Jumatatu, 3 Septemba 2012

SAFARI YETU MBEYA KWA TRAIN

Mara nyingi sana nilimsimulia Flora habari mbalimbali za vijiji vilivyomo pembezoni mwa reli ya Tanzania na Zambia TAZARA na alionyesha hamu sana ya kusafiri na Treni kwani alitaka kufahamu historia na jiografia ya nchi yetu kupitia tazara. na hatimaye tulipanga safari kutoka Tunduma kwenda Dar es salaam.
Huu ni mji wa Vwawa Mbozi ambako ndio nyumbani kwetu ambako wazazi wangu baada ya kustaafu kazi serikalini waliamua kuishi katika mji huu, na sisi pamekuwa ni nyumbani kwetu.
Hiki ni kituo cha garimoshi cha vwawa mbozi
Hapa Flora anaonekana akisubiri kwa hamu kubwa sana galimoshi (gogo)
Baada ya muda garimoshi linaingia likitokea Kapirimposhi Zambia
Flora akikusanya vifaa vyake ili kupanda ndani ya Treni, katika kituo kama hiki Garimoshi hutumia dakika 15 tu.
Baada ya kuingia ndani na kupatiwa chumba ambacho atakitumia kwa kukaa na kulala Flora anaweka vitu vyake sawa
Baada ya hapo tulielekea Buffet kwa ajili ya chakula na vinywaji.
mpaka hapo Flora alikuwa bado hajalikubali Treni aliniambia ni kama linayumba sana nikamwambia atulie ataifurahia tu safari maana tutapita mpaka kweny mbuga za wanyama za Serous ataona wanyama mpaka atasinzia.
Hapa ni safari na muziki wa ala wewe ni kuweka vesi tu maana chuma kwa chuma ni mdundo tu.
Kutoka Tunduma abiria walikuwa wachache sana tofauti na miaka ya nyuma ninavyokumbuka hapa hotelini ilikuwa ni hekaheka muda wote.
Kwa mbali sana unaweza kukiona kiwanda cha saruji cha Songwe eneo hili ndilo wanalojenga kiwanja kikubwa cha kimataifa cha ndege.
Sehemu nyingine unaweza ukatamani ushuke jinsi palivyotulia.
hatimaye tulipita maeneo ya Mbalizi.
Wakati mwingine hali ya hewa ilianza kuwa ya baridi wafanya kazi wa Tazara walitupatia mablanketi mazito kwa ajili ya kujikinga na baridi.
Hapa ni mbeya mjini tulishuka kidogo kwa ajili ya kunyoosha miguu.
Hii ni shule ya msingi majengo hapa ndipo nilipopata limu yangu ya msingi.
Huyu ni rafiki yangu wa utotoni kabisa anaitwa Fredrick Lupembe hapa nilimtembelea ofisini kwake alifurahi sana tulipoonana maana tunapoteana sana
Kama kawaida ukiongozana na Flora huwa anapenda sana kuchepukia kwenye vitu kama hivi kwa ajili ya kujenga mwili.
Kwa kweli picha hii nimeipenda sana hebu nipige na na sanamu hii.
Mandhari nzuri ya kuvutia inaonekana vizuri kabisa katika milima ya Mbeya.
Picha hii inanikumbusha tulipotoka kuangalia makaburi ya ndugu zetu,sio kama tunaamini kitu fulani kuhusu wafu. Hapana tunakwenda kuangalia kwa sababu ya kutunza kumbukumbu.
huu ndio mtaa ambao mimi nimekulia kwa miaka mingi sana. huwa nikifika naona mabadiliko mengi sana ni kama ukiwa fulani hasa nikikumbuka nilipokuwa mdogo rika la hao waheshimiwa wanaocheza mpira wa makaratasi
Hii picha ilipigwa mwenge kama kumbukumbu na sista wangu Rose na mjomba Munde katika duka la vinyago mwenge.
Na hapa ni safari ya kuelekea mashambani.
Flora akia na wifi yake Naomi wakiangalia maeneo ya mashamba ya familia.
Kwa kweli wakati mwingine ulikuwa ni wakati wa furaha sana kuwa katika maeneo ambayo mnakuja kwa nadra sana kiasi cha mara moja kwa mwaka.
Hii ni kumbukumbu ya kutambulisha mchumba Huyu ni mdogo wangu Cecilia Brown Mwakasege siku mchumba wake alipokuja kumchumbia nyumbani kwao Tabata Liwiti.
Pembezoni kidogo ya Jiji la Mbeya picha hii nimeipiga nikiwa eneo la Majengo nimepiga kuelekea usawa wa Iyunga ambako iko stesheni ya galimoshi *TAZARA.

FREEMASON BIBLIA INASEMAJE?


FREEMASON BIBLIA INASEMAJE?
Wapendwa wana wa MUNGU, naamini hamjambo na mnaendelea vizuri katika kuukulia WOKOVU! Sina shaka kwamba maoni na ushauri unaotolewa na watu mbalimbali kuhusu jamii hii ya siri ya masonry,unalenga kuwaweka wacha MUNGU wa ukweli kuwa katika tahadhari si kwa kundi la Masonry peke yake,bali pia hata kwa kazi zote za yule Adui (SHETANI). Kwanza niwatoe wasiwasi kuwa Masonry si kundi la siri kama ambavyo, yeye mwenyenalo (shetani) anavyojaribu kuongopa! Shetani tangu mwanzo ni muongo,hivyo anatumia welevu wake mkubwa kudanganya kuwa yeye hufanya kazi kwa siri kubwa akitaka “ADUI” zake….yaani wacha MUNGU wakweli waamini kuwa ati yeye anauhakika wa ushindi! Ndg zangu mulio katika BWANA YESU KRISTO, jueni hivi kabla ya kujadili jambo lolote unalodhani kuwa ni tata au ni mhimu kulijadili liwe linaonekana kuwa ni la SIRI au si siri ki-ROHO,JIULIZE HIVI: je, BIBLIA ILISHAPATA KULIZUNGUMZIA JAMBO TAJWA MAHALI NA WAKATI WOWOTE? Sababu ya kufanya hivyo ni, Biblia ndiyo pekee neno la MUNGU,limehakikishwa na ndilo pekee linafaa kwa mafundisho,kwa kuonya(kukuweka katika tahadhali kuu) kukuongoza nakuwaadabisha watu,lakini uwe makini hapa watu wanaozungumziwa hapo ni wale tu WALIOOKOLEWA NA BWANA YESU 



KRISTO,Maana wote walio nje ya WOKOVU hawana bahati hata kidogo ya kujua ufafanuzi utolewao na ROHO Mtakatifu ili kuzijua zile lugha au vitendo anavyo jaribu shetani kuzitafsiri kuwa ni”SIRI AU MAFUMBO MAKUU”ROHO MTAKATIFU kupitia Neno la MUNGU- Biblia, yeye ndiye mwalimu. kama mwalimu hawezi kutoa ufumbuzi wa jambo lolote analolifundisha, Mwalimu huyo ANAPOTEZA SIFA YA KUWA MWALIMU mara moja!! Vivyohivyo,Mwanafunzi asiyeweza kujifunza kwa hamu,kwa bidii,hafuatilii mifano na mazoezi yatolewayo na mwalimu wake,mwanafunzi huyo ANAPOTEZA SIFA YA KUWA MWANAFUNZI maramoja! (wakati enzi sisi tunafuta ujinga ktk kisomo chetu,ambacho vijana waleo wanweza kuiita ni “Ngumbalu”)Wale wote waliokuwa hafuatilii masomo tuliwaita “WASINDIKIZAJI” Sasa jiangalie je wewe si msindikizaji?Lakini pia nikueleweshe hivi,mwanafunzi wa chini hujua elimu ya chini – yaani kila mwanadalasa kwa elimu ya dalasa lake tu,ili mtihani uletwe kwa kiwango cha dalasa lako,lakini si kwa ujuzi wako! sasa jiulize hivi, unashida gani, KUJUA au KUELEWA habari juu ya Masonry? Hilo ni swali la kwanza,maana wanafunzi wasio makini husoma KUJUA jambo na si KUELEWA jambo,ndiyo maana wanaigia na vikaratasi ktk mtihani! baada ya swali la kwanza jiulize swali la mwisho kuwa ukisha JUA au KUELEWA jambo unaloliataka utafanyaje?! Kwakuwa naamini kuwa naongea na wana wa MUNGU, basi hebu ni nimnukuu BW.YESU KRISTO. BABA yetu huyu aliyajua yote haya,kama ujuavyo ni BABA tu,ndiye huwajali watoto wake,maana ni lahisi kuwa mzazi ila “ngoma” inakua,kama unapotakiwa kuwa BABA, labda mtu atajiuliza inawezekanaje kuwa mzazi na usiwe baba au mama? inawezekana,..sitaki kuzungumzia hilo! Ndiyo maana MUNGU huitwa BABA YETU,ila ukitaka kumuuita kuwa ni mzazi wako mimi hapo nanyamaza! Kwa hiyo, YESU akasema…watu wangu wanaangamia kwa kukosa MAARIFA,YAANI watu hufuata akili zao wenyewe ili wapotee! NENO linasema LIPO JAMBO LIONEKANALO NI JEMA MACHONI PA MWANADAMU, LAKINI NI NJIA YA MAUTI! Kwakifupi watu hawataki kukaa chini ya miguu ya Mwalimu apaswae kuwafundisha ili waelewe waokolewe yaani chini ya huyo ROHO MTAKATIFU ,HATUPASWI KUJILAUMU KUWA KTK HALI HIYO maana kama alivyo mwanafunzi wa kawaida hayuko tayari na hapendi kabisa kitu kinachoitwa MITIHANI ,maana kiwago cha ubora wa mwanafunzi yeyote ni kwa kiwango gani anafauru mitihani apewayo na mkufunzi wake! SASA jiulize hauingii na vikaratasi katika mitihani ya mwalimu ROHO MTAKATIFU! Maana huenda iko siku ilijisifia kuwa UNA UPAKO, na kuona kuwa MUNGU amekuokoa wewe tu,kwa vile ulimuombea tasa akajifungua mtoto ukashindwa kuelewa pia kwamba IMANI YA MHUSIKA MWENYEWE IMEMPONYA? kwa wale wanaoamini kuwa YESU ndiye huyohuyo ROHO MTAKATIFU nasemanao hivi, BWANA.YESU KRISTO. mara kwa mara katika kufanya uponyaji alizoea kusema, IMANI Yako imekuponya au na iwe kama ulivyoomba(maana hakuna maombi yakawa maombi bila imani) nk. Ndg zangu nisiwachoshe kwa maneno mengi mno ,ila huo ni mfano mmoja kati ya mifano elfu nyingi inayoonyesha wazi kuwa hatuzijui habari na lugha za mbinguni kwakuwa hatutaki kukaa chini ya miguu ya mwalimu GAMALIERI (ROHO MTAKATIFU) YESU alisema “Zitambueni nyakati” kama ndege na wnyama wanajua sasa ni jioni wanawahi kwenye usalama, je, inakuwaje ninyi watu wa MUNGU? BIBLIA inasema SHETANI yupo, sasa unashangaa nini juu ya masonry na habari za kuwepo kwao? sisemi nivibaya kuyachunguza mambo,ila yafanyeni mambo kwa kumtumia roho mtakatifu, na wala si kwa kuumiza akili kwa namna yoyote ile. Neno la MUNGU si gumu wala si maalumu kwa wachungaji peke yao,limewekwa ili kuwa njia ya wokovu wetu mkuu.MUNGU si kama shetani kwa tabia,shetani hufanya mambo yake kwa siri,lakini MUNGU hufanya mambo yake kwa uwazi na ukweli ili watu wapate kuokolewa. mwisho JILINDENI NA ROHO ZIDANGANYAZO NA MAFUNDISHO YA MASHETANI. Kweli masonry wapo,wawe wanabudu uchi,wanakunywa damu za watu,wanapesa sana wako milioni 6 au zaidi,washirika wao ni watu maarufu nk, ni sawa tu, acha wazidi kuwepo na wale watakao jiunga nao acha wafanye hivyo kadri watakavyo.Maadam NENO la MUNGU linasema jambo hilo litakuwepo kwa sababu zilizonenwa! Kuwepo kwao au kutokuwepo kwao sisi kwa nini? MUNGU ndiye hasa anajua sababu yakuwepo au kutokuwepo kwa jambo lolote.cha msingi MUNGU atupe kinga,ambayo kwakweli alisha tupa,hoja tu ni kwa kiasi gani tunatii-BWANA YESU KRISTO, alisema BILA MIMI NYINYI HAMUWEZI NENO LOLOTE (Ulishapata kujiuliza maana ya ‘KUTOWEZA NENO AU JAMBO LOLOTE?’)
Nimefurahi kuona watu wengi wana hamu sana ya kutaka kuujua ukweli kuhusu FREEMASON nimesoma sana katika mitandao mbalimbali kuhusu ukweli wa hili jambo labda niseme tuu kifupi nimepata elimu kiasi na naamini kila mmoja anaweza kuendelea kuperuzi kwenye mtandao, kuna siri kubwa sana kuhusu hili shirika au hii taasisi ya masonic.ukiangalia ktk mitandao utaona inatumia alama nyingi za kishetani kama alama zao za kuwasilina, na kwa kuwa dunia imekumbwa na hili wapo wanaojua na wasiojua wanazitumia hizo alama katika kila kitu au vitu tunavyomia katika maisha yetu iwe marashii, nguo, alama za magari, urembo, na ishara za mikono na mengine mengi …kimsingi hapa penda usipende unakua unaabudu au kusifu na kutangaza hizo logo na signs ambazo huuziita kitaalam Occult..Manake ni ficha katika kuonekana kwake..Inatisha sana kusikia habari hizi kwa nchi za magharibi kama Marekani iko wazi na si jambo la kificho. Mfano kama pesa ya Marekani imetengenezwa na hao masons angalia dola moja nyuma ina piramidi ambayo haijaishaa na juu kuna jicho. Imendikwa maneno fulani kirumi yakisema kwa Kiswahili .tangaza kuzaliwa. na lingine likimalizia kuanza kwa New word order au ina maana ingine god favour our ages ..huyo mungu wao ambae ni lucifer yaani shetani…anawasaidia vizazi na vizazi ipo wapi na unaweza soma na ukaona mwenyewe mambo yao ni siri na yenye kificho sana wana kivuli cha kwamba sisi ni brotherhood sijui charity, hakuna ni ushetani mtupu…kifupi hawa ni wapinga KRISTO .Ipo jinsi ya mji wa WASHINTON DC umejengwa kwa alama zao ambazo ziko wazi kabisa ….wanaamini katika uchafu wao ila hawaamini WOKOVU kabisa wapo kila mahali ni ngumu kuwaepuka hivyo yatupasa kusimama katika imani kisawa sawa ..lakini pia ni wazi mtaona makanisa mengi yapo na hayana muamko au kuwa hai kiroho na wengi wetu ndio tunaoyapenda kwa kuwa tunaona hayagusi maovu yetu,au kila ukienda hubadiliki kiroho kanisa la hivyo nalo linakosa maana kabisa na wengi wetu tumefungwa na historia kuwa nilizaliwa katika dhehebu hili au dini hii ..hivyo yanipasa kuwa hapo hivyo hata kama hawakutibu kiroho …mimi kwa hapo nakataa yatupasa kubadilika na kuwa hai KIROHO.Acha kufungwa na historia badilika kuna umuhimu gani kusali kama sehemu unayosali haikutibu kiroho? au unajua kabisa na kuona madhaifu yake? Sehemu za hivyo iwe ya UKRISTO au ya dini yeyote inayomwamini MUNGU haifai ….! yapo leo makanisa mengii kila mmoja anasema kwangu ni bora na kwa yule si bora wana mali nyingi na wanasisitiza sana matoleo ,wapo wanaounda miujiza …mimi hadi naogopa kwani wanajua ukweli halafu wanalaghai watu ..Maskini ya MUNGU wengi wa waumini ni maskini wanaotaka kuzikomboa nafsi zao lakini pia wanaingia katika mikono isiyo salama ..hawa pia ni wakuwafanyia maombi sana maana hawana tofauti na freemason ambao wanajificha katika vivuli vya vitu vizuri kama misaada mingi mingi ….haya ma hall kama YMCA ,WYMC ,yote ni product za freemason …tunatakiwa tuombe sanaa saanaa..jaman

Jumapili, 2 Septemba 2012

MATUKIO KATIKA PICHA



Mwimbaji Elizabeth Yohana akiwaongoza waimbaji wa kusifu na kuabudu wa kanisa la KLPT majani Mapana Tanga.











Andrew na Mkewe katika siku ya harusi

Samuel na Rejoice siku chache baada ya kufunga ndoa.

Lucy na ndugu zake katika send off Part Dodoma