Alhamisi, 2 Februari 2017

KUSIKIA SAUTI YA MUNGU KUPITIA PICHA, MAONO NA NDOTO (1)




NDOTO NI NINI?
Ndoto ni picha au matukio mbalimbali ambayo mtu anaweza kuyaona wakati akiwa macho au akiwa kwenye usingizi.
Ndoto ni njia mojawapo ya mawasiliano ya mtu na ulimwengu wa roho, Mungu anaweza kuzungumza na wewe kupitia ndoto, lakini pia hivyo hivyo na shetani naye anaweza kuzungumza na wewe kupitia ndoto.
Lakini pia hata wewe mwenyewe unaweza kuota ndoto kutokana na uchovu au kuwa na mawazo mengi, na kwa sababu hiyo upo umuhimu wa kugusia jambo hili la ndoto katika somo letu.
Kuna ndoto zingine ukiota zinajieleza waziwazi wala hazihitaji tafsiri kwa maana ya kwamba ndoto inavyosema ndivyo itakavyomaanisha, lakini pia kuna ndoto zingine zinakuja kimafumbo hizi zinahitaji tafsiri.

MAONO NI NINI?
Maono ni uwezo wa kuona mambo kwa macho ya kiroho kama vile Mungu ayaonavyo, mtu anaweza kuwa na fahamu kamili na macho yaliyo wazi na akaona mambo kama vile tunavyotazama luninga.
Lakini vilevile mtu anaweza kuondolewa ufahamu kama vile amelala usingizi na akaona vitu waziwazi na kusikia sauti ikisema anagalia (Matendo 10:9 - 20)
Petro alikuwa amezimia, lakini macho yake ya kiroho yaliweza kuona maono ya kifurushi cha wanyama mbalimbali. Akiwa katika hali hiyo aliweza kuongea na kuisikia sauti ya Mungu.

Tukilala usingizi ni mwili unaolala kwa maana roho zetu zinakuwa macho. na kama kuna nguvu za giza roho yako huwa inaziona na inapambana nazo katika harakati za kuurudisha mwili katika ufahamu wa kawaida, na hapo ishara kwako itakuwa ni kuota ndoto za kupigana na kuweweseka.
Vivyo hivyo hata kifo kinapotokea ni mwili huharibika lakini roho huwa hai.
UJUMBE WA MUNGU KATIKA NDOTO
Je, unaamini ya kuwa Mungu anaweza kusema na wanadamu kwa njia ya ndoto? Najua na inawezekana ikawa ni lahisi kuamini kuwa Mungu alisema na watu wa zamani kwa njia ya ndoto kama tunavyosoma katika Biblia;
lakini  je! Unaamini ya kuwa Mungu anasema na watu kwa njia ya ndoto siku hizi?
AINA TATU ZA NDOTO
Kwa mujibu wa Biblia kuna ndoto za aina tatu (3)
1. Ndoto kutoka kwa Mungu.                     Sikilizeni basi maneno yangu! Akiwapo nabii kati yenu, mimi Bwana nitajifunua kwake katika maono, nitasema naye katika ndoto.” (Hesabu 12:6)                                                       



Biblia inasema tena;- “Hata itakuwa baada ya hayo. Ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili ; na wana wenu waume kwa wake, watatabiri wazee wenu wataota ndoto na vijana watapata maono”   (Yoeli 2: 28)

2. Ndoto za uchovu                                      ndoto hizi zinazokuja kwa sababu ya shughuli nyingi Biblia inasema “kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi” (Mhubiri 5:3)


3. Ndoto za uongo
                                   ndoto hizi ni zile zinazotoka kwa shetani baba wa uongo Tazama,mimi ni juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema Bwana, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao na kwa majivuno yao ya upuuzi;lakini mimi sikuwatuma, wala kuwapa amri; wala hawatafaidia watu hawa hata kidogo asema Bwana. (Yeremia 23: 32)                                                 Ninyi ni wa baba yenu ibilisi, na tama za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa sababu yeye ni mwongo. Na baba wa huo (Yohana 8:44)
Tukutane tena katika sehemu ya pili, ambayo tutaangalia mambo ya msingi kuhusu kutafsiri ndoto.
Furaha Amon Mob: 0713 461593 - Tanga

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni