Alhamisi, 29 Novemba 2012

JOSE CHAMELEONE BILIONEA ALIYEJARIBU WOKOVU



ninaweza kusema hivyo kwa sababu ilishawahi kutangazwa sana katika vyombo vya habari kwamba gwiji wa nyimbo za duniani mganda Jose chameleone ameokoka. hii ilikuwa ni baada ya kupata maradhi ya kuweweseka katika usingizi na hatimaye kujitupa chini kutoka katika ghorofa ya pili katika hotel aliyokuwa amepanga mjini Arusha. Baada ya tukio hilo bingwa huyu akatangaza kuja kwa Yesu. Lakini hakuendelea zaidi na sijui siri ya moyoni mwake,lakini Biblia inatufundisha kumtambua mtu aliye na Yesu,naamini bado muda upo na nafasi bado iko na Bwana anatamani amtumie wakati huu na sio wakati akiwa amechoka au amekuwa dhaifu kiafya. Najua unajiuliza kwa nini ninamwita Bilionea!




Ndiyo, kwa asiyeamini, hebu angalau baadhi ya mambo yanayothibitisha utajiri wa nyota huyo. 
Anamiliki jumba la kifahari katika vilima vya Sekuku jijini Kampala, pia ana nyumba huko Arizona, Marekani, achilia ile ya Kigali, Rwanda aliyoinunua hivi karibuni kwa mamilioni ya shilingi. 



Ukiachilia mbali gari la kisasa aina ya Cadillac Escalade lililomgharimu zaidi ya Sh milioni 100, Chameleone ambaye ni baba wa watoto watu, pia anamiliki Mercedes Benz, BMW na aina nyingine za magari. 
Kwa ujumla, anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia Sh bilioni 1.5 kwa fedha za Tanzania. Na anasema bado anazisaka, kwani bila ya kuwa na tamaa ya kusaka mafanikio zaidi, ndoto huenda zisitimie. 



Anayasema hayo akisisitiza kuwa, baada ya nyumba, magari na akaunti nono benki, sasa ana ndoto za kumiliki helikopta yake, baada ya kuwa amekuwa akikodi mara kadhaa ama kwenda katika matamasha au kama alivyofanya wakati anamuoa mkewe Daniela Atim.
pia ana jumba lipo karibia na ufukwe wa ziwa victoria kwa upande wa uganda,pia ana apartments kibao huko uganda,hilo cardillac ni zaidi ya million 250 za kitanzania,Ukija kina Bobby winne na Bebe Cool wanamiliki hadi meli na Hummer hizi wanazotembelea kina 50 cent.anakumbuka akiwa na Bebe Cool na Redsun alipata fursa ya kutumbiza katika shindano la kumsaka mrembo wa Kenya. Anakiri hapo ndipo milango ya neema ilipoanza kufunguka. anasema Dorotea ,baada ya kuzoeana alimshawishi ahamie nyumbani kwake badala ya kuendelea kulala studio,ushawishi ambao ulimchukua zaidi ya wiki moja kumkubalia.




 “Nilipohamia tulikuwa marafiki, lakini mengine yaliibuka tukiwa katika nyumba moja. Mara nyingi kila akitoka, alinikuta nimetulia naandika nyimbo, huku akihoji ni lini nitarekodi. Nilikosa jibu kwa kuwa siku wa na fedha. 

Siku moja akiwa safarini huko Afrika Magharibi aliniachia bahasha yenye dola za Kimarekani 1,000 (karibu Sh milioni 1.8 za Tanzania kwa sasa), akaniambia niingie studio ana. 


“Huo ukawa mwanzo wa kibao Mama Mia na sikuamini kama fedha ile ingebadilisha maisha yangu na kunifikisha hapa nilipo. Mengine yanabaki kuwa historia,” anasema. 

Pamoja na utajiri aliovuna kupitia muziki, nyota huyo anasema historia ya kushuhudiwa `Live’ na watu zaidi ya bilioni 9 akitumbuiza wakati wa Kombe la Dunia kwake ni kitu cha kipekee. 

“Mtoto wa Afrika tena Afrika Mashariki kupewa heshima ile haikuwa kitu kidogo. Najiona mwenye bahati na ni mastaa wachache wanaweza kuingia katika kundi la bahati hata wangeishi kwa miaka 1000.” 

Anasema kutokana na baraka alizopata maishani, ameamua kuanzisha taasisi ya Chameleone ili aweze kuwasaidia wasiojiweza. 

“Nikiwa mdogo sikuwa na maisha mazuri, sikutoka katika familia bora, kwa hiyo ninajiona mwenye wajibu wa kuwasaidia wengine wakianzia katika misingi mizuri ya kielimu. “Nimeshanunua eneo kwa ajili ya kujenga kituo. 

Nataka jamii siku moja inikumbuke kwamba niliwika na kuitangaza nchi yangu, lakini pia sikuwa mchoyo, bali niliyatumia vyema matunda ya muziki. 


Kwa kufanya hivi, naamini ipo siku nitawashawishi wengi kufanya mambo makubwa kwa ajili ya jamii wanayotoka.” 

Huyo ndiye Joseph Mayanja ambaye pamoja na misukosuko ya maisha tangu akiwa shule hadi sasa akiwa staa, bado nyota yake inang’ara. 


Je, atazidi kupata mafanikio? Bila shaka ni jambo la kusubiri na kuona, hasa ikizingatiwa kuwa, mwenyewe amejijengea falsafa ya kutolewa sifa, bali kazi kwa kwenda mbele. 

Pamoja na yote, Chameleone anapaswa mfano wa kuigwa kwa wasanii wengi wa Kitanzania ambao huvuma kwa muda mfupi, lakini 

wakishazikamata fedha hupotelea kwenye ulimwengu wa anasa na baadaye kujikuta wakiwa `choka mbaya’, tena wakiwa hawana akiba benki wala hawajawekeza.


Chanzo: kutoka katika mitandao mbalimbali

Jumanne, 27 Novemba 2012

MTOTO WA LUCK DUBE ARITHI KIPAJI CHA BABA YAKE

Marehemu Luck Dube wakati wa uhai wake
Huyu ndiye binti wa Luck Dube aliyekuwa mshindi wa pili katika mashindano ya kuimba nchini afrika kusini
Waombolezaji wakiusindikiza mwili wa marehemu Luck Dube.
sehemu ya mashabiki wa Luck dube wakiomboleza.
Gari la kifahari la Luck Dube ambalo lilikuwa ni shabaha ya wauaji wakehata hivyo hawakuondoka na gari hilo.
Luck Dube akiwa na familia yake.
Wauaji wa Luck Dube wakiwa mahakamani.
Waombolezaji.
Mwanamuziki maarufu Brenda Fassie (Mabree) ambaye kwa sasa naye ni marehemu alishiriki mazishi ya dube.

Jumatatu, 26 Novemba 2012

USHUHUDA MKUBWA WA ALI



Ali
Ali ni mkubwa kati ya watoto tisa lakini hana kumbukumbu yoyote nzuri ya kuwa miongoni mwa familia kubwa hivyo. Walikuwa wakimtania na kumwambia kuwa alikuwa hafanani na mtu yeyote katika familia yake. Mama yake alisema kuwa alikuwa akimchukia na kwamba alikuwa ni mtoto ambaye amefanana naye kidogo sana. Kila siku Ali alijihisi kukataliwa na familia yake na hivyo alipokuwa mtoto alilia sana.
Kwa muda wa miezi minne kila mwaka, Ali alifanya kazi ya kuchunga kondoo. Alianza kazi hiyo alipokuwa na umri wa miaka nane na kuendelea na kazi hiyo hadi alipofikia umri wa miaka kumi na nane. Aliwapeleka kondoo milimani na kwa vile alitumia muda mwingi peke yake alihitaji mtu mwingine wa kuongea naye “alijitengenezea mungu“ moyoni mwake. Mungu huyu alikuwa kama rafiki yake. Angeweza kuongea naye kwa mazungumzo marefu kama vile:“ni vizuri kama nini viumbe vyako ulivyoviumba,“ alipoyaangalia maua, jua, miamba na nyasi. Pengine angeweza kumwuliza huyo mungu swali hili: „Je, utamu wa tunda la apple unatokana na nini?“ Maana aliamini kuwa kulikuwa na Mungu aliyetengeneza au kuviumba vitu vyote vizuri.
Alipokuwa na umri wa miaka ishirini, alianza kunywa pombe sana. Na alipofikia miaka ishirini na mitano alikuwa mlevi wa kupindukia. Wakati mwingine alianza kunywa kabla hata ya saa tatu asubuhi! Aliporudi nyumbani mkewe mara nyingi alikuwa akimwuliza endapo ametoka kunywa pombe. Jambo hili lilimkasirisha mno na kwa hiyo akaanza kumpiga kila siku. Watoto wake walishuhudia manyanyaso hayo na walikuwa na hofu kurudi nyumbani baada ya kutoka shule, kwa hiyo walienda kwenye nyumba za marafiki zao mpaka walipojua kuwa baba yao ameshalala. Ali alitaka sana kuacha kunywa pombe na alichukia sana kwa jinsi alivyokuwa akimnyanyasa mkewe. Hivyo aliamua kuhamia Saudi Arabia ili kufanya kazi kama mkandarasi (fundi mwashi) kwa sababu alikuwa amesikia kuwa ulevi ni kitu kilichokuwa kimekatazwa kisheria. Hata hivyo usiku wa kwanza alipokuwa Saudi Arabia aliona kilevi na akanywa.
Pamoja na kwamba Ali hakuwa ni mtu wa dini, familia yake walisema kuwa ni waislamu lakini hawakujua zaidi kuhusu dini yao. Ali aliamua kwenda Mekka, akitumaini kuwa kwa kutembelea kule kungeweza kumfanya huru kutokana na shida yake ya ulevi. Alisema: „Nilifanya maamuzi moyoni mwangu. Ninaenda kufanya hija ya kweli. Nitakuwa mwislamu halisi na nitaacha kabisa kunywa pombe.“ Usiku ule ule wa kwanza alipokuwa Mekka, Ali aliota ndoto. Katika ndoto ile, alimwona Yesu akishika mkono wake na kumwambia: „Wewe ni wangu.“ Pia aliweka kidole chake kwenye paji la uso la Ali na kusema: “Unahitaji kutoka mahali hapa na kuondoka sasa.” Ali alipoamka alihisi kama alikuwa akielea hivyo akaligusa zulia lake kuhakikisha kuwa alikuwa kwenye nchi kavu. Aliendelea kuisikia sauti ya Yesu ikisema: „Unahitaji kufuatana nami, wewe ni wangu.“ Marafiki zake Ali waliona alama iliyokuwa iking’aa katika paji lake la uso mahali pale ambapo Yesu mwenyewe alikuwa amemgusa, lakini yeye mwenyewe Ali alipojitazama kwenye kioo hakuona chochote. (Alama hii kwenye paji lake ilionekana kama vile „sim,“ aina ya mng’ao ambao hutumika kwa kuwapamba mabibiarusi wa kituruki.)
Ali aliendelea na hija yake. Hata hivyo gari lake alilokuwa nalo kwa mwezi mmoja hivi, liligoma kuwaka ili lianze kutembea. Aliendelea kuisikia sauti ya Yesu: „Unahitaji kuondoka hapa.“ Mara tu alipobadilisha mawazo yake na kuondoka pale Mekka, gari lake liliwaka na kuanza kutembea! Alienda nyumbani kwenye chumba chake alichokuwa amepanga na akasikia sauti ile ile tena. Hapa Bwana Yesu alimwambia kuwa anatakiwa aende Uturuki. Baada ya siku tatu alikuwa Uturuki kwenye sherehe ya „kumkaribisha nyumbani“. Hapo tena akasikia sauti. Wakati huu Yesu alimwambia kuwa awaambie watu wote waliokuwepo pale kuwa, yeye amekuwa Mkristo sasa. Alifanya hivyo, lakini watu hawakutilia maanani juu ya jambo lile la kuokoka.
Hakujua hilo mpaka baada ya miaka michache baada ya ile ndoto ndipo Ali alipoanza kufahamu ina maana gani kuwa Mkristo aliyeokoka. Alikuwa akisikiliza redio aliposikia sauti ikisema: „Yesu alikufa, akafufuka kutoka kwa wafu baada ya siku tatu na sasa anakaa mkono wa kuume wa baba.“ Alimwita mkewe na kumwambia kwamba ameshaipata sauti ya Yesu – ndani ya redio. Kupitia kipindi hicho katika redio, alipokea masomo ya Biblia na pia alipokea Agano Jipya mpya! Alikuwa na umri wa miaka 38 wakati ule na alisema kuwa siku aliyopokea Agano Jipya lile kwa njia ya posta “pengine ilikuwa ni siku ya furaha kubwa maishani mwake kuliko siku yoyote.” Baada ya kumaliza baadhi ya masomo kwa njia ya posta, Ali pamoja na familia yake walihamia Istanbul ili kuweza kusoma shule ya Biblia.
Mpaka leo anaendelea kushuhudia imani yake ya kikristo kwa uwazi na hata bila ya aibu. Ulevi haukuendelea tena kumtawala, na akawa akimtunza na kumpenda mkewe ambaye hapo kwanza alikuwa akimtenda vibaya. Kweli, sasa amekuwa ‚kiumbe kipya ndani ya Kristo.‘


Alhamisi, 22 Novemba 2012

HABARI KATIKA PICHA

Mpiga picha akiwa makini sana katika kupata picha nzuri.nafikiri hapo anawahimiza watabasamu kidogo ili picha itoke vizuri zaidi.
Gari aina ya Fiat (mbaula) ikiwa imebeba mabua
Picha hii inajieleza yenyewe umuhimu wa kuwa na mke mwema
hapa ni gari dogo aina ya PicUp ikiwa imebeba mzigo usio wa kawaida
Hapa ni mahali fulani gari likiwa limebeba mzigo na abiria
Askari akiwa anamsubiri mwenye gari hili amuhoji kuhusu namna alivyobeba mzigo.
Hapa ni kazi tu mapenzi hayana nafasi katika kazi
Haya yalikuwa ni maandamano ya wanaume kupinga kuchomolewa fedha kienyeji na wake zao
Wanasiasa vigogo wakipata tiba ya kikombe cha babu mwasapile
Nimeipenda sana picha hii,inaonyesha kwamba vijana hawa kweli wanapendana.
Picha iliyochakachuliwa(sio picha halisi) ya mzee mwasapile

Jumapili, 18 Novemba 2012

TAFITI: MATUMIZI YA MTANDAO YANAIMARISHA KAZI ZA UBONGO KWA WAZEE





  • Utafiti uliofanywa hivi karibuni nchini Marekani unaonyesha kwamba matumizi ya mtandao (internet) kwa wazee yanaimarisha utambuzi (cognition) na kazi za ubongo wao. Utafiti huu ulihusisha wazee wa jinsia zote wenye umri kati ya miaka 55 na 78. Wazee hawa waligawanywa katika makundi mawili. Moja halikutumia mtandao na kundi jingine lilitumia mtandao mara kwa mara.
  • Matokeo yalionyesha kwamba kazi za ubongo wa wazee katika kundi ambalo lilikuwa linatumia mtandao mara kwa mara ziliimarika zaidi kuliko za wazee katika kundi ambalo halikutumia mtandao. Mabadiliko makubwa yalionekana katika sehemu za ubongo zinazoshughulika na kumbukumbu (memory), lugha, kusoma na upambanuzi. 
  • Matokeo haya yamewafurahisha wanasayansi na wanasema kwamba pengine matumizi ya mtandao yanaweza kuwa silaha mojawapo dhidi ya magonjwa yanayosababishwa na upotevu wa kumbukumbu na utambuzi kama vile Alzheimer.
  •  
  • Sina uhakika kama kweli wazee wa Kiafrika wanahitaji mtandao kuimarisha kazi za ubongo wao. Mimi nadhani kwamba michezo kama vile bao, drafti na hata kuhesabu ng’ombe wanaporudi nyumbani kila jioni ni mazoezi tosha yanayoweza kusisimua kazi za ubongo, mazoezi ambayo yamesaidia kuwafanya wazee wengi wa Kiafrika kubakia makini kiutambuzi (cognitively) hata katika umri mkubwa. Sijui kama tulikuwa na wagonjwa wengi wa Alzmeimer barani Afrika kabla ya hili wimbi jipya la utandawazi tunaolishuhudia kwa sasa. Isitoshe, tulikuwa tunakula vyakula vya kiasili na mfumo wetu wa maisha ulituwezesha kufanya kazi sana. Sasa mambo yamebadilika sana na pamoja nayo magonjwa ya moyo, saratani, kiharusi na si ajabu "dementia" na Alzheimer sasa yanatuandama.