Mtakatifu wakati wa maagano haya mawili; zifuatazo ni baadhi ya tofauti hizo.
Wakati wa agano la kale makao makuu ya Roho Mtakatifu yalikuwa mbinguni. Tunapoyaangalia maisha ya mashahidi wa kazi ya Mungu katika Agano la kale, na wale wanaojulikana kama mashujaa wa imani, tunaweza kuona kwa dhahiri jinsi huduma ya Roho Mtakatifu livyozifaikisha njia zao.
n Roho Mtakatifu aliwasaidia kuwaonya watu na kuwakemea
n Kwa Roho mtakatifu mashujaa hawa waliua samba na dubu
n Mashujaa hawa walitenda mambo mengi makuu yasiyoelezeka kwa akili za kibinadamu.
Wakati wakutenda huduma zote hizi. Roho Mtakatifu alikuwa na makao yake ya kudumu mbinguni pamoja na Mungu Baba na Mwana.

KATIKA AGANO JIPYA, TUNAONA UHAMISHO WA MAKAO YA ROHO MTAKATIFU HUYU WA MUNGU; BADALA YA KUKAA MBINGUNI ALIHAMIA NA KUKAA NDANI YA KANISA, KAMA YANENAVYO MAANDIKO.
Yesu alipokuja kukaa duniani; mbinguni aliwaacha wawili, ambao ni Mungu Baba na Mungu Roho Mtakatifu. Alipomaliza  huduma yake duniani alisema maneno haya kabla ya kwenda kwa Baba yake; Alisema,
“Nami nitamwomba Baba, naye atawapa msaidizi mwingine, ili akae nanyi milele”. (Yohana 14:16.)
Kwa hiyo baada ya Yesu kupaa mbinguni, walikuwepo tena watatu mbinguni kwa muda wa siku kumi. Watatu hawa ni Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, baada ya siku hizo kumi baada ya kupaa kwa Bwana, Roho alikuja duniani kuchukua nafasi ya Yesu; na kuanzia wakati huo hadi wakati huu, wako wawili mbinguni, Baba na Mwana na duniani yuko mmoja naye ni Roho Mtakatifu.

KATIKA AGANO LA KALE ROHO MTAKATIFU ALIKUWA KWA WATU WACHACHE TU;
Udhihirisho wa huduma ya Roho Mtakatifu katika Agano la kale ulikuwa tofauti sana na ilivyo sasa. Katika agano la kale Roho Mtakatifu alikuwa anafanya huduma na kudhihirisha nguvu zake kwa watu wachache waliokuwa na huduma maalumu mbele za Mungu au kwa taifa teule la Bwana, ili tupate picha iliyo kamili hebu tuangalie baahi ya watu walioshuhudia huduma na udhibitisho wa nguvu za Roho Mtakatifu vikitenda kazi ndani yao wakati wa Agano la kale.
KWA WAAMUZI NA WAFALME WA TAIFA LA ISRAELI
Waamuzi na wafalme katika taifa la Israel walikuwa ni muhimu mno katika taifa hilo. Makundi haya mawili ndiyo yaliyotunza nuru ya Mungu wakati taifa lao lilipokuwa linaingia katika giza nene. Kwa umuhimu huo waliokuwa nao. Mungu Roho Mtakatifu alifanya kazi katika maisha yao yote, ila walipomwacha Mungu Roho wa Mungu naye aliweza kuwaacha kwa huduma hii ya Roho Mtakatifu, waamuzi na wafalme, waliweza kuzima nguvu za majeshi yenye nguvu, walirarua simba na muda wote walipopigana au kuongoza chin ya uongozi wa Roho Mtakatifu, waliweza kushinda na zaidi ya kushinda.
MANABII NA MAKUHANI
Manabii na makuhaniwalihusika sana kuongoza taifa la Israeli kiroho; wao walikuwa ni mkono na sauti ya Mungu katika taifa la Israel kiroho; nasema hivi kwani kupitia kwao, Mungu aliyaweka maneno yake aliyotaka kunena na watu wake, kupitia kwao Mungu pia aliweza kupokea toba ya watu wake na dhabihu zao.
MWISHO WA SOMO LA NNE

Kwa leo somo letu linaishia hapa, usikose kufuatilia sehemu inayofuata ya somo hili. Kwa msaada zaidi tuwasiliane 0677 609056

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni