Jumapili, 20 Agosti 2017

TUNAFANYAJE ILI TUWEZE KUSIFU IPASAVYO?



Ufunguo mkuu katika eneo hili ni shauku, au kiu ya kumsifu Mungu,
“Kama ayala aionevyo shauku mito ya maji, vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu wangu. Nafsi yangu inamwonea kiu Mungu, Mungu aliye hai, lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu? Machozi yangu yamekuwa chakula change mchana na usiku, pindi wanaponiambia mchana kutwa yuko wapi Mungu wako?” (Zaburi 42:1- 3)

Inapatikana?

”Nafsi yangu kwa nini kuinama na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, aliye afya ya uso wangu, na Mungu wangu.

Nafsi yangu imeinama ndani yangu kwa hiyo nitakukumbuka, toka nchi ya Yordani, na Mahermoni, na toka kilima cha Mizari.

Kilindi chapiga kelele kilindi kwa sauti ya maboromoko ya maji yako, gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu.
Mchana Bwana ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami, naam maombi kwa Mungu aliye uhai wangu.
Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, kwa nini umenisahau? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?”
Watesi wangu hunitukana mithili ya kuniponda mifupa yangu pindi wanaponiambia mchana kutwa Yuko wapi Mungu wako?
Nafsi yangu, kwa nini kuinama, na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; kwa maana nitakuja kumsifu, aliye afya ya uso wangu na Mungu wangu. (Zaburi 42:5-11)
Kwenye nafsi Zaburi 63:1-11;66: 1-7, Mithali 16:3, Marko 12:30 kusifu kunaweza kuwa;-

a. Kusifu kwa kutumia sauti,
-     Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana Zaburi Zaburi 145:21.
-     Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai, midomo yangu itakusifu (Zaburi 63:3
-     Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote, imbeni utukufu wa jina lake. (Zaburi 66: 1-2)
-     Mpigieni Bwana vigelegele. (Zaburi 33:1a)  

b. Kusifu kwa vitendo.
-     Enyi watu wote mpigieni makofi. (Zaburi 47:1a)
-     Msifuni kwa mvumo wa baragumu,
-     msifuni kwa kinanda na kinubi
-     msifuni kwa matari na kucheza
-     msifuni kwa zeze na filimbi,
-     msifuni kwa matoazi yaliayo,
-     msifuni kwa matoazi yavumayo sana. (Zaburi 150:3-5)
-     Kwa jina lako nitainua mikono yangu. (Zaburi 63:4)

“Ndivyo Israeli wote walivyopandisha sanduku la agano la Bwana kwa shangwe na kwa sauti ya tarumbeta, na kwa baragumu, na kwa matoazi, wakipiga kwa sauti kuu kwa vinanda na vinubi.

Hata ikawa, sanduku la agano la Bwana lilipofika mjini kwa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi, akicheza na kushangilia, akamdharau moyoni mwake”.


MATENDO MBALIMBALI YA KUABUDU
-Kushukuru kwa midomo yetu (kuimba au kusema kwa midomo yetu.
-     Kutenda mema kwa kushirikiana.
-     Kuanguka mbele za BWANA ili kunyenyekea.
-     Kupiga vyombo mbalimbali,
-     Shangwe na upigaji wa vyombo
-     Kuinua mikono.
-     Kupiga magoti mbele za Bwana
-     Kucheza kwa nguvu zote
-     Kwa kucheza.
-     Muziki na kucheza.
-     Makofi.
-     Kelele za shangwe
-     Kufanya mapenzi ya BWANA
-     Kwa kutoa matoleo (zaka)

   Ukimya na mengine mengi. Kutoa kwa moyo wa ukunjufu, upandacho ndicho utakachovuna. Acheni mjue ya kuwa mimi ni Mungu, nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.

Ili uabudu lazima uwe na sababu.
1.             Mungu ni nani.
2.             Mungu amefanya nini.
3.             Kiini cha kuabudu (chanzo) Roho wa Mungu au neno la Mungu.
4.             Mwitikio (matokeo) lazima kuwe na udhihirisho udhihirisho huleta kusherehekea.
5.             Matokeo uwepo wa Mungu unaachiliwa (dhihirika) nguvu za Mungu zinaachilia.
6.             Ni lazima iwe kitu unachokifanya sio unachofanyiwa.
7.             Ikiwa hivyo hakuna atakayetoka bila kuguswa maana amejihudhurisha mbele za Bwana binafsi.
8.              Tunafanya hivyo kwa kushangaa jinsi alivyotuumba na anavyotutendea.
9.             Mungu anatafuta watu watakaofungulia (SHEKINA) utukufu na nguvu zake ili zitiririke, Yeye ni kama ngombe anaelia kwa kujaa maziwa akamuliwe.
10.         Zaburi 139:1-18 kwa kujipendekeza kwake Zaburi 139:21-22 tukisema Baba nakupenda sina Baba mwingine aliye mzuri kama wewe, baba uwe mfano mzuri, ili picha nzuri iwe.
11.         Naye atakwambia nakupenda mwanangu hata bila kikomo (Zaburi 45:1-7, 17).
12.         Ndio maana shetani anapiga vita ushirika huu. Isaya 49: 15-16,

MATOKEO YA KUABUDU.
-     Zakaria aliguswa. Luka 1: 18-20
“Zakaria akamwambia malaika, nitajuaje Neno hilo? Maana mimi ni mzee, na mke wangu ni mkongwe wa siku nyingi. Malaika akamjibu akamwambia, Mimi ni Gabrieli nisimamaye mbele za Mungu, mimi nimetumwa niseme nawe, na kukupasha habari hizi njema. Na tazama! Utakuwa bubu, usiweze kusema, mpaka siku ile yatakapotukia hayo, kwa sababu hukuyasadiki maneno yangu nayo yatatimizwa kwa wakati wake.”

Sifa na kuabudu katika roho na kweli. Angalia katika kitabu cha 1nyakati 16:1-36. Azimia kuthamini (kuabudu) utaona milango imefunguka Marko 16: 1-8

Kuna nguvu za ajabu sana angalia katika kitabu cha Matendo 16:25-34 utaona nguvu iliyowatokea Paulo na Sila hadi misingi ya gereza ikatikisika. Kuna pendo la ajabu, uponyaji, wokovu, Luka 7:36-50 mwanamke Malaya aliuona upendo wa ajabu wa Yesu akampaka mafuta yenye marashi. Kuna utukufu wa Mungu (nguvu, fahari yake, uweza wake, uzuri wake n.k) Ufunuo 7:9-12.

Kuna utakaso, utakatifu Isaya 6:1-7. Kuna kumfahamu Mungu 2Nyakati 20:14-30 Mungu hupata fahari yake (utashi wake) Ezekieli 28:11-15

KUABUDU.

Katika kamusi ya kiyunani LATREIA kumtolea Mungu (sadaka) Warumi 12:1, Waebrania 9:6 Kumtumikia kwa hiari kama mtumishi AU PROSKYREA ni kujinyenyekesha kwa kujitoa, 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni